Steve Dii
JF-Expert Member
- Jun 25, 2007
- 6,402
- 1,254
Watanzania wenzangu, katika kipindi hiki kilichojaa shamra shamra za kufunga mwaka, naomba tusherehekee kwa mavazi yenye asili ya Kitanzania, yanayotokana na malighafi kutoka Tanzania na yaliyobuniwa na Watanzania.
Bidhaa 'feki' nchini mwetu kutoka pande mbalimbali za dunia zimezidi na zinazidi kuongezeka. Kuanzia bidhaa za umeme, madawa, nguo na hata vyakula zisizo kidhi hadhi ya kibinadamu zinazidi kutuingilia.
Hasara yake kiuchumi ni kubwa, na kikubwa zaidi ni ile hasara yake kiafya. Pamoja na kuwa kuna jambo la kutia matumaini limeanza kujitokeza hivi karibuni, maana kampeni kadhaa zimeanza kujitokeza na kushika hatamu katika kukabiliana na JANGA hili la bidhaa zisizofaa. Kwenye vyombo vya habari na pahala penginepo pengi, swala la bidhaa feki linazidi kuongelewa na tumeshuhudia bidhaa mbalimbali zikiteketezwa baada ya kugundulika kuwa hazitufai. Hivyo katika kuendeleza mapambano haya, bidii zaidi katika kuhamasisha na kuelimisha wananchi zinahitajika.
Ndiyo nakubali kuwa nchini mwetu hatutengenezi 'microchips', hatutengenezi 'energy serving bulbs', hatutengenezi 'mobile phone handsets' na vingine vingi. Lakini ninafurahi na kujisifia kwani tuna uwezo wa kulima zao la pamba na tunaweza kutengeneza nguo. Sasa kwanini basi tusitumie fursa kama hii kwenye sherehe za Idd, Noel na Mwaka Mpya kununua kilicho chetu 'ndani na nje'?!
Basi Wana JF na Watanzania wote, tuhamasike na kuchochea nguvu ya kuinua uchumi wetu. Tumelalamika na tumekosoa vya kutosha, sasa tutende angalau moja tu - TUNUNUE MADE IN TANZANIA. Hata hivyo naomba tu kuweka jambo moja bayana, ombi na changamoto hii siyo surutisho la mapambano yetu katika kukosoa, kukemea, kurekebisha, kufichua, kuelimishana n.k. katika mambo ya mustakabali wa Taifa letu. HII NI CHANGAMOTO KWA WATANZANIA KUFANYA KILE TUNACHOWEZA, TENA TUNAKIWEZA KIURAHISI NA KITU HIKI NI NGUO/MAVAZI!!
Miezi michache iliyopita tulishuhudia Spika wa Bunge letu Tukufu akijisifia na vazi lake la kikazi kwa vile lilibuniwa na kutengenezwa kule Uingereza. Sasa tukiacha siasa pembeni, hili swala kinamna na kwa maoni yangu ni jambo la kutia aibu. Hilo joho hata kama lingetengenezwa na "fundi Hamisi pale kwa jirani" mimi ningeliona ni jambo la kujisifia zaidi kuliko jinsi ilivyotokea.
Na cha kuleta matumaini zaidi ni kuwa, njia za mawasiliano zinazidi kuongezeka (nyezo za kutaka kujua vazi hili linaweza kupatikana wapi zinajizatiti). Pia wabunifu hapa nchini (tena wengine wenye hadhi ya kimataifa) wanazidi kuongezeka, na kikubwa kuhusiana na mavazi ni kuwa, ufanisi nao unaongezeka na kutia faraja katika mioyo ya wengi. Matukio mengi kudhihirisha hili yanatokea, na kwa waliopo hapa Dar-es-salaam basi hawana kabisaa la kujitetea wanapogundulika kuwa ni baadhi ya wale wachache wenye uwezo wa kununua bidhaa wapendazo toka nje ya nchi.
Katika kuinua pato la Taifa, kusaidia ndugu zetu walio katika biashara ya nguo/mavazi: WANA JF, WATANZANIA WOTE, SIFIENI WALE WALIOVAA "MADE IN TANZANIA", SIFIENI WALIOVAA VITENGE NA KANGA KUTOKA TANZANIA... TUDUMISHE NA KUENDELEZA VILIVYO VYETU KWA KUVINUNUA NA KUVISIFIA, KWA KUVITUKUZA NA KUVIENZI.
Tutafika tu....
Nawatakia Sikukuu Njema!
SteveD.
Bidhaa 'feki' nchini mwetu kutoka pande mbalimbali za dunia zimezidi na zinazidi kuongezeka. Kuanzia bidhaa za umeme, madawa, nguo na hata vyakula zisizo kidhi hadhi ya kibinadamu zinazidi kutuingilia.
Hasara yake kiuchumi ni kubwa, na kikubwa zaidi ni ile hasara yake kiafya. Pamoja na kuwa kuna jambo la kutia matumaini limeanza kujitokeza hivi karibuni, maana kampeni kadhaa zimeanza kujitokeza na kushika hatamu katika kukabiliana na JANGA hili la bidhaa zisizofaa. Kwenye vyombo vya habari na pahala penginepo pengi, swala la bidhaa feki linazidi kuongelewa na tumeshuhudia bidhaa mbalimbali zikiteketezwa baada ya kugundulika kuwa hazitufai. Hivyo katika kuendeleza mapambano haya, bidii zaidi katika kuhamasisha na kuelimisha wananchi zinahitajika.
Ndiyo nakubali kuwa nchini mwetu hatutengenezi 'microchips', hatutengenezi 'energy serving bulbs', hatutengenezi 'mobile phone handsets' na vingine vingi. Lakini ninafurahi na kujisifia kwani tuna uwezo wa kulima zao la pamba na tunaweza kutengeneza nguo. Sasa kwanini basi tusitumie fursa kama hii kwenye sherehe za Idd, Noel na Mwaka Mpya kununua kilicho chetu 'ndani na nje'?!
Basi Wana JF na Watanzania wote, tuhamasike na kuchochea nguvu ya kuinua uchumi wetu. Tumelalamika na tumekosoa vya kutosha, sasa tutende angalau moja tu - TUNUNUE MADE IN TANZANIA. Hata hivyo naomba tu kuweka jambo moja bayana, ombi na changamoto hii siyo surutisho la mapambano yetu katika kukosoa, kukemea, kurekebisha, kufichua, kuelimishana n.k. katika mambo ya mustakabali wa Taifa letu. HII NI CHANGAMOTO KWA WATANZANIA KUFANYA KILE TUNACHOWEZA, TENA TUNAKIWEZA KIURAHISI NA KITU HIKI NI NGUO/MAVAZI!!
Miezi michache iliyopita tulishuhudia Spika wa Bunge letu Tukufu akijisifia na vazi lake la kikazi kwa vile lilibuniwa na kutengenezwa kule Uingereza. Sasa tukiacha siasa pembeni, hili swala kinamna na kwa maoni yangu ni jambo la kutia aibu. Hilo joho hata kama lingetengenezwa na "fundi Hamisi pale kwa jirani" mimi ningeliona ni jambo la kujisifia zaidi kuliko jinsi ilivyotokea.
Na cha kuleta matumaini zaidi ni kuwa, njia za mawasiliano zinazidi kuongezeka (nyezo za kutaka kujua vazi hili linaweza kupatikana wapi zinajizatiti). Pia wabunifu hapa nchini (tena wengine wenye hadhi ya kimataifa) wanazidi kuongezeka, na kikubwa kuhusiana na mavazi ni kuwa, ufanisi nao unaongezeka na kutia faraja katika mioyo ya wengi. Matukio mengi kudhihirisha hili yanatokea, na kwa waliopo hapa Dar-es-salaam basi hawana kabisaa la kujitetea wanapogundulika kuwa ni baadhi ya wale wachache wenye uwezo wa kununua bidhaa wapendazo toka nje ya nchi.
Katika kuinua pato la Taifa, kusaidia ndugu zetu walio katika biashara ya nguo/mavazi: WANA JF, WATANZANIA WOTE, SIFIENI WALE WALIOVAA "MADE IN TANZANIA", SIFIENI WALIOVAA VITENGE NA KANGA KUTOKA TANZANIA... TUDUMISHE NA KUENDELEZA VILIVYO VYETU KWA KUVINUNUA NA KUVISIFIA, KWA KUVITUKUZA NA KUVIENZI.
Tutafika tu....
Nawatakia Sikukuu Njema!
SteveD.