Chama kipya chaundwa Tanzania kuendeleza falsafa ya Magufuli

Falsafa ya kuendeleza kazi ya Magufuri itawasaidia sana lakini watakwama kwa sababu Magufuri hakupenda kukosolewa hivyo waanzilishi wake nao hawatopenda kukosolewa ili kulinda heshima ya Hayati Magufuri.
Comment yako sio appropriate.You can have a different style of managing politics na uka achieve the same goals.
 
Benjamin William Mkapa aliiweka Tanzania katika ramani ya dunia kiuchumi,kisiasa,kijamii na kidiplomasia kwa hiyo kama hukumpenda nenda ujinyonge ili wale tuliofaidi utawala wake tuendelee kumuenzi kwa mazuri yake.
Umesahau biashara Ikulu?Umesahau kuifanya Tanzania shamba la Bibi kwa kuwapa mabeberu rasilimali zetu kwa bei ya kutupa?Msitukumbushe.
 
Comment yako sio appropriate.You can have a different style of managing politics na uka achieve the same goals.
Don't force to speak or comment what you want yourself,am not Magufulist philosopher,my point is to remember a real President who was a president of people by that time he raised Tanzania from mud and made it louder in the whole world,his speeches,linguistic man and heavy thinker and creative person who made several institutions which are prevailing till now,Mr Benjamin Mkapa.
 
Hakika damu hizi hazitopotea bure,lile kubwa la maadui lazma liingie moton
Damu zipi,hizo picha za Kivu na CAR.Anyway,tunachosena ni hiki tushirikiane wote kuiletea nchi yetu maendeleo,kusitokee mmoja wetu akawa Covert CIA operative or whatever akatuvuta miguu nyuma,hiyo haitakubalika.
 
Huu ni usanii kama usanii mwengine wowote mwaka umeisha wako katika process ya kusubiria ofisi ya msajili wa vyama iseme chochote. Ofice isiposema mpaka 2040 watakuwa wakisubiria tu. Puaa puaa puaa×2
 
Sijawahi muona Beberu Tangu nizaliwe Tanzania kwa sababu nilizaliwa baada ya uhuru hivyo ukoloni na ubeberu sijawahi uona labda kidogo ukoloni uliibuka kipindi cha utawala wa awamu ya tano chini ya Kayafa mwendakuzimu.
Umesahau biashara Ikulu?Umesahau kuifanya Tanzania shamba la Bibi kwa kuwapa mabeberu rasilimali zetu kwa bei ya kutupa?Msitukumbushe.
 
Don't force to speak or comment what you want yourself,am not Magufulist philosopher,my point is to remember a real President who was a president of people by that time he raised Tanzania from mud and made it louder in the whole world,his speeches,linguistic man and heavy thinker and creative person who made several institutions which are prevailing till now,Mr Benjamin Mkapa.
Institutions?Tunataka institutions ziwasaidie watu,sio ziwe mzigo kwa watu.
 
UTANGULIZI
TAFADHALI NAOMBA NISIRUSHIWE MADONGO,MIMI NI MJUMBE TU.HATA HIVYO NIKIRI KWAMBA HILI WAZO NIMELIPENDA, INGAWA MIMI NI MWANA CCM.NIKIRI KWAMBA BAADA YA MIAKA 61 YA UHURU, BADO CCM INATUPIGISHA WATANZANIA MAKIDA MAKIDA.


Chama kipya cha kisiasa kimeanzishwa nchini Tanzania, kikiwa na lengo la kuendeleza sera na mtindo wa uongozi wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo John Pombe Magufuli.

Waanzilishi wa Umoja party wanaripotiwa kuwa wanachama na watu maarufu ndani ya chama kinachotawala cha CCM, ambao hawana furaha na uongozi wa sasa.

Mwanzilishi wa chama hicho Seif Maalim Seif, ameambia sauti ya Amerika VOA kwamba “Tuliwasilisha maombi ya usajili mwaka jana na tumefikia hatua ya marekebisho kadha wa kadha. Katika Ofisi ya msajili wa vyama kuna katiba na kanuni za chama chetu na vielezo vyote vinavyotakiwa.”

Baadhi ya vigogo wa CCM wanaunda Umoja party?

Kuna ripoti kwamba huenda watu maarufu na wa ngazi ya juu katika chama kinachotawala, ambao wangependelea Tanzania iongozwe namna alivyokuwa anaongoza aliyekuwa rais wa nchi hiyo hayatoi John Pombe Magufuli, ndio wanaosukuma kuundwa kwa chama cha umoja.

“Chama chetu kilifikia hatua ya kuwekwa kwenye gazeti la serikali mwezi Novemba mwaka jana kwa mda wa siku 21 kwa yeyote aliye na pingamizi. Kwa hivyo hiki chama sio kwamba watu wamejikusanya na kuamua kufanya hivi na hivi. Tunachosubiri ni maelekezo ya msajili wa vyama kwa ajili ya kupewa cheti cha usajili.” Amesema Maalim Seif.

Picha za watu ambao wamevalia fulana za chama cha umoja, zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii. Fulana hizo zina picha ya aliyekuwa rais wa Tanzania John Magufuli.

“sisi wa upande wetu hatuna deni lolote la mahitaji ya kisheria ya kutaka kusajiliwa. Ni Afisi tu ya msajili wa vyama kutuambia kiachofuata. Tulishamaliza mwaka mmoja sasa.” Ameongezea Seif Maalim Seif.

Malengo ya umoja party

Misingi ya chama hicho ni kuendeleza falsafa ya aliyekuwa rais John Mgufuli. Waanzilishi wake wanasema kwamba Tanzania sasa ipo katika hali ya sintofahamu, miongoni mwa vyama vya kisiasa huku hali ya maisha kwa watanzania ikiendelea kuwa ngumu, na kwamba ipo haja ya kufuata nyayo za Magufuli kuongoza taifa hilo.

Hata hivyo, Seif Maalim amesita kusema iwapo chama cha mapinduzi kina mapungufu kwa sasa kuendeleza falsafa ya Magufuli akisema kwamba “nadhani falsafa yake, kama chama cha mapinduzi kinaitumia au la, ni jukumu la wananchi wenyewe kuamua.”

Wanachama wengine wa Umoja party hata hivyo bado ni siri ya wenye chama.

“Jamii inaona ukweli ni akina nani wana dhati ya kumuenzi rais Magufuli. Wale ambao wapo tayari kupoteza nyadfa zao, na wale wanaoona kwamba falsafa ya Magufuli haitekelezwi. Siwezi kuwataja majina lakini dhamira zao zinajulikana.” Amesema Maalim Seif, akiongezea kwamba “wimbi la kisiasa ni la kawaida” akiwa anajibu swali iwapo kuundwa kwa umoja Party kutavuruga chama cha CCM ambacho alikipenda John Magufuli.

Mvutano ndani ya chama cha CCM

Mnamo mwezi Januari, mjadala mkali ulitokea Tanzania kuhusu deni la nchi hiyo linaloendelea kuongezeka, baadhi ya viongozi katika chama kinachotawala cha CCM wakisikika hadharani wakimkosoa rais Samia Suluhu Hassan kwa kile walisema ni “kuendelea kukopa kiholela” ili kufadhili miradi ya serikali.

Mjadala huo ulipelekea spika wa buge la taifa Job Ndugai kujiuzulu.

Ndugai alikuwa miongoni mwa viongozi wakuu wa CCM walikosoa uongozi wa rais Samia, ambaye baadaye alifanya mabadiliko serikali na kuwatimua baadhi ya viongozi, siku chache baada ya kusema hadharani kwamba angewatimua wale ambao wanataka kufanya siasa badala ya kutumikia wananchi kuleta maendeleo.

Imetayarishwa na Kennes Bwire, VOA, Washington DC

Hakuna kiongozi wa CCM atakayehama, hakika nakwambia.
 
Udikteta na ukabila uliuona wewe,sisi wengine hatukuuona.Subiri wananchi wataamua kwenye box la kura 2025.

Aliyeongea naye Ni mwananchi. Huyo Magufuli alizuia siasa kwa miaka mitano, je hicho chama na chenyewe kikizuiliwa kufanya siasa miaka mitano kitakubali?
 
Na zinatusaidia sana mfano,TRA inakusanya mapato ambayo yanafanya nchi isonge mbele,TCRA mawasiliano nchi nzima mambo ya barua tulishasahau,TAKUKURU watu wanajiliwa huko na kutnza familia zao,mambo mengi tena mengi sana kuyaeleza kimoja kimoja itakuchukua mwaka.
Institutions?Tunataka institutions ziwasaidie watu,sio ziwe mzigo kwa watu.
 
Sijawahi muona Beberu Tangu nizaliwe Tanzania kwa sababu nilizaliwa baada ya uhuru hivyo ukoloni na ubeberu sijawahi uona labda kidogo ukoloni uliibuka kipindi cha utawala wa awamu ya tano chini ya Kayafa mwendakuzimu.
Tumieni akili zenu mlizopewa na Mungu,msishikiwe akili.Ninyi mmeshikiwa akili,sio independent thinkers.Soft Power ya mabeberu imewaharibu.
 
Wataungwa mkono na walio wengi !!


Wachache wa juu ndo watawapinga!!.


Ukweli ni kua Magufuli alipendwa na walio wengi.

Sent using Jamii Forums mobile app

Acheni kuongea uongo na unafiki. Mtu anapendwa na wengi anapata asilimia 57 za Kura Tena za wizi. Na kuongezea mtu anayependwa anaweza kuharibu uchaguzi mkuu wa 2020. Magufuli alipendwa kinafiki kwa sababu ya dola.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom