Changia Mawazo muhimu Kwa Tanzania yetu

diamond d

JF-Expert Member
Dec 20, 2018
812
2,048
Ndugu watanzania, napenda kuanzisha Uzi huu muhimu Kwa maendeleo ya Taifa letu.

Ni kwamba, baada ya miaka mingi kupita, ni miaka hii jiji letu la Dar es Salaam limekuwa likitajwa sasa katika Top 10 tofautitofauti. Mfano:

Imo kwenye Top 10 ya miji mizuri Africa,
Top 10 ya miji inayokua Kwa kasi Africa,
Top 10 ya miji mikubwa Africa na ni mji mkubwa kuliko yote Africa Mashariki na Kati,
Top 12 ya miji tajiri Africa, nk.

Sasa Kama tumeweza kuingia kwenye List hizi, ni wazi kwamba kuna umuhimu wa kumaintain heshima na Sifa hizi.

Watanzania tumekuwa tukiwapuuza Jirani zetu kwamba wanajisifu Sana, nami Leo naungana nao kabisa kwamba vitu hivi tunavyoona si vya msingi ndivyo vinavyovuta watalii, na vinajenga taswira akilini mwa watu kwamba ndivyo ilivyo.

Sasa kwanini kuna umuhimu wa kumaintain Sifa hizi?
Ni kwamba itatufanya tufanye mambo makubwa zaidi ili tusipoteze hadhi yetu ya jiji letu hasa Dar es salaam.

Pia itatufanya tuwe na ukisasa zaidi hasa katika masuala mazima ya majengo na miundo mbinu.
Nchi Jirani wamekuwa wakiji tangaza na hata kujilinganisha na miji mingine mikubwa licha ya kuwa wao ni wakawaida tu.

Sasa Mawazo yangu!

Ni wakati sasa wa kuanza kuwa na majengo Unique, Matefu na makubwa ya kisasa, Barabara zenye ubunifu na ufurahishi inapo bidi.

Tutafute kuwa na majengo marefu Sana ili kuweza kufanya tutamkwe pia midomoni mwa nchi nyingine, na si kwamba sisi tutakuwa wa kwanza kufanya hivi Bali na wenzetu wanawaza hivi pia.

Ipo faida ya kujulikana kupitia sababu hizi tunazodhani ni za kijinga.

NAULIZA SWALI

Je, tumewahi jiuliza ni faida gani tulizo pata kupitia vitu vya kisasa kama vile,
Usafiri wa mwendo kasi,
Uwanja mkubwa wa mpira Afrika mashariki na Kati,
Daraja la kisasa la Kigamboni,
Mfugale Flyover,
Majengo marefu ya sasa Posta nk.

Ikumbukwe siku hizi utalii si tu kuangalia vitu vya kale (Kizamani), wanyama nk, Bali ni pamoja na vitu vizurivizuri na vya kisasa. MF, Dubai yenye majengo marefu zaidi duniani, South Africa nchi yenye miji ya kisasa Africa, Marekani nchi yenye miji mizuri na mikubwa.

Hitimisho:

Tujenge jengo hata moja REFU Sana ikiwezekana kuliko yote yajayo Africa mashariki na Africa Kwa ujumla ili pia tujipatie kujulikana zaidi Africa. Lakini pia ikumbukwe siku hizi lugha ya macho ndio inayo bamba Sana. Yaani Lugha ya Picha.

Mfano wenzetu Kenya, South Africa nk wameplani Kama inavyoonekana pichani;

TUKUMBUKE WENZETU WANAO FANYA HIVI SI WAJINGA, They win Investments kiutani utani. Tusiishie tu vi floor 35, 30, 12 nk. Au vijengo pacha no.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, AMEN.

Thanks.
DURBAN-ICONIC-TOWER_02-Large-520x400.jpeg
1726874_Centurion01.jpeg
CiB4ikKWsAA8L17.jpeg
nariobi-nssf-convention-centre-and-hotel.jpeg
 
Hahaha hiyo list kakuingiza nani?! Sio kila mnyama mwenye pembe ni ng'ombe.
 
Chadema sasa hivi wanakuja kuvuruga uzi na hoja zao za madawa hospitalini na madawati mashuleni. Watakwambia wakulima na wafanyakazi watanufaika vipi?
 
Chadema sasa hivi wanakuja kuvuruga uzi na hoja zao za madawa hospitalini na madawati mashuleni. Watakwambia wakulima na wafanyakazi watanufaika vipi?
Tena Watulie maana wafahamu hata duka lazima litangazwe na sio tu kujaza mzigo huku hujulikani, changamoto huwa haziishi.
 
Tujitahidi miji yetu tupige lami zaidi kwa kutumia wakandarasi wa ndani kwa technolojia nafuu. Tarura wanajitahidi sana katika hilo na watatufikisha pazuri.
 
Kuna uhaja wa kukuza sanaa ..hasa movies na music ..michezo hasa mpira wa kikapu.volleyball .netball...mchezo wa kuogelea ..
Hii itafanikishwa kwa yafuatayo
1.Serikali Kupitia Wizara ya michezo na sanaa .wajenge multipurpose indoor stadiums hata 4 kwa kila kanda mfano Dar.Mwanza Arusha .Mbeya
2.Michezo hii ihusishwe mashuleni
3.Muziki na Sinema zipwe kipaumbele ma vyuoni kwa kufundishwa vizur

Hii itasaidia sana kuongeza ajira kwa vijana..kwa sababu sio kila mtu anaweza kuwa daktari au mwalimu au mhasibu

Cha pili itaongeza pato la taifa..kwa njia ya viingilio kwenye shoo..kodi ..na pia utalii
 
Kwenye uwanja wa taifa pembezoni mwa uwanja wa kuchezea kuwekwe yale mabango ya kisasa ya mfumo kama wa TV, Kisha matangazo ya mbuga zetu na vivutio vilivyopo viwe vinaoneshwa pale wakati wa mechi mbali mbali.
 
Saaaaaafi Sana we need to be Classic bhana
Kwenye uwanja wa taifa pembezoni mwa uwanja wa kuchezea kuwekwe yale mabango ya kisasa ya mfumo kama wa TV, Kisha matangazo ya mbuga zetu na vivutio vilivyopo viwe vinaoneshwa pale wakati wa mechi mbali mbali.
 
Kuna uhaja wa kukuza sanaa ..hasa movies na music ..michezo hasa mpira wa kikapu.volleyball .netball...mchezo wa kuogelea ..
Hii itafanikishwa kwa yafuatayo
1.Serikali Kupitia Wizara ya michezo na sanaa .wajenge multipurpose indoor stadiums hata 4 kwa kila kanda mfano Dar.Mwanza Arusha .Mbeya
2.Michezo hii ihusishwe mashuleni
3.Muziki na Sinema zipwe kipaumbele ma vyuoni kwa kufundishwa vizur

Hii itasaidia sana kuongeza ajira kwa vijana..kwa sababu sio kila mtu anaweza kuwa daktari au mwalimu au mhasibu

Cha pili itaongeza pato la taifa..kwa njia ya viingilio kwenye shoo..kodi ..na pia utalii
Exactly mkuu. Ukiwa na indoor hata moja ya kisasa unaweza kuandaa michuano ya kimataifa kabisa. Mfano ikiwa Arusha watu wataweza kwenda mbugani baada ya mashindano.
 
Hili ni Jengo litakalo jengwa Kampala, sasa sisi Dar ni lipi? Hebu wahusika walifikirie hili aisee, majengo pale post ya mwanzo ni SA na Kenya
tapatalk_1545231178062.jpeg
 
Back
Top Bottom