Swahilian
JF-Expert Member
- Apr 28, 2009
- 591
- 66
Kwanza, salaam za dhati ni kwenu ninyi ndugu, nimetafiti kidogo juu ya neno ASILI na CHANZO lakini bado nakanganyika kimatumizi hadi inafika wakati naamua kuyatumia popote tu hali ambayo imenipa sononeko la moyo hasa ninatumia hii lugha yangu itamu ya kiswahili, nimepata kusikia mf. chanzo cha mziki huu ni... au asili ya neno hili ni.... tafadhali nipeni fasili na matumizi ya maneno hayo? tupigeni mbizi jamani bahari ya lugha ni ndefu na pana!!