Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,127
- 35,138
Mwanzoni (wakati Magufuli akiwa bado hai) ilikuwa kama tetesi lakini sasa kila kitu kiko wazi kuwa Chato imejipanga kuhakikisha inakuwa mkoa, tena mkoa mkuu na imara kwa gharama za kuimega Kagera na Geita.
Kwa sasa ni vuta nikuvute, kila upande unavutia kwake, wezee wa mkoa wa Kagera wakisema; hawako tayari kuona historia, tamaduni na uchumi wa mkoa wa Kagera ukipotezwa kimakusudi chini ya mpango wa kuumega mkoa wa Kagera ili kuundwa mkoa mpya wa Chato. Na wakati huo huo, viongozi wa wilaya ya Chato wakijiapiza kuwa iwe isiwe, mkoa wa Chato lazima uundwe kwa gharama ya kumega wilaya muhimu za mkoa wa Kagera, Geita na Kigoma.
Chini ya sera za CCM za siku zote za kuwagawa watu kimaeneo na kitamaduni ili iwe rahisi kuwatawala (chini ya mwamvuli wa kuunda mikoa na wilaya mpya), mpango huu kwa sasa huenda ukaleta maafa, chuki na visasi visivyokwisha kwa karne kadhaa ikiwa busara haitatumika.
Kwa sasa ni vuta nikuvute, kila upande unavutia kwake, wezee wa mkoa wa Kagera wakisema; hawako tayari kuona historia, tamaduni na uchumi wa mkoa wa Kagera ukipotezwa kimakusudi chini ya mpango wa kuumega mkoa wa Kagera ili kuundwa mkoa mpya wa Chato. Na wakati huo huo, viongozi wa wilaya ya Chato wakijiapiza kuwa iwe isiwe, mkoa wa Chato lazima uundwe kwa gharama ya kumega wilaya muhimu za mkoa wa Kagera, Geita na Kigoma.
Chini ya sera za CCM za siku zote za kuwagawa watu kimaeneo na kitamaduni ili iwe rahisi kuwatawala (chini ya mwamvuli wa kuunda mikoa na wilaya mpya), mpango huu kwa sasa huenda ukaleta maafa, chuki na visasi visivyokwisha kwa karne kadhaa ikiwa busara haitatumika.