Changamoto nilizokutana nazo kwenye kilimo na jinsi nilivyozikabili

Fursakibao

JF-Expert Member
Dec 12, 2017
6,676
11,109
Habari za mida wadau wenzangu wa kilimo.

Niende moja kwa moja ni share safari yangu kwenye hii fani ya kilimo ili wale wanaotegemea kujiunga wapate ka uzeofu kadogo japo wapate pa kuanzia.

Nimekuwa nikifanya shuguli za kilimo toka mwaka 2014 toka hapo nimekuwa nikipata na kukosa pia.
Nilianza kulima tumbakuku mwaka 2014 huko wilaya ya Serengeti; katika hichi kilimo cha tumbaku tulifanikiwa kupata milioni 20 ambazo tuligawana kwani tulilima kifamilia.
Mwaka 2015 nikalima Mahindi na Alizeti wilaya ya kiteto; ambapo nilifanikiwa kuvuna tani 15 za mahindi na tani 6 za alizeti.

Mwaka 2016 nililima heka 50 za mahindi, mbaazi pamoja na alizeti wilaya ya Kiteto. Huu mwaka sikupata hata shilingi kumi, hivyo nikaishia kupata hasara ya milioni 10.

Mwaka 2017 /18 nililima matikiti maji pamoja na pilipiili hoho. Hichi kilimo kilikuwa tofauti na vingine kwani nilijikita zaidi katika kilimo cha umwagiliaji licha ya kufanya kilimo cha umwagiliaji niliishia kupata hasara ya Milioni 8.

Kulingana na hasara nilizo zipata mwaka 2016 – 2018 nilighafirika sana na kuamua kupumzika kwa muda huku nikitafuta njia ya kukabiliana na changemoto zilizosababisha nipate hasara.

Mimi sio mwandishi mzuri na ni mvivu pale linapokuja suala la kuandika makala ila nitajitahidi kuandika ili wale wanaotarajia kuingia kwenye kilimo wajifunze kitu.

Hivyo basi nitajitahidi kuchambua hizi changamoto kwa kila msimu niliolima.

2015
Huu mwaka kama nilivyoeleza hapo juu sikupata hasara japokuwa nilichokipata kilikuwa chini ya matarajio kwa sababu ya changamoto zifuatazo:

1. Kukosa muda wa kusimamia shamba kwa 100%

Hii ni moja ya changamoto inayotukabili wakulima wengi ambao tunajihusisha na kilimo wakati huo huo tukiwa tumeajiliwa hivyo; kukosa muda wa kulisimamia shamba kwa 100% kulipelekea kazi kufanyika chini ya kiwango kinachotakiwa hivyo kupelekea mimi kupata mavuno kidogo.

Mambo vitu vilivyosababisha nipate mazao chini ya mategemeo vilikuwa:

i. Eneo lililolimwa lilikuwa chini ya lile liliotakiwa kulimwa. Nilipanga nilime heka 45 matokeo yake nilikuta heka 35 tu.

ii. Palizi kutofanyika kwa wakati. Kati ya hizo heka 35 nilikuta heka 10 hazijapaliliwa kabisa licha ya kwamba nilipokuwa napiga simu kuulizia naambiwa shamba liko vizuri. Siku nilipofika shambani nilitaka kulia kwani hali niliikuta kama muonavyo hapo chini.

1572430607606.png
1572430639276.png

iii. Kuibiwa mazao wakati wa mavuno. Hapa niliibiwa kiasi ambacho siwezi kujua kilikuwa ni kiasi gani kwani tulikuwa tunavuna alafu tunaacha mazao shambani mpaka siku inayofuata. Picha hapo chini

1572431560809.png


Itaendelea.
 
Changamoto ni sehemu ya kilimo. Tatizo naona ulijikita kulima mazao yote yanayohitaji uangalizi wa hali ya juu na pia soko lake halieleweki.

Usipokuwa makini na mbaazi huvuni kitu, hoho ukibugi kwenye mbegu au matunzo na dawa ni kilio. Tikiti nalo hivyo hivyo litakuliza shambani na zaidi sokoni. Mahindi inategemea msimu

Tafuta eneo moja utulie epuka mashamba ya kukodi yana mambo mengi

Wewe ni mpiganaji kweli popote unakwenda fanya utafiti wa kina kujua ni zao gani lina mahitaji na bei stable ndio ulime, epuka kulima mazao ya wengi/kufuata mkumbo angalia mahitaji ya soko kwanza
 
Changamoto ni sehemu ya kilimo. Tatizo naona ulijikita kulima mazao yote yanayohitaji uangalizi wa hali ya juu na pia soko lake halieleweki.

Usipokuwa makini na mbaazi huvuni kitu, hoho ukibugi kwenye mbegu au matunzo na dawa ni kilio. Tikiti nalo hivyo hivyo litakuliza shambani na zaidi sokoni. Mahindi inategemea msimu

Tafuta eneo moja utulie epuka mashamba ya kukodi yana mambo mengi

Wewe ni mpiganaji kweli popote unakwenda fanya utafiti wa kina kujua ni zao gani lina mahitaji na bei stable ndio ulime, epuka kulima mazao ya wengi/kufuata mkumbo angalia mahitaji ya soko kwanza
Suala la kulima mazao yanayo hoitaji uangalizi wa juu nitakubalian na wewe; kwenye suala la soko nitakataa maana tayali nilikuwa nimeshapata soko tatizo lilikuja kuwa wale watu niliowaajiri kwenye shamba la tikiti walikuwa hawana utaaalamu na mazao hayo na pia hawakuwa wanajali.

Nitakupa mfano kuna siku vibarua waliniambia kuwa wameacha kumwagilizia hoho kwani zimeharibika, hivyo wameona wasiharibu mavuta. baada ya siku kadhaa nikaenda shambani; kwa kweli machozi yalinitoka kwani jinsi nilivyokuta hoho sivyo walivyokuwa wanasema. hivi mtu mwenye kujali anaweza kusema kuwa hoho hizo hapo chini zimeharibika?



20181208_172333.jpg


20181208_172408.jpg
 

Attachments

  • 20181208_172347.jpg
    20181208_172347.jpg
    242.3 KB · Views: 14
Suala la kulima mazao yanayo hoitaji uangalizi wa juu nitakubalian na wewe; kwenye suala la soko nitakataa maana tayali nilikuwa nimeshapata soko tatizo lilikuja kuwa wale watu niliowaajiri kwenye shamba la tikiti walikuwa hawana utaaalamu na mazao hayo na pia hawakuwa wanajali.

Nitakupa mfano kuna siku vibarua waliniambia kuwa wameacha kumwagilizia hoho kwani zimeharibika, hivyo wameona wasiharibu mavuta. baada ya siku kadhaa nikaenda shambani; kwa kweli machozi yalinitoka kwani jinsi nilivyokuta hoho sivyo walivyokuwa wanasema. hivi mtu mwenye kujali anaweza kusema kuwa hoho hizo hapo chini zimeharibika?



View attachment 1249853

View attachment 1249855
Mkuu pole sana, hao wafanyakazi wako usingekwenda shamba wangeingiza hizo hoho sokoni, hawa ndio watz!

Jipange anza upya, Kama uliweza kuwekeza 50m tafuta mazao ya muda mrefu yenye soko la uhakika upande, jenga kijumba shambani simamia mwenyewe kwa ukaribu kuulinda uwekezaji wako. Kilimo ni matunzo na kinalipa sana ukituliza akili
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom