Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,013
- 144,371
Kampuni ya ndege ya Fastjet jijini Mwanza leo Jumapili Oktoba 28, 2018 imeeleza kusitisha safari zake kuanzia asubuhi hadi mchana kutoka Mwanza kuelekea Dar es Salaam kutokana na ndege kupata hitilafu.
Abiria waliopaswa kusafiri saa 2:00 asubuhi sasa watasafiri saa 1:30 usiku wakati waliotakiwa kusafiri leo jioni, wataondoka Mwanza saa 5:00 usiku.
Uamuzi huo umetangazwa kwa mamia ya abiria waliojazana nje ya ofisi ndogo ya kampuni huyo katika uwanja wa ndege Mwanza.
“Kampuni itatoa Sh30,000 kwa kila abiria kwa ajili ya kunywa chai asubuhi na usafiri wa kurejea mjini wakati wa kusubiri muda wa safari," amesema mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo
Mwanza kwa sharti la kutotajwa.
Kutokana na wingi wa abiria, muda wa abiria kuingia uwanja wa ndege itakuwa kuanzia saa 11:00 jioni."
Mfanyakazi huyo amewahakikishia abiria hao uhakika wa kusafiri jioni na usiku kutokana na hitilafu katika ndege kurekebishwa.
Abiria waliopaswa kusafiri saa 2:00 asubuhi sasa watasafiri saa 1:30 usiku wakati waliotakiwa kusafiri leo jioni, wataondoka Mwanza saa 5:00 usiku.
Uamuzi huo umetangazwa kwa mamia ya abiria waliojazana nje ya ofisi ndogo ya kampuni huyo katika uwanja wa ndege Mwanza.
“Kampuni itatoa Sh30,000 kwa kila abiria kwa ajili ya kunywa chai asubuhi na usafiri wa kurejea mjini wakati wa kusubiri muda wa safari," amesema mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo
Mwanza kwa sharti la kutotajwa.
Kutokana na wingi wa abiria, muda wa abiria kuingia uwanja wa ndege itakuwa kuanzia saa 11:00 jioni."
Mfanyakazi huyo amewahakikishia abiria hao uhakika wa kusafiri jioni na usiku kutokana na hitilafu katika ndege kurekebishwa.