Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Muswada mpya wa katiba ni kielelezo kuwa Chama Cha Mapinduzi bado hakiko tayari kuleta usawa na haki katika taifa hili.
Wakati wengi wetu wakijawa na matumaini kuwa huenda kukawa na mabadiriko tunayoyataka kufuatia kujiudhuru kwa CC na NEC ya CCM ndani ya chama hiki kikongwe binafsi naona hii ni fursa nyingine ya kuongeza muda na kuwalaghai watanzania. Matamanio ya CCM ni kuhakikisha kuwa kinaminya uhuru hata kidogo uliopo ili kuhakikisha kuwa kundi la watawala wanaendelea kuwepo kupitia vibaraka wao.
Kama kweli CCM ilikuwa na nia ya kuleta mabadiriko yanayotarajiwa ingekuwa mstari wa mbele kuikemea serikali yake iondokane na mpango wa kupeleka muswada wa ajabu na hii, ingewaomba wabunge wake wasiuunge mkono, lakini kwa sababu hiki ni chama cha kidhalimu kimebariki udhalimu huu na bado kinataka kutudanganya kuwa kimeanza kupambana na ufisadi kwa kuwaondoa makada wake wanaotuhumiwa kwa ufisadi kutoka kwenye vyombo vyake vya maamuzi.
Nionavyo CCM siyo chama cha kuaminika hata kidogo, hawa wanatakiwa wawajibishwe kwa kunyimwa idhini ya kututawala wakae pembeni watu wengine nao watumikie hatutaki kuletewa mvinyo ule ule kweny chupa mpya
Wakati wengi wetu wakijawa na matumaini kuwa huenda kukawa na mabadiriko tunayoyataka kufuatia kujiudhuru kwa CC na NEC ya CCM ndani ya chama hiki kikongwe binafsi naona hii ni fursa nyingine ya kuongeza muda na kuwalaghai watanzania. Matamanio ya CCM ni kuhakikisha kuwa kinaminya uhuru hata kidogo uliopo ili kuhakikisha kuwa kundi la watawala wanaendelea kuwepo kupitia vibaraka wao.
Kama kweli CCM ilikuwa na nia ya kuleta mabadiriko yanayotarajiwa ingekuwa mstari wa mbele kuikemea serikali yake iondokane na mpango wa kupeleka muswada wa ajabu na hii, ingewaomba wabunge wake wasiuunge mkono, lakini kwa sababu hiki ni chama cha kidhalimu kimebariki udhalimu huu na bado kinataka kutudanganya kuwa kimeanza kupambana na ufisadi kwa kuwaondoa makada wake wanaotuhumiwa kwa ufisadi kutoka kwenye vyombo vyake vya maamuzi.
Nionavyo CCM siyo chama cha kuaminika hata kidogo, hawa wanatakiwa wawajibishwe kwa kunyimwa idhini ya kututawala wakae pembeni watu wengine nao watumikie hatutaki kuletewa mvinyo ule ule kweny chupa mpya