Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
Kama mlivyosikia kwenye vyombo vya habari kuwa
MAHAKAMA ya Wilaya ya Chato, mkoani Geita, imemhukumu kifungo cha miaka mitano jela, mwenyekiti wa kijiji cha Minkoto, Alphonce Kanungu (44), na wenzake wawili baada ya kupatikana na hatia ya kuhamasisha vurugu, kuchoma nyumba na kuwakatakata ngombe 30 na mbuzi 20 kinyume cha sheria.
Wengine waliohukumiwa kifungo kama hicho ni Marco Elias (36) na Cosmas Kanungu (30) wote wakazi wa kijiji cha Minkoto, kata ya Bwanga.
Habari kutoka Chato zinaeleza kuwa mbali na kifungo hicho, washtakiwa hao wametakiwa kulipa fidia ya sh milioni 38 kwa mlalamikaji, Paul Mhunda.
Akitoa hukumu hiyo mwishoni mwa wiki, Hakimu Khasan Koja alisema ametoa adhabu hiyo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka ukiongozwa na Mwendesha Mashtaka Mkaguzi wa Polisi, Mkwasi Rashid.
Washtakiwa hao walidai kuwa April 3, mwaka huu, majira ya saa 2 usiku waliongoza kundi la wananchi, kwenda kufanya uharibifu mkubwa wa nyumba, mifugo na mali ya Paul Mhunda na kusababisha hasara ya sh milioni 38.
Response
Kwa imani na ushahidi mkubwa kuwa hukumu hii imetolewa kwa kuihusanisha na siasa, wanaharakati na wapenda Chadema wa Chato wameamua kuchanga mchango wa hiari ili kuwezesha kukata rufaa. Hadi hivi sasa tayari mwanasheria amemwandikia hakimu kutoa nakala ya hukumu ndani ya siku kumi ili tuweze kusonga mbele.
Kwa mwenye kuweza kuchangia aliyeko Chato amuone bwana Mange ambaye ni Katibu wa Chadema Chato au mchango kwa M pesa kwa
FAUSTINE KITASANJA - 0753 277741 - Katibu wa Tawi Chato
COSMAS MAKUNE - 0753 945 888 - Mwanaharakati
Appreciation itatolewa kwa wote watakao husika na jumla ya kiasi kilichochangwa kitatajwa kwa wahusika wote.
Asanteni........by Ta Muganyizi - Activist Kagera
MAHAKAMA ya Wilaya ya Chato, mkoani Geita, imemhukumu kifungo cha miaka mitano jela, mwenyekiti wa kijiji cha Minkoto, Alphonce Kanungu (44), na wenzake wawili baada ya kupatikana na hatia ya kuhamasisha vurugu, kuchoma nyumba na kuwakatakata ngombe 30 na mbuzi 20 kinyume cha sheria.
Wengine waliohukumiwa kifungo kama hicho ni Marco Elias (36) na Cosmas Kanungu (30) wote wakazi wa kijiji cha Minkoto, kata ya Bwanga.
Habari kutoka Chato zinaeleza kuwa mbali na kifungo hicho, washtakiwa hao wametakiwa kulipa fidia ya sh milioni 38 kwa mlalamikaji, Paul Mhunda.
Akitoa hukumu hiyo mwishoni mwa wiki, Hakimu Khasan Koja alisema ametoa adhabu hiyo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka ukiongozwa na Mwendesha Mashtaka Mkaguzi wa Polisi, Mkwasi Rashid.
Washtakiwa hao walidai kuwa April 3, mwaka huu, majira ya saa 2 usiku waliongoza kundi la wananchi, kwenda kufanya uharibifu mkubwa wa nyumba, mifugo na mali ya Paul Mhunda na kusababisha hasara ya sh milioni 38.
Response
Kwa imani na ushahidi mkubwa kuwa hukumu hii imetolewa kwa kuihusanisha na siasa, wanaharakati na wapenda Chadema wa Chato wameamua kuchanga mchango wa hiari ili kuwezesha kukata rufaa. Hadi hivi sasa tayari mwanasheria amemwandikia hakimu kutoa nakala ya hukumu ndani ya siku kumi ili tuweze kusonga mbele.
Kwa mwenye kuweza kuchangia aliyeko Chato amuone bwana Mange ambaye ni Katibu wa Chadema Chato au mchango kwa M pesa kwa
FAUSTINE KITASANJA - 0753 277741 - Katibu wa Tawi Chato
COSMAS MAKUNE - 0753 945 888 - Mwanaharakati
Appreciation itatolewa kwa wote watakao husika na jumla ya kiasi kilichochangwa kitatajwa kwa wahusika wote.
Asanteni........by Ta Muganyizi - Activist Kagera