Chanjo ya Iran ya COVID-19 inaweza kukabiliana na 'kirusi cha Uingereza'

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
8,816
17,405
Chanjo ya Iran ya COVID-19 inaweza kukabiliana na 'kirusi cha Uingereza'

Jan 30, 2021 12:16 UTC

Chanjo ya Iran ya COVID-19 au corona ambayo majaribio yake yanakaribia kumalizika ina uwezo wa kukabiliana na aina mpya ya kirusi cha corona ambacho kimeibuka Uingereza.

Hayo yamedokezwa na Dkt. Hassan Jalili mkuu wa timu ya utengenezaji chanjo ya Iran katika Idara ya Utafiti ya Taasisi ya Utekelezaji wa Maagizo ya Imam Khomeini (MA).

Itakumbukwa kuwa mnamo Disemba 29 mwaka 2020 chanjo ya corona iliyotengenezwa na shirika la Barakat la Iran ilifanyiwa majaribio kwa mwanadamu. Chanjo hiyo ambayo inajulikana kama COVIRAN Barekat imetengenezwa na Shirika la Barakati ambalo liko chini ya Idara ya Utafiti ya Taasisi ya Utekelezaji wa Maagizo ya Imam Khomeini (MA).

Akizungumza na Shirika la Habari la Tasnim, Dkt. Jalili amesema majaribio yaliyofanywa yanaonyesha kuwa plasma ya damu ya watu waliodungwa chanjo ya COVIRAN Barekat wakati wa majaribio, inaweza kusambaratisha kabisa aina mpya ya kirusi cha COVID-19 kutoka Uingereza.

Mbali na chanjo ya COVIRAN Barekat iliyoundwa Iran kikamilifu, Iran iko mbioni kutengeneza chanjo zingine za corona ndani ya nchi na pia kwa ushirikiano na washirika wa kigeni. Aidha Iran pia itaagiza baadhi ya chanjo zake za corona kutoka nje ya nchi.

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuingizwa Iran chanjo kutoka Marekani na Uingereza ni marufuku lakini ameruhusu kuagizwa chanjo kutoka nchi zingine zenye kuaminika.

Tayari Iran imeshatangaza mpango wa kununua chanjo ya corona ya Russia inayojulikana kama Sputnik V.

4bxxfc77b228d01sz69_800C450.jpeg
4bvgb5312f9b8d1shla_800C450.jpeg
 
Sasa huyu jamaa ndio atakapo wapukutisha wazungu. Mara unakuta inaweza kupambana na kirusi hichi kipya cha uingereza, ila baada ya miaka 10 inageuka sumu mwilini.

Tusije kushangaa Iran akaja kuwa mtetezi wetu wa Africa, hii chanjo ikawa madhubuti kwetu kuliko za kina Bill Gates wanaotaka kutupunguza Africa (Depopulize Africa To Save Europe).
 
Sasa huyu jamaa ndio atakapo wapukutisha wazungu. Mara unakuta inaweza kupambana na kirusi hichi kipya cha uingereza, ila baada ya miaka 10 inageuka sumu mwilini.

Tusije kushangaa Iran akaja kuwa mtetezi wetu wa Africa, hii chanjo ikawa madhubuti kwetu kuliko za kina Bill Gates wanaotaka kutupunguza Africa (Depopulize Africa To Save Europe).
unadhani ni rahisi kihivyo kutengeneza kitu kama hicho na kupita undetected ?

Binadamu tunawapa credit kubwa sana mkuu, na ukifuatilia hata happenstance nyingine huwa zinafanikiwa kama bahati tu sio programmed
 
Hii sasa ndio tunaona umuhimu wa kuwa na wataalamu wako (nchini - wazalendo) ambao ni competitive

Ndio maana tunazidi kuomba nchi hii tuache kuwekaza na kuwajali sana wanasiasa, hatutofika

Tuwekeze kwa wataalamu, kuwekeza kwa wataalamu ni uchumi, ni maisha, ni maendeleo, ni uendelevu

Sasa wabunge na mawaziri wanalipwa fedha nyingi ambazo daktari, mwalimu, bwana mifugo, bwana shamba wala IT hapati hiyo fedha hata siku akistaafu.

Tuwekeze kwa wataalamu yaani kizazi chetu kione mbeleni kuwa ni fahari mtu kuwa mwalimu au daktari au muhandisi ua IT au nesi badala ya kuwa mbunge au waziri au diwani au sijui nani?

Hili wazo ni kwa nchi ambayo ipo serious kupata maendeleo au kama tunapenda blaaa blaaa basi tuendelee hivi hivi eti mbunge anmafukuzisha kazi mkurugenzi au daktari au mwalimu aiseh
 
Sasa huyu jamaa ndio atakapo wapukutisha wazungu. Mara unakuta inaweza kupambana na kirusi hichi kipya cha uingereza, ila baada ya miaka 10 inageuka sumu mwilini.

Tusije kushangaa Iran akaja kuwa mtetezi wetu wa Africa, hii chanjo ikawa madhubuti kwetu kuliko za kina Bill Gates wanaotaka kutupunguza Africa (Depopulize Africa To Save Europe).
Hayo ni matamshi ya Billgets ya awali na ya wakati huu kwenye Machano yaoo
FB_IMG_16119272767327868.jpg
 
Ila twende mbele turudi nyuma wairan wanajitutumua Sana.
Ni aibu Afrika mzima sijaskia nchi inayojaribu kutengeneza chanjo hii kwa uwezo wa wataalam wa ndani!
Hii inatisha vibaya
 
hata wewe unaweza ukaingia field mkuu; tofauti yao na sisi ni (investment ) time and money....., ila ubongo ni ule ule..., tatizo asilimia kubwa ya bongo zetu zinawaza vitu visivyo na tija
Ubongo wa mwafrika ndio tatizo mkuu angalia viongozi wanakuongoza uendelee na kwingineko
 
Hamna chanjo hapo hizo ni tambo tu kwani nani haijui Iran?
Vichupa chupa kama vya Madagascar.

Ngoja na mimi nitafute vichupa chupa nitie gongo halafu nibandike stickers Vaccine vaccines.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom