Dejane
JF-Expert Member
- Jan 1, 2014
- 49,654
- 68,604
Nilivyokua mdogo kuna vitu nilikua sivijui na naona kawaida wala sijali najali kucheza na kula na vingine vya kitoto
Sasa nimekua nimekutana na changamoto nyingi mpaka sasa hapa nilipo nashukuru nimekua na moyo mgumu,moyo wangu unavumilia mengi kusemwa vibaya,kukosolewa hata kama umefanya vyema,ukijitetea unaonekana umejawa na kiburi.
Walivyosema kua uyaone kumbe sio kuyaona maghorofa au magari ,
Kwa niliyopitia moyo wangu umekuwa jiwe la fatuma hautikisiki abadan hata nisikie nini kutoka kwa wanadamu najua nao sio watimilifu kama mim,namshukuru aunt yangu na mama angu hua hawanikatishi tamaa kabisa kama wengine nawapenda hawa wanawake sijui ntawalipa nini!!
naamini nimekua naweza haswa kua mke wa mtu "japo naiogopa ndoa "nishazoea kua huru aisee"
Nimejifunza kutomdharau mtu yeyote awe mdogo au mkubwa ,yeyote yule namuheshimu (wanasema dharau maiti hawez kuamka,usimdharau anaepumua,dunia duara inazunguka)
Najitahidi kujifunza kuwa kimya hata nisikie neno la kuniumiza vibaya na kusamehe halaf nakaa kimya naacha yapite,naamini kila kitu kina muda wake ,wanaokusema vibaya ndio hao hao unaokula nao na kucheka nao lakin moyo haujali ,na siku zote kikulacho kinguoni mwako
Namshukuru Mola kwa kila jambo naamin changamoto ni nyingii lakin usikate tamaa,nimejifunza kutokata tamaa maishani mwangu ,nimejifunza pia kufanya kitu kuuridhisha moyo wangu na sio kuridhisha mwingine
Nimejifunza kujipa raha sisubiri kupewa raha na mwingine maana maisha mafupi haya watu wanakufa kila siku,
Napenda kusikiliza muziki wowote unipao raha na kucheza kama nikiweza pia naburudisha mwili wangu,yale magumu sitaki yaniumize kichwa maana naamini yatapita ,
Marafiki ni muhimu kubadilishana mawazo,kuna marafiki pia nimekutana nao nawapenda ,kuna mwingine aliniletea zawadi nzuri amekua rafiki yangu sana japo yupo mbali lakin urafiki wetu unaendelea ,ni wengi mno marafiki wazuri ,naamin undugu si kufanana bali ni kufaana
Wenu Dinazarde
Sasa nimekua nimekutana na changamoto nyingi mpaka sasa hapa nilipo nashukuru nimekua na moyo mgumu,moyo wangu unavumilia mengi kusemwa vibaya,kukosolewa hata kama umefanya vyema,ukijitetea unaonekana umejawa na kiburi.
Walivyosema kua uyaone kumbe sio kuyaona maghorofa au magari ,
Kwa niliyopitia moyo wangu umekuwa jiwe la fatuma hautikisiki abadan hata nisikie nini kutoka kwa wanadamu najua nao sio watimilifu kama mim,namshukuru aunt yangu na mama angu hua hawanikatishi tamaa kabisa kama wengine nawapenda hawa wanawake sijui ntawalipa nini!!
naamini nimekua naweza haswa kua mke wa mtu "japo naiogopa ndoa "nishazoea kua huru aisee"
Nimejifunza kutomdharau mtu yeyote awe mdogo au mkubwa ,yeyote yule namuheshimu (wanasema dharau maiti hawez kuamka,usimdharau anaepumua,dunia duara inazunguka)
Najitahidi kujifunza kuwa kimya hata nisikie neno la kuniumiza vibaya na kusamehe halaf nakaa kimya naacha yapite,naamini kila kitu kina muda wake ,wanaokusema vibaya ndio hao hao unaokula nao na kucheka nao lakin moyo haujali ,na siku zote kikulacho kinguoni mwako
Namshukuru Mola kwa kila jambo naamin changamoto ni nyingii lakin usikate tamaa,nimejifunza kutokata tamaa maishani mwangu ,nimejifunza pia kufanya kitu kuuridhisha moyo wangu na sio kuridhisha mwingine
Nimejifunza kujipa raha sisubiri kupewa raha na mwingine maana maisha mafupi haya watu wanakufa kila siku,
Napenda kusikiliza muziki wowote unipao raha na kucheza kama nikiweza pia naburudisha mwili wangu,yale magumu sitaki yaniumize kichwa maana naamini yatapita ,
Marafiki ni muhimu kubadilishana mawazo,kuna marafiki pia nimekutana nao nawapenda ,kuna mwingine aliniletea zawadi nzuri amekua rafiki yangu sana japo yupo mbali lakin urafiki wetu unaendelea ,ni wengi mno marafiki wazuri ,naamin undugu si kufanana bali ni kufaana
Wenu Dinazarde