Chama kipi kinasimamia Haki?

Nakwetu

Member
Apr 27, 2009
72
11
Viti maalum zimetangazwa. Chadema kimepata viti 23, hongera sana.
Jinsi chama kinavyopigania haki kwa wananchi sikutegemea kama nao hivyo viti watagawana kwa upendeleo mkubwa.
Kuna mkoa kama Mwanza na Shinyanga umetoa wabunge wengi ambao ndio ilitosababisha chama kupata viti vingi, wameambulia patupu!. Wanawake waliogombea majimboni waliahidiwa wakikosa watapewa, wasio na ndugu ngazi za juu za chama Hawakupata.
Ni utaratibu upi umetumika Kilimanjaro viti 3, Dsm viti 3, Manyara na Moro na Singida viti 2 kila moja? Je huu sio UKANDA!
Hebu angalieni hiyo mikoa ndio mtajua naongea nini. Sasa nimeona kumbe Chadema ikipata haina tofauti na CCM. Heri tena CCM maana inaeleweka waliochukuliwa ni wale walioongoza mikoani mwao kwa chaguzi za UWT ambazo nayo ilikuwa ni RUSHWA tupu iliyotawala.
 
Hauwezi kwenda kukurupuka kuwapa tu watu ubunge eti kwa sababu wametoa wabunge wengi. Je kama hakukuwa na kina dada competent wa kupewa hiyo nafasi? Kumbuka ubunge sio halua au tende useme unapewa tu bob...CHADEMA bado ni chama kidogo watu wengi wanaogopa hata kujiunga nacho hivyo subiri 2015 kutakuwa na wadada makini toka mikoa unayo sema na watapewa ubunge wakidhibitika ni makini.
:bowl:
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom