Chanika umwinyi ulipitiliza nadhani fundisho wamepata sasa

junky

JF-Expert Member
May 11, 2017
413
976
Kata nyingi Dar es salaam ukiacha mitaa ya kishua kama masaki,osterbay,msasani,upanga na nyinginezo zinazofanana na maeneo hayo pia kuna kata za kistaarabu yaani za wastani kidogo zina afadhali na unafuu


Lakini asilimia kubwa za kata jijini Dar ni mchanganyiko ya wa walionacho na wasio nacho ,sehemu nyingi hapa dar kuna watoto wanaoitwa number D

Number D ni vijana wanaochipukia na kupenda usela hivyo wamebatizwa jina la number D..maeneo mengi dar watoto kusoma kwao mwisho form 4 na wengi hio form 4 hawafiki na shule zao ni shule za kata na tunafahamu vijana wengi wanaosoma shule za kata ni nadra kuvuka na kufaulu


Ndipo ukienda kata nyingi unakuta vijana wengi wanakaa maskani na kusikiliza nyimbo za singeli na kuvuta bangi siku hizi kuna maskani nyingi za mabinti wadogo wanavuta bangi sasa hawa wa kiume ndio usiseme na wengi wanapenda usela na usiku wanatoka mchomoko aidha kwenda kuvunja au kukaba sababu wengi hawafanyi kazi na hawataki kazi

Ndio maana kuna kata nyingi saizi wameweka sungusungu ili kulinda mtaa na wakabaji na wanaovunja na kuiba,saizi ukienda sehemu kibao usiku utaona unasimamishwa na kuanza kuhojiwa

Lakini kata ambazo hazina sungusungu ni rahisi kuwa wahanga sababu wezi wa mchomoko wanajua rada za mitaa na hivyo sehemu tulivu au za kimwinyi ni rahisi kuingia na kuiba huku ninapoishi kulikuwa na umwinyi sana ikawa kila siku watu wanaibiwa mwisho wa siku vijana wakajikusanya na kuanza doria kimya kimya na kufanikiwa kuwadaka wanaonyata usiku na kuiba na kuwaadabisha tokea hapo wezi wakawa hawagusi mtaani wanapaogopa


Maeneo mengi dar kuna hawa number D na wako wengi kazi yao ni kuitana unakuta mtaa una sura ngeni ya vijana wengi sababu wenyeji ndio wanaowaleta hao marafiki wa maskani za mbali na huwa ni rahisi kufanya michongo

Kimara palikuwa panaonewa sana mwisho wa siku vijana wengi wamekufa ,tabata kuna vijana wengi wameuliwa kikatili na sungusungu

Yaliyotokea chanika yametokea maeneo mengi ,na maeneo mengi dar kuna maskani za kijinga sana na asilimia kubwa ya vijana ni wahovyo wapenda usela,matusi,watukutu na sifa za vijana hawa hufanana

Kuna eneo tandika wakisikia kijana kafanya ujinga wa kipumbavu alikuwa anafuatwa huyo mtu hadi chumbani kwake na kutolewa na kupewa adabu


Kilichotokea chanika ni umwinyi kupitiliza maana kuna sehemu palikuwa panasifika kwa usela,uhuni na kila aina ya ujinga kama Tandale na mwananyamala? Lakini vijana wa Tandale na mwananyamala wanaishia kutumia tu kwa kunywa pombe na umalaya mtaani lakini wizi wa kijinga hukuti ukifanyika kwasababu ya kanuni zilizowekwa mtaani kila mtaa kuna sungusungu mwisho wa siku wale watukutu wanaenda kuiba kata za mbali

Kwahili natumai Chanika mtajifunza ulizeni kwanini mwananyamala ,Tandale na maeneo mengine wameweza kutuliza mitaa na wakati sehemu hizo kuna wahuni wengi tu...
 
kile
Kata nyingi Dar es salaam ukiacha mitaa ya kishua kama masaki,osterbay,msasani,upanga na nyinginezo zinazofanana na maeneo hayo pia kuna kata za kistaarabu yaani za wastani kidogo zina afadhali na unafuu


Lakini asilimia kubwa za kata jijini Dar ni mchanganyiko ya wa walionacho na wasio nacho ,sehemu nyingi hapa dar kuna watoto wanaoitwa number D

Number D ni vijana wanaochipukia na kupenda usela hivyo wamebatizwa jina la number D..maeneo mengi dar watoto kusoma kwao mwisho form 4 na wengi hio form 4 hawafiki na shule zao ni shule za kata na tunafahamu vijana wengi wanaosoma shule za kata ni nadra kuvuka na kufaulu


Ndipo ukienda kata nyingi unakuta vijana wengi wanakaa maskani na kusikiliza nyimbo za singeli na kuvuta bangi siku hizi kuna maskani nyingi za mabinti wadogo wanavuta bangi sasa hawa wa kiume ndio usiseme na wengi wanapenda usela na usiku wanatoka mchomoko aidha kwenda kuvunja au kukaba sababu wengi hawafanyi kazi na hawataki kazi

Ndio maana kuna kata nyingi saizi wameweka sungusungu ili kulinda mtaa na wakabaji na wanaovunja na kuiba,saizi ukienda sehemu kibao usiku utaona unasimamishwa na kuanza kuhojiwa

Lakini kata ambazo hazina sungusungu ni rahisi kuwa wahanga sababu wezi wa mchomoko wanajua rada za mitaa na hivyo sehemu tulivu au za kimwinyi ni rahisi kuingia na kuiba huku ninapoishi kulikuwa na umwinyi sana ikawa kila siku watu wanaibiwa mwisho wa siku vijana wakajikusanya na kuanza doria kimya kimya na kufanikiwa kuwadaka wanaonyata usiku na kuiba na kuwaadabisha tokea hapo wezi wakawa hawagusi mtaani wanapaogopa


Maeneo mengi dar kuna hawa number D na wako wengi kazi yao ni kuitana unakuta mtaa una sura ngeni ya vijana wengi sababu wenyeji ndio wanaowaleta hao marafiki wa maskani za mbali na huwa ni rahisi kufanya michongo

Kimara palikuwa panaonewa sana mwisho wa siku vijana wengi wamekufa ,tabata kuna vijana wengi wameuliwa kikatili na sungusungu

Yaliyotokea chanika yametokea maeneo mengi ,na maeneo mengi dar kuna maskani za kijinga sana na asilimia kubwa ya vijana ni wahovyo wapenda usela,matusi,watukutu na sifa za vijana hawa hufanana

Kuna eneo tandika wakisikia kijana kafanya ujinga wa kipumbavu alikuwa anafuatwa huyo mtu hadi chumbani kwake na kutolewa na kupewa adabu


Kilichotokea chanika ni umwinyi kupitiliza maana kuna sehemu palikuwa panasifika kwa usela,uhuni na kila aina ya ujinga kama Tandale na mwananyamala? Lakini vijana wa Tandale na mwananyamala wanaishia kutumia tu kwa kunywa pombe na umalaya mtaani lakini wizi wa kijinga hukuti ukifanyika kwasababu ya kanuni zilizowekwa mtaani kila mtaa kuna sungusungu mwisho wa siku wale watukutu wanaenda kuiba kata za mbali

Kwahili natumai Chanika mtajifunza ulizeni kwanini mwananyamala ,Tandale na maeneo mengine wameweza kutuliza mitaa na wakati sehemu hizo kuna wahuni wengi tu.
Kile kilichotokea juzi chanika kinasikitisha sana,ila nadhani tukio lilivyotokea ndio mwanzo na wao wakaimarisha ulinzi
 
Wengine hatujui kilichotokea. Tunaomba uzi unaoelezea kilichotokea kwa ufupi.
 
Sungusungu wenyewe ni wezi kama nini. Hawako na maadili ya kazi
Kuna siku niko Moshi(Kilimanjaro) nilikuwa na washkaji zangu watano tumetoka kupiga mitungi, Ilikuwa kama saa 5 usiku,Sasa Kufika mtaa fulani hivi nikaona tochi kama tatu zimewashwa kwa pamoja, Tukagumiana na njemba ziko kama kumi na kitu hivi, hapo tayari kila mmoja wetu alikuwa anajiandaa kwa litakalotokea, SunguSungu mmoja akauliza"mchana"kuna mwamba alikuwa nyuma yangu akajibu "usiku" mara nikasikia "kaa chini,kaa chini" Tulianza kutoka nduki,Wale sungusungu wakafanikiwa kuwakamata washkaji wetu wawili, Jamaa tulivoamka asubuhi masela wakaja wameibiwa simu,walleti,na viatu na wale Sungusungu, Kuna watu wanatumia kivuli cha Sungusungu kuwaibia raia nyakati za usiku.
 
Kuna siku niko Moshi(Kilimanjaro) nilikuwa na washkaji zangu watano tumetoka kupiga mitungi, Ilikuwa kama saa 5 usiku,Sasa Kufika mtaa fulani hivi nikaona tochi kama tatu zimewashwa kwa pamoja, Tukagumiana na njemba ziko kama kumi na kitu hivi, hapo tayari kila mmoja wetu alikuwa anajiandaa kwa litakalotokea, SunguSungu mmoja akauliza"mchana"kuna mwamba alikuwa nyuma yangu akajibu "usiku" mara nikasikia "kaa chini,kaa chini" Tulianza kutoka nduki,Wale sungusungu wakafanikiwa kuwakamata washkaji wetu wawili, Jamaa tulivoamka asubuhi masela wakaja wameibiwa simu,walleti,na viatu na wale Sungusungu, Kuna watu wanatumia kivuli cha Sungusungu kuwaibia raia nyakati za usiku.

Na huu ndio ukweli sungusungu ni mkusanyiko wa vijana waliokata tamaa na maisha.
 
Back
Top Bottom