Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Kwanza nampa pole kijana Sajuki pamoja na familia yake kwa ugonjwa unaomsumbu.Nilisikia uchungu sana jana nilipomsikia mke wa Sajuki,Wastara akiomba msaada redioni ili mumewe akatibiwe India,kilichonifanya nipate uchungu ni kiasi cha fedha alichokua anahitaji,milioni 25!Hivi ni kweli kwa kiwango alichofikia Sajuki katika bongo muvi anakosa fedha hizi?Kama kweli hana namshauri akipona atafute shughuli nyingine ya kufanya.Ni jambo la ajabu sana kwa alipofikia Sajuki halafu akose kiasi hicho cha fedha.Halafu wasanii wenzie wako wapí?Hivi kweli wameshindwa kuchana kiasi hicho cha fedha?Msiniambie hawana fedha wasanii wote hao,hii mikogo yao tunayoiona ya kujibandua ngozi,kuendesha magari,ulevi n.k wanatoa wapi hela?Plz msiniambie wanaazima,bongo muvi itakua haina maana kabisa na bora isiwepo.Kama mnashindwa kumsaidia mwenzeu muda huu mnataka afe ili mje na mikogo yenu ya kijinga msibani?Jamani hata wasanii wenzie wa bongo fleva?Jamani mpaka mkewe huyu kijana aende redioni?I don't believe this,it's a shame!Wizara ya utamaduni na michezo,wabunge mko wapi?Au mnataka msimame bungeni au muende msibani na msururu wenu wa magari kwenda kusaini kitabu cha maombolezo kwa mikogo huku mkisema "kijana alikua anajituma,mchango wake tunautambua" huku sauti yake ikiwa ringtone ya simu zenu,eti mnamuenzi!!Shame in both of you!Siamini kama hatujitambui kiasi hiki,uko wapi utu wetu?