Lizzy mi chapati nakulaga ila sizipendi sana, na zaidi nnopenda kula mimi ni zile za unga wa atta(brown flour).
Ama chapati za maji(za upawa) apo ata 10 nafyeka tena kwa asali tu bila hata mboga yoyote.
Kwa wanaojua kula wanakwambia chapati za kusukuma mwenziwe supu ya kuku wa kienyeji na chai ya maziwa iloungwa kwa fresh vanilla.
Karibu kitaani kwetu utapata za kutosha...
Za unga wa atta, ule wanaita ngano nzima.Angel Nylon angalau unapenda za maji. Zile ie napenda kupikia watu wengine tu ila kula sipendi. . .
Kuna mtu mmoja tu alikua akipika nakula na kipindi hicho nilizipenda sana ila tangu afariki hataaa sitamani.
Alafu hizo za brown sijawahi kula. . .nazo ni nzuri?
Msije tupikia chapati ngumu kama ngozi tu.