share
JF-Expert Member
- Nov 22, 2008
- 6,062
- 10,459
Bila kificho wala unafiki ningekushauri ndugu yangu Charles Hilary kuwa huu ndio wakati wako sasa kuwatumiakia watanzania baada ya kustaafu utangazaji kwa mafanikio makubwa, utashi na busara yako bado tunaihitaji watanzania ituletee faida.
Hivyo basi ni wakati sahihi wa kuchukua form ya Ubunge na jimbo linalo kufaa ni Kibamba kwa kuwa ndipo unapoishi na unakubalika sana.
Ushauri kwa CCM kama kweli mna nia ya dhati ya kulichukua Jimbo la Kibamba na kumuondoa John Mnyika basi huyu Charles Hilary ndio chagua sahihi ni mtu mwenye ushawishi mkubwa na anapendwa na wengi.
Nini maoni yenu Wana JF tunaihitaji huduma ya Charles Hilary kwenye bunge lijalo?
Na si bunge tu mana ninahakika akiingia bungeni hatokosa kuwa waziri huyu.
Umechukua buku ngapi? Nenda kanywe chai naye kama unampenda.