Changamoto ya kununua magari ya mkononi

KndNo1

JF-Expert Member
Oct 26, 2021
627
2,023
Siku hizi magari yamekuwa bidhaa iliyozagaa kama Madera pale Kariakoo.

Kuna gari yard.. Kuna za minada.. Kuna za mikononi..

Gari za mikononi ni pendwa kutokana na bei yake kupoa kidogo.. Ingawa udalali ni mwingi.. Maneno kama AC unaganda.. Gari ya kufugwa.. Gari ya Mhindi..Namba D hiyo.. Safari popote.. Usitume sms unachelewa.. Jiandae kukutana nayo..!

Changamoto ya hizi gari..
1. Ujanja ujanja mwingi.. Dalali anauza gari ambayo hata yeye haifahamu, hapo lazima aweke chumvi zake.. Atakwambia hii gari service haivuki km 3000 na Castro oil ndio inatumika.. Ukimuuliza mwaka wa gari.. Engine code.. Kilometers.. Lazima akate simu kwanza akavute pumzi..!

2. Gharama ya fundi kwa ukagauzi.. Inabidi nje ya bei ya manunuzi uandae fundi wa kwenda kukagua.. Masega kama yapo au walishayatoa..! Gari ilishapata ajali.. Gari ilisharudiwa rangi.. Uaminifu ni mdogo..!

3. Uwe na smartphone na bando.. Hii ili kukagua madeni ya gari.. Gari za mkononi unakuta ina madeni ya kutosha.. Kuna deni la polisi.. Kuna deni la parking.. Na muuzaji hasemi anajikausha tuu.

4. Gari inaweza kuwa ilitumika kuchukulia mkopo mahali.. Hii hatari zaidi.. Muhimu kukagua kabla hujafanya malipo..! Uone kadi OG ya gari.

Kununua gari ya mkononi hakukupi option ya kuchagua gari zaidi unachofanya ni kukagua.

Tofauti na Be Forward ambapo unaweza ukafumba macho ukapoint gari yoyote. Changamoto ya Be Forward ni jinsi unavyozidi kuscroll down ndio bei inaongezeka..!
 
Hata Yale ya yard mengi Yana ujanja ujanja tu, pote ni kubahatisha, gari za mikononi kwa watu unaweza ukapata iliosimama mpaka ukashangaaa! Nilinunua matako ya nyani kwa mwarabu mmoja hivi kwa 14.5m nikakaa nayo wiki 2 nikaiuza 24m kwa mtu wangu wa karibu sana na iko imara balaa, mpaka sasa ina km 68,000 haina shida yeyote.
 
Kuna Mwanangu alienda na Fundi wake kukagua Gari vile anafika kisiri siri Fundi akakamatishwa 150k na Madalali Mkononi, basi Bwana Fundi akaanza kuisifia ile Gari kama yake kumbe Kimeo..... baada ya kununua Jamaa ikaanza kumsumbua hadi alijuta kuinunua
 
Niliona gari FB nikaipenda nikaamua tu kujilipua, nikapiga simu kesho nikaenda nikakutana na muuzaji kwa kumwangalia tu ni mjanja mjanja na mimi sikuwa najua lolote kuhusu magari hata kuendesha sijui. Akaniuliza fundi wako yuko wapi?

Nikamwambia mshkaji wazi tu kuwa mini sijui lolote kuhusu magar na hata kuendesha sijui kwahiyo kila kitu nakutegemea wewe hapa ukiingiza chaka ni wewe ila mimi gar nimeipenda.

Aisee ile gari mpaka inakata mwaka haikuwahi kunipa headache na bado ipo inapiga mzigo. Yani ni service za kawaida tu ..sana yan. Nilibahatisha naweza kusema.
 
Niliona gari fb nikaipenda nikaamua tu kujilipua.nikapiga cm kesho nikaenda nikakutana na muuzaji kwa kumwangalia tu ni mjanja mjanja na mm sikua najua lolote kuhusu magar hata kuendesha sijui.akaniuliza fundi wako yuko wap?

Nikamwambia mshkaji wazi tu kuwa mini sijui lolote kuhusu magar na hata kuendesha sijui kwahiy kila kitu nakutegemea wewe hapa ukiingiza chaka ni wewe ila mi gar nimeipenda.

Aisee ile gar mpaka inakata mwaka haikuwah kunipa headache na bado ipo inapiga mzigo.Yan ni service za kawaida tu ..sana yan.Nilibatisha naweza kusema
Duuh mshukur mungu TU Wala sio huyo jamaa
 
Niliona gari fb nikaipenda nikaamua tu kujilipua.nikapiga cm kesho nikaenda nikakutana na muuzaji kwa kumwangalia tu ni mjanja mjanja na mm sikua najua lolote kuhusu magar hata kuendesha sijui.akaniuliza fundi wako yuko wap?

Nikamwambia mshkaji wazi tu kuwa mini sijui lolote kuhusu magar na hata kuendesha sijui kwahiy kila kitu nakutegemea wewe hapa ukiingiza chaka ni wewe ila mi gar nimeipenda.

Aisee ile gar mpaka inakata mwaka haikuwah kunipa headache na bado ipo inapiga mzigo.Yan ni service za kawaida tu ..sana yan.Nilibatisha naweza kusema
Hongera yako..
FB itakuwa bado hawajachangamka kama kina Sossy Magari..!
 
Siku hizi magari yamekuwa bidhaa iliyozagaa kama Madera pale Kariakoo.

Kuna gari yard.. Kuna za minada.. Kuna za mikononi..

Gari za mikononi ni pendwa kutokana na bei yake kupoa kidogo.. Ingawa udalali ni mwingi.. Maneno kama AC unaganda.. Gari ya kufugwa.. Gari ya Mhindi..Namba D hiyo.. Safari popote.. Usitume sms unachelewa.. Jiandae kukutana nayo..!

Changamoto ya hizi gari..
1. Ujanja ujanja mwingi.. Dalali anauza gari ambayo hata yeye haifahamu, hapo lazima aweke chumvi zake.. Atakwambia hii gari service haivuki km 3000 na Castro oil ndio inatumika.. Ukimuuliza mwaka wa gari.. Engine code.. Kilometers.. Lazima akate simu kwanza akavute pumzi..!

2. Gharama ya fundi kwa ukagauzi.. Inabidi nje ya bei ya manunuzi uandae fundi wa kwenda kukagua.. Masega kama yapo au walishayatoa..! Gari ilishapata ajali.. Gari ilisharudiwa rangi.. Uaminifu ni mdogo..!

3. Uwe na smartphone na bando.. Hii ili kukagua madeni ya gari.. Gari za mkononi unakuta ina madeni ya kutosha.. Kuna deni la polisi.. Kuna deni la parking.. Na muuzaji hasemi anajikausha tuu.

4. Gari inaweza kuwa ilitumika kuchukulia mkopo mahali.. Hii hatari zaidi.. Muhimu kukagua kabla hujafanya malipo..! Uone kadi OG ya gari.

Kununua gari ya mkononi hakukupi option ya kuchagua gari zaidi unachofanya ni kukagua.

Tofauti na Be Forward ambapo unaweza ukafumba macho ukapoint gari yoyote. Changamoto ya Be Forward ni jinsi unavyozidi kuscroll down ndio bei inaongezeka..!
Usahau, ''gari inaendeshwa na mwanamke tu'',sokoni - nyumbani:cool:
 
Gari za mkononi hizo.. Dalali anataka ajenge kupitia gari ya Bosi..!
_20220510_222918.JPG

_20220510_222831.JPG
 
Back
Top Bottom