Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,500
- 9,279
Wanasayansi kutoka nchini Italia wamegundua chanjo dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI "AIDS" (Acquired Immune Deficiency Syndrome / Upungufu wa Kinga Mwilini).
Kinga hio imefanikiwa kupunguza mwilini idadi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukımwi "HİV" kwa asilimia 90.
Timu ya utafiti huu iliongozwa na Barbara Ensoli ambaye amefahamisha yafuatayo kuhusiana na matokeo ya utafiti huo:
Utafiti wao mpaka ulipofikia imethibitika kwamba chanjo waliyoitengeneza imetoa majibu ambayo waliyakusudia, yaani kuwa na uwezo wa kutoa kinga dhidi ya virusi vya Ukimwi.
Na cha zaidi imefanikiwa kupunguza kiwango cha virusi vya Ukimwi kwa asilimia 90.
Chanjo hiyo ambayo bado ipo kwenye majaribio inailenga aina maalum ya "protein " ijulikanayo kama HIV-1 Tat.
Protein hii ni muhimu katika maisha ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi.
Matokeo ya utafiti huu yamechapishwa katika jarida la Frontier in Immunology.
TRT
Kinga hio imefanikiwa kupunguza mwilini idadi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukımwi "HİV" kwa asilimia 90.
Timu ya utafiti huu iliongozwa na Barbara Ensoli ambaye amefahamisha yafuatayo kuhusiana na matokeo ya utafiti huo:
Utafiti wao mpaka ulipofikia imethibitika kwamba chanjo waliyoitengeneza imetoa majibu ambayo waliyakusudia, yaani kuwa na uwezo wa kutoa kinga dhidi ya virusi vya Ukimwi.
Na cha zaidi imefanikiwa kupunguza kiwango cha virusi vya Ukimwi kwa asilimia 90.
Chanjo hiyo ambayo bado ipo kwenye majaribio inailenga aina maalum ya "protein " ijulikanayo kama HIV-1 Tat.
Protein hii ni muhimu katika maisha ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi.
Matokeo ya utafiti huu yamechapishwa katika jarida la Frontier in Immunology.
TRT