mwongozo junior
Senior Member
- Jul 28, 2015
- 180
- 64
Wanajukwaa habari zenu
Siyo vibaya tukajadili muungano Wa ukawa baada ya uchaguzi. Najua kuna malakamiko mengi kuhusu kura Nk... lakini naomba tuchukulie /tukubali kuwa matokeo yalishatangazwa na tume na mlango umefungwa. Tufikirie mipango ya 2020.
Je chama kipi cha ukawa kimefaidi zaidi KISIASA kuliko vingine?
URAIS
Bila shaka ulikua uamuzi mgumu kwa cuf na nccr (khasa cuf) kukubali kutosimamisha mgombea urais ili kumuachia mgombea Wa ukawa (chdm). Ikumbukwe kuwa mgombea urais huongeza umaarufu Wa chama kwa kuzunguka nchi nzima. Chama kinaposhiriki uchaguzi bila mgombea urais hupunguza umaarufu na nguvu zake. Kura za urais pia huchangia kwenye ongezeko LA ruzuku kutoka serikalini.
Kwa hili LA mgombea urais naona chdm kimefaidi zaidi. Japo ni kura za ukawa lkn kiuhalisia (kwa mujibu Wa NEC) hizo kura milioni 6 plus ni za chadema. Ruzuku ya chadema itaongezeka sana hivyo kusaidia ktk uendeshaji Wa chama.
Je cuf na nccr wanastahiki kila mwezi kupewa asilimia ndogo kwenye hii ruzuku au yote itakua ya chadema? Tujadili. Wasipopewa hudhani kuwa muungano Wa ukawa utayumba? Haitaonekana kuwa chadema ilivitumia nccr, cuf na nld kama ngazi?
Je ujio Wa lowassa ulochangia hizo kura utaijenga chdm baada ya uchaguzi au utaibomoa? Chadema imefaidi kisiasa kwa kumleta lowassa kwenye urais au itaathirika negatively kwa kumleta?
UBUNGE
Nccr ilikua na wabunge 4 bunge lilopita. Kwa uchaguzi huu imepata mbunge 1. Ni neema au nakama? Ukawa imeisaidia nccr au imeingamiza?
Cuf ilikua na wabunge 2 (kutoka bara) bunge lilopita. Sasa hivi imepata wabunge 10 bara. hili ni ongezeko la zaidi ya 90%. In neema au hasara?
Chadema iilikua na wabunge 25 bunge lilopita. Sasa hivi ina 34. Ongezeko LA chini ya asilimia 20. Je ni neema au hasara kwa chadema?
Naomba tujadili. Kama nimekoseya kwenye idadi ya wabunge napokea masahihisho.
Siyo vibaya tukajadili muungano Wa ukawa baada ya uchaguzi. Najua kuna malakamiko mengi kuhusu kura Nk... lakini naomba tuchukulie /tukubali kuwa matokeo yalishatangazwa na tume na mlango umefungwa. Tufikirie mipango ya 2020.
Je chama kipi cha ukawa kimefaidi zaidi KISIASA kuliko vingine?
URAIS
Bila shaka ulikua uamuzi mgumu kwa cuf na nccr (khasa cuf) kukubali kutosimamisha mgombea urais ili kumuachia mgombea Wa ukawa (chdm). Ikumbukwe kuwa mgombea urais huongeza umaarufu Wa chama kwa kuzunguka nchi nzima. Chama kinaposhiriki uchaguzi bila mgombea urais hupunguza umaarufu na nguvu zake. Kura za urais pia huchangia kwenye ongezeko LA ruzuku kutoka serikalini.
Kwa hili LA mgombea urais naona chdm kimefaidi zaidi. Japo ni kura za ukawa lkn kiuhalisia (kwa mujibu Wa NEC) hizo kura milioni 6 plus ni za chadema. Ruzuku ya chadema itaongezeka sana hivyo kusaidia ktk uendeshaji Wa chama.
Je cuf na nccr wanastahiki kila mwezi kupewa asilimia ndogo kwenye hii ruzuku au yote itakua ya chadema? Tujadili. Wasipopewa hudhani kuwa muungano Wa ukawa utayumba? Haitaonekana kuwa chadema ilivitumia nccr, cuf na nld kama ngazi?
Je ujio Wa lowassa ulochangia hizo kura utaijenga chdm baada ya uchaguzi au utaibomoa? Chadema imefaidi kisiasa kwa kumleta lowassa kwenye urais au itaathirika negatively kwa kumleta?
UBUNGE
Nccr ilikua na wabunge 4 bunge lilopita. Kwa uchaguzi huu imepata mbunge 1. Ni neema au nakama? Ukawa imeisaidia nccr au imeingamiza?
Cuf ilikua na wabunge 2 (kutoka bara) bunge lilopita. Sasa hivi imepata wabunge 10 bara. hili ni ongezeko la zaidi ya 90%. In neema au hasara?
Chadema iilikua na wabunge 25 bunge lilopita. Sasa hivi ina 34. Ongezeko LA chini ya asilimia 20. Je ni neema au hasara kwa chadema?
Naomba tujadili. Kama nimekoseya kwenye idadi ya wabunge napokea masahihisho.