Chama kipya cha Siasa kinachoitwa "Umoja Party" kuanzishwa

Sasa siwangeenda kufufua moja kati chausta, udpd maendeleo, and the kuliko kupoteza muda wa kusajili chama kipya
 
Je kina siasa za KIBEPARI. ? KIRIBELAR???? ama KIJAMAA????

Yote haya tunahitaji kujua
 
Chama chochote chenye mlengo, nia na Imani ya Nyerere au Magufuli hao nitakwenda nao
Chadema wanaamini wazungu ndio watatukomboa na dubwana lao lisu + Robertson,
CCM kimetekwa na majizi
Ngoja tuone kama huu umoja utazaa jambo gani.
Hakuna jipya hapo. Ni umoja wa wasaliti, vigeugeu na watafuta ruzuku.
 
Wangekiita Magufuli Party
Magufuli peoples Party kipo tayari na Nembo yake ni hii sijui kwanini Wanachelewa kukisajili ila TWITTER kina mwanga Sera zake
Screenshot_20210704-161108_Twitter.jpg
 
Wangekiita Magufuli Party
Kama ni #TeamMagufuli ndiyo wameanzisha chama hicho kama wangenitaka ushauri mapema basi mimi ningewashauri waachane na mpango huo usioweza kuzaa matunda badala yake wangeanzisha MAGUFULI FOUNDATION ili kumuenzi vizuri na labda kama zilivyo Nyerere Foundation, Mkapa Foundation na Kikwete Foundation huenda nacho kingezaa matunda mazuri ya kumuenzi. Mwenye masikio na asikie! Asomaye na afahamu!
This is Africa Bwana!
 
Demokrasia ya vyama vingi inazidi kushamiri Tanzania.

Angalizo, Kamwe wasikigeuze chama kuwa Genge la Kihalifu kama walivyo fanya viongozi wa Chadema.

Chama cha siasa lazima kiwe kweli chama cha kisiasa.
HIVI CCM ni chama Cha siasa? Kina hati ya USAJILI?
 
Mapema sana
Nanukuu toka kwa Bulesi "Sukuma........ waaanzisha Chama chao kumuenzi mwendazake!!!"

My take.
Japokuwa Wasukuma pekee wako 16% ya population ya nchi kati ya makabila 120 wakikalia mikoa 6 (kati ya 31) yenye utajiri wa uchumi wa bluu (Ziwa Victoria), mifugo, ardhi oevu na anuai, miundombinu ya aina zote (barabara, madaraja ya ardhini na majini, viwanja vya ndege viwili vya hadhi ya Kanda (Regional Airports na Airstrips nyingi)), reli za aina mbili za MGR na SGR, hifadhi 6 katika ushoroba wa Kaskazini kati ya hifadhi 22 za taifa, mapori makubwa ya akiba, mito mikubwa ya kudumu, mabonde mazuri, mazao ya chakula na biashara, jiografia kuiweka katikati ya EAC na Maziwa Makuu, kuwa na asilimia takriban zaidi ya 50% ya migodi yote ya nchi, wasomi mahiri, na hivi sasa wakisambaa takriban mikoa yote ya bara kupitia ufugaji wa kuhamahama (#wamenyimwa nini!), bado naamini hawawezi kufua dafu kujiundia chama ili kuking'oa CCM (CCM kiliaga kwao). Bado sana!
 
Sasa Bashiru kuwa mwenyekiti wa chama ndio anguko lingine kwa hilo zoezi!?

Wengi wa wanasiasa wa vyama pinzani Tanzania hawana nia ya dhati ya kupeleka nchi kwenye maendeleo ya watu. Ndio maana upinzani unazidi kuwa dhaifu siku baada ya siku

Mungu ibariki Tanzania
Upinzani Kama ni DHAIFU dola ingeingilia? Wakifanya jogging tu tayari Polisi hawa hapa, mikutano wa ndani tu, Polisi hawa hapa. Upinzani dhaifu sasa uachwe huru tuone CCM kama watakuwepo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom