Chanika kidugalo tunasherehekea Muungano tukiwa bado gizani kwa sababu za kisiasa

PSEUDOPODIA

JF-Expert Member
Aug 9, 2020
376
735
Jamani sitachoka kupiga kelele kuende kuileta hii kero yetu kwenu hasa viongozi wetu.

Sisi wananchi wa Chanika kitongoji cha Kidugalo hususani baadhi ya mashina ya kitongoji kero yetu kubwa ni umeme.

Tulipoona mradi wa Rea umefika tulifurahi sana nae kusema hatimae Mungu amesikia kilio chetu, lakini cha ajabu ni kuwa ulipo Anza ugawaji umeme tulimejikuta kwenye hali ya sintofahamu baada ya mkandarasi kupokea maagizo kutoka kwa mwenyekiti wa mtaa kwamba kuna baadhi yae mashina hawaruhusiwi kupata umeme.

Mwenyekiti alitoa maagizo hayo kama adhabu kwa wananchi hao kwakuwa kipind cha uchaguzi wa wenyeviti wa mitaa hatukumpigia kura kwenye uchaguzi wa ndani wa chama.

Hivyo basi mkandarasi akafuata maelekezo ya mwenyekiti na kweli kuna mashina mengi yanerukwa licha ya kuwa nguzo za umeme mkubwa zimepita kwao kwenda kwenye mashina mengine yanayostahili kupewa umeme. Tumejaribu kufuatilia kwenye ofisi za Tanesco zilizofunguliwa huku Chanika lakin hatujapata msaada, na mkandarasi anasema yeye mradi kashamaliza hukue kwetu nae kashakabizi.

Hivyo basi Mimi nawaomba viongozi wetu mnao husika na haya maswala mjaribu kutusaidia kwani na sisi ndoto yetu ni siku moja tuwashe umeme kwenye nyumba zetu kama wengine.

Ahsanteni.
 
Rohoo mbaya ya mwendazake.
Hapana, ni roho mbaya ya mwenyekiti wa mtaa wetu, yeye ukienda kwake kuna mita tano za umeme zote zimeenda kwenye nyumba zake...lakini kwa wenzake kapigat marufuku wasipewe umeme.
Anapokea maelekezo ndugu sisi tunaojua rohoo mbaya ya mwendazake amini tunachokuambia.
 
Rohoo mbaya ya mwendazake.

Anapokea maelekezo ndugu sisi tunaojua rohoo mbaya ya mwendazake amini tunachokuambia.
Lakin sisi wote chama kimoja, kama unavyofahamu mwaka ule uchaguzi ulikuwa ni ndani ya chama tu, ukishapita kwenye chama basi umeshindae uchaguzi kulingana na maelekezo ya mkuu. Hivyo kinyongo cha mwenyekiti wa mtaa wetu ni kuwa hatukumpa kura kwenye uchaguzi wa ndani wa chama.
 
Rohoo mbaya ya mwendazake.

Anapokea maelekezo ndugu sisi tunaojua rohoo mbaya ya mwendazake amini tunachokuambia.

Si mumpige petrol na kiberiti tu mkae kwa amani? Mtu mmoja anawaletea kero mnamuachaje kwa mfano?
 
Wale ambao enzi za Magufuri hamkupata maendeleo hamtakaa mkayapata tena.maana mzee alikuwa mpambanaji wa kweli.
 
Si mumpige petrol na kiberiti tu mkae kwa amani? Mtu mmoja anawaletea kero mnamuachaje kwa mfano?
Sisi Watanzania hatujaumbiwa hivyo. Ila tungekuwa tupo Somalia mbona asingekwepo huyu.
 
Sisi Watanzania hatujaumbiwa hivyo. Ila tungekuwa tupo Somalia mbona asingekwepo huyu.
Somalia ilikuwa na amani kuliko Tanzania ila baada ya watu kama wewe kuona unakusanya vya nchi unaweka kwako watu wakaanza kupiga mapanga .
 
Rohoo mbaya ya mwendazake.

Anapokea maelekezo ndugu sisi tunaojua rohoo mbaya ya mwendazake amini tunachokuambia.
Kama sio yeye hata hizo nguzo mnazosema zimepita mtaani kwenu msingeziona labda kama hamuna kumbukumbu kipindi JPM anaingia madarakani Tanesco walikuwa hawana nguzo za umeme na hizo nguzo zikiisha ndio msahau kuhusu umeme mtakula jeuri yenu
 
Jamani sitachoka kupiga kelele kuende kuileta hii kero yetu kwenu hasa viongozi wetu.

Sisi wananchi wa Chanika kitongoji cha kidugalo hususani baadhi ya mashina ya kitongoji kero yetu kubwa ni umeme...
Ndugu mpendwa mteja wetu

Tulitekeleza mradi eneo hilo hata hivyo awamu hiyo hawakuweza kupata wateja wote na sasa shirika linaandaa budget kwajili ya awamu nyingine ya utekelezaji wa mradi wa umeme vijiji.Ikumbukwe kuwa miradi hii inaenda kwa awamu mbalimbali.

Mradi unajengwa kulingana na scope na mchoro na sio kwa maelekezo ya uliowatuhumu kwenye maelezo yako.Jm
 
Ndugu mpendwa mteja wetu

Tulitekeleza mradi eneo hilo hata hivyo awamu hiyo hawakuweza kupata wateja wote na sasa shirika linaandaa budget kwajili ya awamu nyingine ya utekelezaji wa mradi wa umeme vijiji.Ikumbukwe kuwa miradi hii inaenda kwa awamu mbalimbali.

Mradi unajengwa kulingana na scope na mchoro na sio kwa maelekezo ya uliowatuhumu kwenye maelezo yako.Jm
Si kweli, kama ni kufuata mchoro basi sisi ndio tungekuwa wa kwanza kupata umeme, maana mchoro ulianzia kwetu na alama za vigingi wakaweka paka leo vipo.

Matokeo yake tukarukwa makusudi na kupelekwa hatae kule ambapo hakukuwa na alama wala mchoro.

Tukisema ni sababu za kisiasa ujue hivyo maana hata mwenyekiti mara kadhaa amenukuliwa akituambia pale tunapokwenda kuulizia suala hilo amekuwa akituambia tupambane na hali zetu.
 
Hapana, ni roho mbaya ya mwenyekiti wa mtaa wetu, yeye ukienda kwake kuna mita tano za umeme zote zimeenda kwenye nyumba zake...lakini kwa wenzake kapigat marufuku wasipewe umeme.
Mtu mmoja mkubwa alipata kusema." Msipochagua Chama changu sitoleta maendeleo"

Huyo mwenyekiti wenu anamuenzi, huyo mtu.
 
Mtu mmoja mkubwa alipata kusema." Msipochagua Chama changu sitoleta maendeleo"

Huyo mwenyekiti wenu anamuenzi, huyo mtu.
Daah, Mwenyekiti wetu Tatizo sana kwa afya ya maendeleo ya mtaa wetu. Yeye kazi yake ni kupiga pesa tu..Tunashida ya barabara lakin utadhani haoni, maji tunashkuru huku tumejichimbia visima wenyewe...Kifupi hana msaada wowote.
 
Si kweli, kama ni kufuata mchoro basi sisi ndio tungekuwa wa kwanza kupata umeme, maana mchoro ulianzia kwetu na alama za vigingi wakaweka paka leo vipo.

Matokeo yake tukarukwa makusudi na kupelekwa hatae kule ambapo hakukuwa na alama wala mchoro.

Tukisema ni sababu za kisiasa ujue hivyo maana hata mwenyekiti mara kadhaa amenukuliwa akituambia pale tunapokwenda kuulizia suala hilo amekuwa akituambia tupambane na hali zetu.
Tafadhi fika ofisini tukusikilize, Hii ni taasisi haiendeshwi bila mipango ya wapi umeme uende kwa kipindi gani na sio ambavyo unadai wewe.jm
 
Back
Top Bottom