Chama Hiki Hata Ukitendee Mema Kitakulipa Mabaya Tu.

Waga

JF-Expert Member
Feb 6, 2008
322
14
Mlala hoi ambaye hawezi kumudu mlo kamili kwa siku anakuwa na matumaini pale anapoamua kukipigia kura chama hiki, na chama alichokichagua kinampa ahadi hizi

Tuta watengenezea ajira milioni moja
Tutawaletea maisha bora kwa kila mtanzania
Tutawatengenezea bara bara nzuri
Tutahakikisha hakuta kuwa na shida ya maji.

Mbaya zaidi hao hao tuliowapa kura wapo ambao wameamua kujinufaisha wao wenyewe na familia zao kwa kuamua kuitumbukiza nchi hii kwa kuchota mahela ambayo ni wazi ni za walipa kodi.

Hawa hawa tuliowapa kura wameamua kuwatetea wale wote waliojichotea mapesa ya walipa kodi kwa kutuambia..

Lowasa hausiki na sakata la Richmond
Karamagi hausiki na sakata la Richmond
Chenge pesa alizokutwa nazo hajavunja nyumba kuiba
Pesa za Epa si pesa za serikali
Report ya madini mpaka leo hatujaisikia

Haya ni machache tu kati ya mengi ambayo wanachi waliowapa kura wangependa kusikia mustakhabali wake lakini yaonekana dhahiri kuna mpango wa kuyazima na yameshaanza kupotea taaratibu.

Kinachouma zaidi ni pale wanaposahau kuwa tumewateua kuwa wapigania maslahi ya walalahoi wa Tanzania kwa kuonyesha wazi nia ya kuwanyamazisha wale wanaoonekana kuguswa na shida zilizokithiri hapa nchini kwa kuamua kutetea moja kwa moja maslahi ya Taifa hili. Tumeona wazi juzi kwa kuamua kutoonyesha hotuba ya kambi ya upinzani kuhusu bajeti ya waziri mkuu, inawabidi muelewe wazi kuwa hapo mnawakilisha wanachi na tungependa kujua nini kinachoendelea na si kuwanyima fursa hiyo.

Ni mengi sana ambayo tumeahidiwa na chama hiki lakini mpaka leo hii hakuna utekelezaji kiasi kwamba baadhi ya wabunge wake wanadiriki kusema ndani ya bunge kuwa wasipotekelezewa ahadi zao walizopewa na serikari kama hazitatekelezwa hatatoka mtu ndani ya bunge.

Cha kujiuliza hapa ni kwa nini hata wabunge wao wanafikia maamuzi ya kusema hivi ?
Ni dhahiri wamechoshwa na ahadi hewa za serikali ya chama chao ndo mana wanaamua kusema hayo wanayoyasema, na kama mbunge anachoshwa mwananchi wa kawaida ambaye hana uhakika wa kula mlo kamili kwa siku anafikiriwaje ?

TUMETENDA MEMA KUWACHAGUA LAKINI DHAHIRI MMETULIPA MABAYA
 
Mlala hoi ambaye hawezi kumudu mlo kamili kwa siku anakuwa na matumaini pale anapoamua kukipigia kura chama hiki, na chama alichokichagua kinampa ahadi hizi

Tuta watengenezea ajira milioni moja
Tutawaletea maisha bora kwa kila mtanzania
Tutawatengenezea bara bara nzuri
Tutahakikisha hakuta kuwa na shida ya maji.

Mbaya zaidi hao hao tuliowapa kura wapo ambao wameamua kujinufaisha wao wenyewe na familia zao kwa kuamua kuitumbukiza nchi hii kwa kuchota mahela ambayo ni wazi ni za walipa kodi.

Hawa hawa tuliowapa kura wameamua kuwatetea wale wote waliojichotea mapesa ya walipa kodi kwa kutuambia..

Lowasa hausiki na sakata la Richmond
Karamagi hausiki na sakata la Richmond
Chenge pesa alizokutwa nazo hajavunja nyumba kuiba
Pesa za Epa si pesa za serikali
Report ya madini mpaka leo hatujaisikia

Haya ni machache tu kati ya mengi ambayo wanachi waliowapa kura wangependa kusikia mustakhabali wake lakini yaonekana dhahiri kuna mpango wa kuyazima na yameshaanza kupotea taaratibu.

Kinachouma zaidi ni pale wanaposahau kuwa tumewateua kuwa wapigania maslahi ya walalahoi wa Tanzania kwa kuonyesha wazi nia ya kuwanyamazisha wale wanaoonekana kuguswa na shida zilizokithiri hapa nchini kwa kuamua kutetea moja kwa moja maslahi ya Taifa hili. Tumeona wazi juzi kwa kuamua kutoonyesha hotuba ya kambi ya upinzani kuhusu bajeti ya waziri mkuu, inawabidi muelewe wazi kuwa hapo mnawakilisha wanachi na tungependa kujua nini kinachoendelea na si kuwanyima fursa hiyo.

Ni mengi sana ambayo tumeahidiwa na chama hiki lakini mpaka leo hii hakuna utekelezaji kiasi kwamba baadhi ya wabunge wake wanadiriki kusema ndani ya bunge kuwa wasipotekelezewa ahadi zao walizopewa na serikari kama hazitatekelezwa hatatoka mtu ndani ya bunge.

Cha kujiuliza hapa ni kwa nini hata wabunge wao wanafikia maamuzi ya kusema hivi ?
Ni dhahiri wamechoshwa na ahadi hewa za serikali ya chama chao ndo mana wanaamua kusema hayo wanayoyasema, na kama mbunge anachoshwa mwananchi wa kawaida ambaye hana uhakika wa kula mlo kamili kwa siku anafikiriwaje ?

TUMETENDA MEMA KUWACHAGUA LAKINI DHAHIRI MMETULIPA MABAYA

waga,

hii imetulia mwanawane!

Imebidi nitulie kidogo na kutafakari...
 
Ndio maana serikali ikiongozwa na CCM inapinga hoja ya wagombea binafsi, wanajua sana kuwa watakimbiwa na wengi
 
akutendeae ubaya na wewe mlipe ubaya......mwka 2010 hakikisha kura yako na ya jamii yako ya karibu haiendi tena kwa waliokulipa baya.
ahsante
 
Tupo pamoja mwk, maana inauma hawa jamaa wanapotupeleka sipo kabisa, tunaongopewa hivi hivi, naona wamejisahau kuwa limbwata tulilolishwa la kusahau mabaya yanayotendwa na viongozi limeshaanza kuisha sasa wangojee watapata majabu soon
 
Tupo pamoja mwk, maana inauma hawa jamaa wanapotupeleka sipo kabisa, tunaongopewa hivi hivi, naona wamejisahau kuwa limbwata tulilolishwa la kusahau mabaya yanayotendwa na viongozi limeshaanza kuisha sasa wangojee watapata majabu soon

Ukiona watu wamefikia hatua ya kupeleka uchawi dodoma basi ujue maji yako shingoni. Hesabu siku tu ... tik tak tik tak
 
Hakuna marefu yasiyokuwa na mwisho, CCM inajimaliza yenyewe. Ngoja angalau hata tuweze kupata manufaa ya raslimali zetu. watu wanakula hata bila kunawa. halafu eti visenti ndo pesa, Eti nimewajibika kama mwinyi (kwani mwinyi aliiba?).
 
Wapo wengi sana ambao wameonyesha udhaifu kwa kutaka kuendelea kuwapumbaza watanzania juu ya issues za richmond na epa sasa mtu kama mzindakaya ambaye na yeye amejichotea mapesa B.O.T na kufungua miradi huko kwao kwela naye anaendelea kutetea uchafu huu kwa kusema haina haja ya kuijadili tena eti tusubiri maamuzi ya serikali kweli ni halali?? Hainiingii akilini kuona watu ambao wamelitia hara kubwa taifa hili wanaendelea kutanua tuu na mavx yao uku wakisubiri serikali itoe majibu while waliokamatwa kuhusiana na kuanguka kwa ghorofa maamuzi ya haraka haraka wanachukuliwa juu ya na vyombo hivi hivi vya serikali sasa nani anayestahili kutolewa maamuzi ya haraka kati ya watu hawa?
Ghorofa amefariki mtu mmoja (1)
Mipesa ya Richmond je?? ( wangapi wamekufa kutokana na huduma mbovu mahospitalini??? kama hizo pesa zingeingia kwenye kununua vifaa vya mahospitalini zisingesaidia?)
Epa je? Hiyo mihela si ingeingia kwenye mradi wa mabasi yaendayo kasi angalau mpunguze makali ya usafiri kwa wapiga kura wenu ili angalau wawahi kwenye vituo vyao vya kazi ambapo wakichelewa mnawapa barua za onyo while nyie mnawahi na mavx yenu?
Chenge's billions huko naomba hata nisiseme maana inauma kiasi kwamba machozi yanelenga lenga
 
Tatizo tutapiga kelele weeeee...2010 wanarudi tena vile vile..tupelekeni elimu huko vijijini jamani..huko ndio kunakotu cost.......tusambazeni hii elimu ya uraia kama injili...wale walioko huko ambao ndio hazina kubwa ya CCM nao wawe na machungu kama yetu
 
mWISHO WA MWISHO WA MWISHO, WALISEMA menemene tekeli na Peresi maana yake utawala wako umekoma na umetupiliwa mbali Wakristo na wasomaji wa Biblia mnanielewa ,KURAN sijui imeandikaje .
 
Wakunyuti Re: Chama Hiki Hata Ukitendee Mema Kitakulipa Mabaya Tu.

--------------------------------------------------------------------------------
Tatizo tutapiga kelele weeeee...2010 wanarudi tena vile vile..tupelekeni elimu huko vijijini jamani..huko ndio kunakotu cost.......tusambazeni hii elimu ya uraia kama injili...wale walioko huko ambao ndio hazina kubwa ya CCM nao wawe na machungu kama yetu

Naungana na wewe mia kwa mia kwa sababu vijijini ni wepesi sana kudanganyika once wanapopewa t'shirt na kofia, kule hawasikii TBC, hawapati MAGAZETI so they dont know whats going on juu ya chama wanachokipigia kura.
 
wakunyuti Re: Chama Hiki Hata Ukitendee Mema Kitakulipa Mabaya Tu.

--------------------------------------------------------------------------------
Tatizo Tutapiga Kelele Weeeee...2010 Wanarudi Tena Vile Vile..tupelekeni Elimu Huko Vijijini Jamani..huko Ndio Kunakotu Cost.......tusambazeni Hii Elimu Ya Uraia Kama Injili...wale Walioko Huko Ambao Ndio Hazina Kubwa Ya Ccm Nao Wawe Na Machungu Kama Yetu

Naungana Na Wewe Mia Kwa Mia Kwa Sababu Vijijini Ni Wepesi Sana Kudanganyika Once Wanapopewa T'shirt Na Kofia, Kule Hawasikii Tbc, Hawapati Magazeti So They Dont Know Whats Going On Juu Ya Chama Wanachokipigia Kura.



Tulia Tu Dawa Yao Inaiva Jikoni Wameiandaa Wenyewe Si Muda Mrefu Tutakuwa Na Form Leavers Wengi Kila Kta Huko Vijijini Kutoka Katika Shule Za Secondary Za Kata.
Mimi Nimeisha Liona Hilo. Ccm Wakiendelea Kukumbatia Wezi Itawagharimu Sana Na Viongozi Wa Sasa Wataingia Katika Historia Ya Tz Ya Kuiangusha Chama Kikubwa Cha Ccm.

Wakifanikiwa Sana 2010 Lakini 2015 Ita Wa Ngumu Saaaaaaaaaaaaana! Wao Kundelea Labda Wachenji Staili Ya Utawala Wa Kukumbatia Wezi Wachache Na Kuamua Kukumbatia Maslahi Ya Wengi!
You Will Tell Me!

Tutakuwa Na Form 4 Amd 6 Leavers Wengi Wao Wakiwa Na Diviaon Zero Na Four Lakini Watakuwa Na Mawazo Ya Kimapinduzi Kwa Sababu Watakuwa Na Maisha Magumu Na Mabaya
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom