Filosofia ya Rorya
JF-Expert Member
- Sep 20, 2021
- 3,214
- 3,587
Mkuu Eliasmisinzo,HIVI CCM ni chama Cha siasa? Kina hati ya USAJILI?
Ngoja niwaambie, CCM siyo chama cha siasa, CCM ni #Dini kama zilivyo dini zingine kama Ukristo, Uislamu, Udruze, Bahai, Uyahudi, Kurd, Aramean, Armenia, Upagani, Budha nk. Ni makosa makubwa yasiyosahishika kwa kanuni yoyote ile kuamini kwamba CCM ni chama cha siasa, la hasha! CCM ni #Dini na ndani ya Dini ya CCM kuna Madhehebu (Mitandao na Vyama unavyoweza kuviita Vibaraka), na ijulikane kuanzia leo kwamba hakuna mtu anaweza kuvunja Dini (ikiwemo Dini ya CCM), Hitler, Musolini, Mao, Botha, Karl Marx, Socrates, Galileo Galilee, Plato, Paulo Mtume, Martin Luther, Mafarao wote 40, Makaisari wote 12, Mapapa wote 266 walijaribu lakini hawakuweza kuvunja Dini yoyote chini ya jua, itakuwa mimi na wewe tuliolelewa kwa samaki za Ziwa Victoria na ndizi za Moshi ndiyo tuivunje CCM? Namshauri mtu yeyote atubu kwa kuamini kinyume na ukweli huu.
Tafsiri yangu hii itaishi kutimia japo leo naweza kupopolewa mawe kwayo kama Socrates 399 BC.