Chanjo, teknolojia ya kiafrika na simulizi ya Onesimus, mtumwa wa Kiafrika aliyeiokoa dunia

Aug 22, 2015
26
46
Mnamo mwanzoni mwa miaka ya 1700, mji wa Boston, Massachusetts kama ilivyokuwa kwa dunia nzima kipindi hiko, ulikumbwa na ugonjwa mbaya wa Ndui uliosababisha vifo vya watu wengi. Inakadiliwa watu zaidi ya milioni 300 walifariki kwa ugonjwa wa Ndui duniani kote.

Ugonjwa wa Ndui kipindi hiko ulikuwa kama hukumu ya kifo kwa waliougua na hata wagonjwa wachache waliopona waliachwa na makovu na vilema kwenye miili yao.

Lakini mnamo mwaka 1716, mtumwa wa kiafrika aitwaye Onesimus alimwambia mmiliki wake, bwana Cotton Mather, kuwa anafahamu siri ya ugonjwa wa Ndui. Onesimus alieleza kuwa alipokuwa Afrika alifanyiwa upasuaji mdogo na kupewa sehemu ya ugonjwa kwenye mwili wake na hivyo kumsababishia kinga dhidi ya kuugua tena ugonjwa huo.

onesimus 1.jpg

Upasuaji huo mdogo ulijumisha kusuguliwa juu ya ngozi kwa maji maji kutoka kwenye vidonda vya mgonjwa wa Ndui na hivyo kumfanya kuwa na kinga ya ugonjwa huo.

Mather, alishangazwa na simulizi hiyo ambapo ilimbidi kufanya uchunguzi kwa watumwa wengine wa kiafrika ambao pia walimthibitishia juu ya ukweli wa tiba hiyo. Simulizi ya tiba hii kutoka kwa mtumwa wa kiafrika haikupata ushawishi mkubwa kwenye jamii ya watu weupe ila Mather aliendelea kuhubiri juu ya teknolojia hii.

Mnamo mwaka 1721, Mather pamoja na daktari mzungu Boylston Zabdiel walifanikiwa kujaribu teknolojia hiyo kwa mara ya kwanza ambapo walianza na mtoto wa Mather na baadhi ya wakazi wa Boston. Tiba hiyo ilionyesha mafanikio makubwa sana kwani kati ya watu 242 waliopata tiba hiyo ya chanjo ni watu 6 tu waliofariki kwa ugonjwa wa Ndui ikilinganisha na uwiano wa vifo 7 kwa kila wagonjwa 40 bila ya chanjo.

Mwaka 1796. Edward Jenner alifanikiwa kutengeneza chanjo ya kwanza rasmi kutokana na kirusi cha Ndui wa ng’ombe na hatimaye chanjo ya Ndui ikawa ni ya lazima kwa wakazi wote wa Boston, Massachussets.

Kutokana na mafanikio hayo na maboresho mbalimbali, mwaka 1980, shirika la afya duniani WHO walitangaza kuwa ugonjwa wa Ndui umetokomezwa rasmi katika uso wa Dunia.

Mwaka 2016, Onesimus alipewa heshima ya mtu bora wa wakati wote kwenye mji wa Boston. Mengi hayasemwi juu ya kifo cha Onesimus ila alifanikiwa kununua uhuru wake mwenyewe kwa kumlipa mmiliki wake kiasi sawa cha kuweza kununua mtumwa mwingine.

Leo hii, zaidi ya miaka 300 baadae, tiba na teknolojia ya chanjo imepiga hatua kubwa ambapo magonjwa kama Surua na Polio ni magonjwa yanayokaribia kutokomezwa kabisa katika uso wa dunia.

Chanjo ni dawa ya kibaologia ambapo kipande cha ugonjwa au ugonjwa uliofubazwa uingizwa kwenye mwili wa binadamu kama namna ya kujenga kumbukumbu kwenye kinga ya mwili dhidi ya ugonjwa fulani.
 
Ahsante kwa Bandiko hili, ingawaje ningependa kujuwa kwa miaka hiyo ya 1700 ni Nchi gani ya Afrika ilikuwa na hospital ya kuweza kufanya upasuaji wa namna hiyo?

Na je, kama tuliweza kufanya hivyo kwa miaka hiyo hapa kati kati iliitokea nn hadi tukashindwa kuendeleza huo Utalaamu wa kutengeneza Chanjo zetu?
 
Afrika ndo kila kitu angalia pyramid na mafarao miaka 3500 walishaweza kufanya anbayo hadi leo sisi hatujui yamefanyikaje .....
 
Waafrika tukitaka tunaweza ila hatuna confidence kabisa
Kila kitu tunasema tunaonewa gele mara wazungu mabeberu nk
Tuamke sio kulia tu na tunaweza sana
 
Ahsante kwa Bandiko hili, ingawaje ningependa kujuwa kwa miaka hiyo ya 1700 ni Nchi gani ya Afrika ilikuwa na hospital ya kuweza kufanya upasuaji wa namna hiyo?
Na je, kama tuliweza kufanya hivyo kwa miaka hiyo hapa kati kati iliitokea nn hadi tukashindwa kuendeleza huo Utalaamu wa kutengeneza Chanjo zetu?
Wazungu walipofika hapo Uganda kwenye Buganda Kingdom, walistaajabu kukuta watu wakifanyiwa upasuaji na tiba mbalimbali. Shida ni kwamba tulikuwa hatudocument vitu.
Sidhani kama tulikuwa mbele ya wazungu, kama tungekuwa hivyo wasingetutawala isipokuwa kuna sehemu za afrika zilikuwa na teknolojia na maarifa ya mbele sana.
Wazungu hawakupendi kutoa any creditd kwa waafrika
 
Asante sana....
Ngoja nikachukue majimaji yenye virusi vya ukimwi nijipatie kinga.
Nita leta mrejesho....
 
Back
Top Bottom