Changamoto isiyoongelewa: Maelfu ya wanafunzi wa Kitanzania kushindwa kwenda kusoma nje kutokana na corona

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Baadhi yetu kwa muda mrefu tumekuwa tunaongelea athari za kufanya mjadala wa athari za corona nchini kuwa ni mwiko.

Moja ya athari zake ni familia za kitanzania pamoja na taasisi mbalimbali kushindwa kujipanga (kutokana na kwamba hawana taarifa) kutokana na mabadiliko ya lazima yanayoendelea duniani kote.

Mjadala mpana ulihitajika badala ya kutegemea vichwa vichache na mambo kufanywa kwa usiri mkubwa. Naona kama tunaficha tu vitu ambavyo wakati ukifika vinaweza kuja kutuumbua.

Kila mwaka, watanzania wengi (mwenye takwimu anaweza kutusaidia) wanakwenda sehemu mbalimbali duniani kutafuta elimu.

Kutokana na janga la corona, binafsi ninaamini (na hili nimeliwaza muda mrefu kidogo), idadi hiyo wanaokwenda nje imelazimu kupungua saana, hasa kwa sababu ya woga na utashi wa wanafunzi wenyewe na wazazi wao.

Hii ina maana kuwa kutakuwa na shinikizo kubwa la mahitaji, hasa ya elimu ya juu kwa vyuo vyetu vya ndani kwa mwaka huu wa masomo 2020-2021 na inawezekana hata kwa mwakani.

Nimesikia vyuo kama UDSM, vimefanya usajili mkubwa sana awamu hii. Sina uhakika hali ikoje katika vyuo vingine.
 
Inawezekana hata matibabu nje imekuwa mtihani. Kama unaumwa ugonjwa ambao ni juu ya uwezo wa Hospital za Bongo ni nafasi ya akina Mwamposa,Manyau nyau au Sheikh Sharif.
 
Na leo yamezuka mapya Marekani inadai Tanzania tunaongoza takwimu ya corona ukijiuliza takwimu hizo wametoa wapi na.kam. nchi kam. Nchi tuja toa yaa.n
Just beef ya mmarekani. Na Tanzania sio bure
 
Na leo yamezuka mapya Marekani inadai Tanzania tunaongoza takwimu ya corona ukijiuliza takwimu hizo wametoa wapi na.kam. nchi kam. Nchi tuja toa yaa.n
Just beef ya mmarekani. Na Tanzania sio bure
Marekani haina bifu na nchi iitwayo tanzania. Ila wanatoa mbinyo kidogo ili kuwashikisha adabu wanaoanza kuota mapembe wanaodhani wanaweza kuikanyaga katiba na kujifanyia maamuzi watakavyo.

Tatizo maumivu huanzia kwa raia wa kawaida wakisha kongoroka yanahamia kwa vigogo. Baada ya hapo? Tunakwenda zimbabwe
 
Marekani haina bifu na nchi iitwayo tanzania. Ila wanatoa mbinyo kidogo ili kuwashikisha adabu wanaoanza kuota mapembe wanaodhani wanaweza kuikanyaga katiba na kujifanyia maamuzi watakavyo.

Tatizo maumivu huanzia kwa raia wa kawaida wakisha kongoroka yanahamia kwa vigogo. Baada ya hapo? Tunakwenda zimbabwe
Sas hiz data wanatoa wapi kam. Nchi tu haijatoa
 
Marekani haina bifu na nchi iitwayo tanzania. Ila wanatoa mbinyo kidogo ili kuwashikisha adabu wanaoanza kuota mapembe wanaodhani wanaweza kuikanyaga katiba na kujifanyia maamuzi watakavyo.

Tatizo maumivu huanzia kwa raia wa kawaida wakisha kongoroka yanahamia kwa vigogo. Baada ya hapo? Tunakwenda zimbabwe
Koo tumeota mapembe
 
Kila chuo kimedahili wanafunzi wengi mwaka huu. Bado nashindwa ku connect dots kwamba ni covid ndio chanzo au ni vipi.
 
Ni kweli kabisa

Na huwenda mwakani shinikizo likawa kubwa zaidi, maana kuna ambao waliapply, post zikatoka, lakini hawajaitwa chuoni bado kwa sababu ya korona.so bado wanasikilizia.
Na kuna wengine hata hizo post bado hazijatoka.

Sasa haya mambo ya korona yakiendelea hivhivi mpaka mwakani, watalazimika kuapply hapahapa nyumbani.
 
Back
Top Bottom