Changamoto ya biashara ya mgahawa kipindi cha ramadhani

milionea wa kesho

JF-Expert Member
Dec 28, 2015
328
631
wakuu nina kimgahawa cha kizushi napikaga chakula. leo mwezi wa ramadhani umeanza na waumini wengi wa kiislam wanafunga mchana hawali. nahisi kabisa kabiashara kangu katadhoofika. au mnasemaje wakuu?
 
biashara yako ipo mtaa gani? Nenda sokoni nunua futari ndizi mbivu mshale, magimbi, tambi, mihogo, kama unajua pika kalimati, ndizi mbichi utumbo, nunua tende kidogo, pika na uji mwepesi usiwe mzito sana (vyakula vikolee nazi). Weka bango KARIBUNI KWA FUTARI, hakikisha uji unakuwa free (wape offer wanaofunga kuonyesha unawajali sana) toa viti kidogo na tandika mikeka safi unaetaka anakaa, Utawapata hata wasio funga, hakikisha mboga smaki ama nyama unaweka ya kutosha, panga bei zako vizuri kisha mwezi ukiisha lete mrejesho hapa.
 
asante sana mkuu...tatizo mgahawa wangu upo maeneo ya sokoni ambapo basically watu wanakuepo mchana na asubuhi tu
biashara yako ipo mtaa gani? Nenda sokoni nunua futari ndizi mbivu mshale, magimbi, tambi, mihogo, kama unajua pika kalimati, ndizi mbichi utumbo, nunua tende kidogo, pika na uji mwepesi usiwe mzito sana (vyakula vikolee nazi). Weka bango KARIBUNI KWA FUTARI, hakikisha uji unakuwa free (wape offer wanaofunga kuonyesha unawajali sana) toa viti kidogo na tandika mikeka safi unaetaka anakaa, Utawapata hata wasio funga, hakikisha mboga smaki ama nyama unaweka ya kutosha, panga bei zako vizuri kisha mwezi ukiisha lete mrejesho hapa.
 
asante sana mkuu...tatizo mgahawa wangu upo maeneo ya sokoni ambapo basically watu wanakuepo mchana na asubuhi tu
Fuata ushauri wa jamaa.
Uzur wa futari inauzika hata barabarani kwa sababu muda wa kufuturu jua linakuwa limezama.
Kama unahisi hapo sokoni pamejificha sana kiasi Cha kutoonekana hamisha mabenchi yako na viti kaweke kandokando ya barabara wanakopita abiria/wasafiri au hata wanapopita wafanyakazi wa aina yoyote watakufuata.
Hapo kwenye mgahawa wako bandika tangazo tu kwamba umehamia mtaa fulani kwa sababu ya kuuza futari.
 
Fuata ushauri wa jamaa.
Uzur wa futari inauzika hata barabarani kwa sababu muda wa kufuturu jua linakuwa limezama.
Kama unahisi hapo sokoni pamejificha sana kiasi Cha kutoonekana hamisha mabenchi yako na viti kaweke kandokando ya barabara wanakopita abiria/wasafiri au hata wanapopita wafanyakazi wa aina yoyote watakufuata.
Hapo kwenye mgahawa wako bandika tangazo tu kwamba umehamia mtaa fulani kwa sababu ya kuuza futari.

Mkuu mbu wa dengue uzuri wa futari hizi huwa ni za msimu, ukichanganya na vitu kama maharage ya sukari, njugu mawe na bidhaa kama hizo na watu wakishagundua utauza tu.
 
Mkuu mbu wa dengue uzuri wa futari hizi huwa ni za msimu, ukichanganya na vitu kama maharage ya sukari, njugu mawe na bidhaa kama hizo na watu wakishagundua utauza tu.
Ni kweli hakuna dawa zaidi ya utamu wa chakula.
Ukienda kwenye migahawa ya watu wa kutoka Tanga wanajulia sana yaani lazima utarud tena.
 
Futari uza barabara za namba kule au Mtaa wa Chako Ni chako Kuna mazaa anawateja pale nyuma ya chako Ni chako
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom