KndNo1
JF-Expert Member
- Oct 26, 2021
- 627
- 2,023
Siku hizi magari yamekuwa bidhaa iliyozagaa kama Madera pale Kariakoo.
Kuna gari yard.. Kuna za minada.. Kuna za mikononi..
Gari za mikononi ni pendwa kutokana na bei yake kupoa kidogo.. Ingawa udalali ni mwingi.. Maneno kama AC unaganda.. Gari ya kufugwa.. Gari ya Mhindi..Namba D hiyo.. Safari popote.. Usitume sms unachelewa.. Jiandae kukutana nayo..!
Changamoto ya hizi gari..
1. Ujanja ujanja mwingi.. Dalali anauza gari ambayo hata yeye haifahamu, hapo lazima aweke chumvi zake.. Atakwambia hii gari service haivuki km 3000 na Castro oil ndio inatumika.. Ukimuuliza mwaka wa gari.. Engine code.. Kilometers.. Lazima akate simu kwanza akavute pumzi..!
2. Gharama ya fundi kwa ukagauzi.. Inabidi nje ya bei ya manunuzi uandae fundi wa kwenda kukagua.. Masega kama yapo au walishayatoa..! Gari ilishapata ajali.. Gari ilisharudiwa rangi.. Uaminifu ni mdogo..!
3. Uwe na smartphone na bando.. Hii ili kukagua madeni ya gari.. Gari za mkononi unakuta ina madeni ya kutosha.. Kuna deni la polisi.. Kuna deni la parking.. Na muuzaji hasemi anajikausha tuu.
4. Gari inaweza kuwa ilitumika kuchukulia mkopo mahali.. Hii hatari zaidi.. Muhimu kukagua kabla hujafanya malipo..! Uone kadi OG ya gari.
Kununua gari ya mkononi hakukupi option ya kuchagua gari zaidi unachofanya ni kukagua.
Tofauti na Be Forward ambapo unaweza ukafumba macho ukapoint gari yoyote. Changamoto ya Be Forward ni jinsi unavyozidi kuscroll down ndio bei inaongezeka..!
Kuna gari yard.. Kuna za minada.. Kuna za mikononi..
Gari za mikononi ni pendwa kutokana na bei yake kupoa kidogo.. Ingawa udalali ni mwingi.. Maneno kama AC unaganda.. Gari ya kufugwa.. Gari ya Mhindi..Namba D hiyo.. Safari popote.. Usitume sms unachelewa.. Jiandae kukutana nayo..!
Changamoto ya hizi gari..
1. Ujanja ujanja mwingi.. Dalali anauza gari ambayo hata yeye haifahamu, hapo lazima aweke chumvi zake.. Atakwambia hii gari service haivuki km 3000 na Castro oil ndio inatumika.. Ukimuuliza mwaka wa gari.. Engine code.. Kilometers.. Lazima akate simu kwanza akavute pumzi..!
2. Gharama ya fundi kwa ukagauzi.. Inabidi nje ya bei ya manunuzi uandae fundi wa kwenda kukagua.. Masega kama yapo au walishayatoa..! Gari ilishapata ajali.. Gari ilisharudiwa rangi.. Uaminifu ni mdogo..!
3. Uwe na smartphone na bando.. Hii ili kukagua madeni ya gari.. Gari za mkononi unakuta ina madeni ya kutosha.. Kuna deni la polisi.. Kuna deni la parking.. Na muuzaji hasemi anajikausha tuu.
4. Gari inaweza kuwa ilitumika kuchukulia mkopo mahali.. Hii hatari zaidi.. Muhimu kukagua kabla hujafanya malipo..! Uone kadi OG ya gari.
Kununua gari ya mkononi hakukupi option ya kuchagua gari zaidi unachofanya ni kukagua.
Tofauti na Be Forward ambapo unaweza ukafumba macho ukapoint gari yoyote. Changamoto ya Be Forward ni jinsi unavyozidi kuscroll down ndio bei inaongezeka..!