Chanzo cha umasikini Afrika sio viongozi ila ukosefu wa ujuzi wa sayansi na teknolojia

Kwa taarifa yako maswali ninayouliza haimaanishi nakulazimisha uyajibu. Hii ni mitego ya kujenga hoja ambazo huwezi kuzijibu na ukijaribu kujibu lazima utapotea.

Kiufupi tu ni kwamba nilitaka kukuonesha lwamba haihitaji kutoa muda zaidi kwa uongozi wa JPM ili tuhukumu kama hali ya uchumi itatengemaa au umasikini utaendelea kutamalaki kwasababu tayari anawekeza kwenye ujenzi unaoteketeza matrilioni ya shilingi badala ya kujikita kwenye maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Lakini ni muhimu kukumbuka kwamba hadi sasa ambapo muhula wake wa kwanza unaelekea ukingoni, hakuna hata mradi mmoja uliokamilika ua hata nusu. Hii maana yake ni kwamba miradi hii itaendelea kuteketeza fedha hadi muhula wake wa mwisho na hakuna kitakachokamilika. Kwamaana hii nikisema JPM amechemsha na kwamba hataweza kuvunja rekodi ya kikwete ya kukuza uchumi kwa zaidi ya 8%.

Zaidi nataka nirekebeshe pale uliposema uimara wa thamani ya sarafu ndo kigezo cha hali nzuri ya chumi na eti kwavile kasi ya kushuka kwa thamani ya shilingi chini ya uongozi wa JPM ni ndogo ukilinganisha na enzi za JK maana yake uchumi umeimarika, si kweli.

Kwa taarifa yako tu ni kwamba sarafu (Dinar) za Kuwait, Bahrain na Oman zinaongoza kwa kuwa na kuwa na thamani kubwa duniani na zinashika nafasi tatu za kwanza katika orodha ya sarafu 10 zinazoongoza kwa thamani hapa duniani. Je, unatakata uchumi wa nchi hizi uko juu kuliko Marekani, China na Japani, Ujerumani na Uingereza nchi ambazo ni nambari moja kwa uwezo wa sayansi na teknolojia?

Naomba uwasiliane tena na rafiki zako wanaosomea uchumi Uingereza wakuelekeze vizuri kuhusu uchumi.
Sikiliza kijana, mie sikutoa mada hii kujadili rais yeyote ila sie wote waafrika na ujinga wetu wa sayansi na tachnolojia tunaoukimbia kwa kuwatupia lawama viongozi wetu na kucheza siasa, siasa haitajenga madaraja na reli ila mchina kama sio siye. Ukileta hoja ya Magufuli sikujibu wala sisomi kama nilivyodharau jibu lako refu baada ya sentensi ya kwanza, sina muda huo wa kuongelea hayo.
 
Sawa mzee, ila mie nazungumzia mashine za viwanda, engine za magari, ndege, meli, Drones, hata mashine za kutengenezea nguo, dawa hata za mashambani. Pia uwezo wa kutengeneza barabara, madaraja, reli n.k.
Nakuelewa sana mkuu.
Ili twende kwa kasi, tunahitaji technology (ndiyo machine unazosema) na know-how kwenye yote hayo.
Bila investment financing kwa ajili ya kutengeneza products za pamba kama nyuzi, pamba za hospitali, vitambaa, nguo, animal feeds; yote haya hayatatokea.

Hivyo basi, tungeanza na investment financing kwenye vitu vinavyozalisha kwa vingi ikuwamo agro-inputs (mbolea na viwatilifu) na kuongeza ongeza thamani kwenye output.
Then kodi inayopatikana inakuwa kubwa. Na kwenye majenzi ya miradi mikubwa kama reli, meli na barabara nako pia tunaweza kuingia ili ku-service usafirishaji wa bidhaa za kilimo na output ya madini tunayochimba na kuyachakata kwenye ubora.
 
Nakuelewa sana mkuu.
Ili twende kwa kasi, tunahitaji technology (ndiyo machine unazosema) na know-how kwenye yote hayo.
Bila investment financing kwa ajili ya kutengeneza products za pamba kama nyuzi, pamba za hospitali, vitambaa, nguo, animal feeds; yote haya hayatatokea.

Hivyo basi, tungeanza na investment financing kwenye vitu vinavyozalisha kwa vingi ikuwamo agro-inputs (mbolea na viwatilifu) na kuongeza ongeza thamani kwenye output.
Then kodi inayopatikana inakuwa kubwa. Na kwenye majenzi ya miradi mikubwa kama reli, meli na barabara nako pia tunaweza kuingia ili ku-service usafirishaji wa bidhaa za kilimo na output ya madini tunayochimba na kuyachakata kwenye ubora.
Ni kweli tunahitaji investment, lakini technology kwanza kabla hujapata capital, hivi ndivyo wanavyofanya wenzetu, wanatoa au present idea zao baada ya kuzifanyia kazi za kisanyansi, kisha wanaomba pesa za kuendesha mradi.
 
Ni kweli tunahitaji investment, lakini technology kwanza kabla hujapata capital, hivi ndivyo wanavyofanya wenzetu, wanatoa au present idea zao baada ya kuzifanyia kazi za kisanyansi, kisha wanaomba pesa za kuendesha mradi.
Kama kuna good feasibility study ya uhakika wa soko; kwa mfano Tanzania sukari inatengenezwa yote inauzika na bado tuna uhitaji wa zaidi ya tani 50,000

Kwa lugha rahisi ukipata dhamana ya bank ya kilimo au BoT kununua technology kwa ajili ya kununua kulima miwa au sugar beet kwa ajili ya kiwanda cha sukari; baada ya mauzo unakuwa na nafasi ya kurejesha mkopo kupitia mauzo ya sukari.

Katika uchumi wa soko, uhakika wa soko unaweza kumfanya mwekezaje apate mkopo wa uwekezaji
 
Kama kuna good feasibility study ya uhakika wa soko; kwa mfano Tanzania sukari inatengenezwa yote inauzika na bado tuna uhitaji wa zaidi ya tani 50,000

Kwa lugha rahisi ukipata dhamana ya bank ya kilimo au BoT kununua technology kwa ajili ya kununua kulima miwa au sugar beet kwa ajili ya kiwanda cha sukari; baada ya mauzo unakuwa na nafasi ya kurejesha mkopo kupitia mauzo ya sukari.

Katika uchumi wa soko, uhakika wa soko unaweza kumfanya mwekezaje apate mkopo wa uwekezaji
Sawa, lakini tunazungumzia teknolojia ya viwanda, ujenzi na kutengeneza vyombo vya usafiri na mawasiliano etc.
 
Tatizo kelele zote huwa zinaishia humu Jukwaani Wala hata nje hazifiki....
Kuna wanaojadiliana nje ya JF, hilo nalo litasaidia kuamsha watu, kwani utajiri wa mmoja mmoja ndiyo utajiri wa taifa kutokana na kodi, na ujuzi na utaalamu unaleta utajiri, na ujuzi huu ni sisi wananchi kuujua siyo viongozi sababu wao ni wanasiasa sio wataalamu.
 
Sayansi gani unaongelea mkuu. Afrika tuna sayansi na techno ya hali juu kupambana na upinzani kuhakikisha hawapumui, nje na ndani ya bunge
Pia sayansi ya kuiba kura
Mtu anachaguliwa tu, kitu cha kwanza anaapa kuua upinzani.
Hizo ndo sayansi zetu
 
Tatizo kelele zote huwa zinaishia humu Jukwaani Wala hata nje hazifiki....
Jukwaa hili ukiandika upuuzi, kudhalilisha au kutukana wakubwa; haichukui muda unakamatwa hasa kama ID ya jina lako linafahamika.

Ni heri hata mambo ya maana kwa mustakabali wa nchi yetu kusema. Huenda anaweza kutokea mtu mwenye nia njema na fikra mbadala akashikiana nasi kwenye kuijenga Tanzania kwa kuwekeza kwa kuanza na wazawa.
 
Mtoa mada sema tu umekusudia kumsema JK kwa husda uliyonayo kutokana na mafanikio yake katika utendaji wake ukilinganisha na JPM. Enzi za JK uchumi ulishawahi kupanda zaidi ya 8% kiwango ambacho JPM hatakaa akifikie pamoja na kujifanya kuwa "mjenga uchumi".

Lakini ukweli ni kwamba ukuaji wa uchumi wetu kwa sasa ni chini ya 6% kwa mujibu wa IMF taarifa ambazo JPM hataki zichapishwe. Ingawa waziri wa wa Fedha na Minpango ameonesha "mgando" katika ukuaji wa uchumi kwa kulinganisha miaka miwili iliyopita (7%) ni uongo, uchumi umedidimia zaidi bali serikali inajaribu kufanya "balance" kuficha uhalisia wa kushuka kwa uchumi kujilinda kisiasa.

Tukirudi kwenye hoja kwamba tatizo la umasikini (uchumi mbaya) ni kutokana na ukosefu wa teknolojia na si uongozi, hapa ni dhahiri unakusudia "kumkinga" JPM na lawama za anguko la kiuchumi ambalo tunapitia kwa sasa. Kwamba tatizo si JPM bali ni "asili" yetu ya kukosa maarifa ya kisayansi. Unapotosha.

Kumbuka, dhima ya uongozi ni kutoa dira katika maendeleo ya nchi. Tofauti ya maendeleo ya kiuchumi baina ya nchi tajiri na masikini (Africa) inatokana na tofauti ya kiwango cha uwekezaji (support) katika utafiti na maendeleo (R&D) ambayo ndo msingi wa teknolojia na uchumi wenyewe. Serikali (uongozi) za nchi zenye maendeleo makubwa zinawekeza zaidi kwenye R&D kuliko nchi masikini ambazo huwekeza zaidi katika vitu (structures).

Hebu jiulize mwenyewe serikali hii ya JPM imetenga kiasi gani cha fedhs katika bajeti yake kwa ajili ya R&D? Lakini kama kweli unaamini tatizo la umasikini si uongozi bali ukosefu wa teknolojia, je, unatarajia Tanzania itaondokana na umasikini uliopo kwa kuwekeza matrilioni ya shilingi kwenye miradi ya ujenzi wa SGR na JNHPP? Hivi anayeamua fedha za nchi zitumike zaidi kwenye miradi ya ujenzi badala ya R&D si viongozi?

Je, unafahamu kwamba changamoto ya mlipuko wa ugonjwa wa korona inaweza kuwa ni chachu ya kuwekeza kwenye utafiti na maendeleo? Je, serikali imetenga fedha kiasi gani na maelekezo gani hadi sasa kusapoti wanasayansi ili wafanye tafiti na kuweza kuzalisha vipimo, dawa, kinga na vifaa tiba dhidi ya korona na magonjwa mengine?
Umesema yote mkuu.. viongozi wengi ni wapumbafu.. yaani hawafaham umuhim wa R&D.. hawajui kuwa hata hizo SGR na Rufiji zinahitaji R&D.. ili uendelvu uwepo.. utaona kuwa TZ imefeli katika projects nyingi kwa kukosa hiyo element. Unakuta kila kitu kinaongozwa kwa mihemko bila kufuata matokeo ya utafiti.. hata serikaliiliyopo ipo ipo tu. Yaani ni shida tupu na hatuwezi kuendelea kwa mtindo huu
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom