BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Muswada wa Katiba: Kikwete sasa njia panda
na Grace Macha, Arusha
Tanzania Daima
CHAMA cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kuwasikiliza wananchi wanaopinga Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 kwa madai kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa sheria za nchi, taratibu na kanuni za Bunge, na kimesema wataenda mahakamani kufungua kesi ya Kikatiba kuupinga iwapo Rais atausaini.
Rais wa chama hicho , Francis Stolla, aliyasema hayo juzi alipokuwa akitoa mada katika mjadala juu ya ushiriki wa wananchi wa jamii za wawindaji, wakulima, wafugaji, warina asali na waokota matunda asili kwenye mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya ulioandaliwa na jukwaa la umoja wa mashirika yasiyo ya kiserikali ya wafugaji na wakusanya matunda ya asili (PING's Forum) uliofanyika mjini Arusha.
Alisema kuwa Rais Kikwete anapaswa kuliepusha taifa na vurugu kwa kusilikiliza maoni ya wananchi wengi kwa vile haikuwa haki kuchukua maoni ya wananchi wachache kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma na Zanzibar.
"Rais asisaini muswada huo kuwa sheria kwa sababu ni kweli kwamba maoni yaliyokusanywa kwenye mikoa ya Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar ni ya wachache tu na bado tulishuhudia vurugu kubwa hadi Katiba ikichanwa ….tunataka haki ya wananchi kutoa maoni iwe kweli si kwenye makaratasi na wala wananchi wasinyimwe kwa kuhisi kuwa wakipewa fursa hiyo hawataitumia," alisema Stolla.
Alisema kuwa wameunda kamati maalum ya wanasheria watano inayoongozwa na Prof. Angelo Mapunda wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam kwa ajili ya kufanya utafiti juu ya vipengele vya sheria vilivyokiukwa jambo litakalowawezesha kwenda mahakamani endapo Rais Kikwete ataamua kusaini mswada huo.
Rais huyo wa TLS alitaja baadhi ya mapungufu hayo kuwa ni suala la kuwapo kwa miswada miwili ambapo ule wa lugha ya Kiingereza uliowasilishwa bungeni mwezi wanne mwaka huu na kusomwa bungeni mara tatu wakati ule wa Kiswahili uliwasilishwa bungeni kwa mara ya kwanza mwezi Novemba mwaka huu na ukapitishwa ukiwa umesomwa mara mbili jambo alilodai kuwa ni kinyume cha sheria.
Alisema kuwa muswada huo uliopitishwa unaendelea kuminya haki ya wananchi katika kutoa maoni kwani kimewekwa kipengele ambacho endapo mwananchi atatoa maoni ya kupinga vipengele ndani ya muswada huo basi anaweza kushtakiwa kwa kutenda kosa la jinai ambalo adhabu yake itakuwa kifungo cha miaka mitatu jela.
Stolla alisema kuwa hata muundo wa Bunge la Katiba una kasoro kwa kile alichosema kuwa kwa namna lilivyoainishwa ndani ya muswada huo umekaa kisiasa zaidi kwani idadi ya watu kutoka makundi mengine mbali ya kuwa hawajaainishwa bayana lakini ni ndogo hivyo kuna hatari Katiba hiyo ikaundwa kwa kuzingatia na kukidhi matakwa ya wanasiasa zaidi.
Alisema kuwa baada ya kosa hilo kufanyika kimbilio pekee lililobaki kuhakikisha muswada huo unarudishwa bungeni kisha kwa wananchi ili wapatiwe fursa ya kusikilizwa ni kwa Rais Kikwete kutousaini.
"Hatutanyamaza tutasema mapungufu yaliyopo kisheria, sisi kama wanasheria na wanaharakati hatutengenezi fursa zozote za kiuongozi wa kisiasa, tunasema Rais awasikilize wananchi aurudishe muswada huo bungeni, lakini akikataa tutaenda mahakamani," alisema Stolla.
Bunge: Muswada wa Katiba unaweza kubadilishwa
Kwa upande wake Bunge limesema kuwa Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya mwaka 2011 unaweza kubadilishwa au kufutwa wote endapo itaonekana kuna sababu za msingi za kisheria kufanya hivyo.
Taarifa iliyotolewa jana na Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Ushirikiano wa Kimataifa ya Bunge, imebainisha kuwa ikiwa muswada huo utasababisha mtazamo tofauti, unaweza kufanyiwa marekebisho kwa kuzingatia kanuni na taratibu kama inavyokuwa wakati mwingine wowote linapokuja suala la kurekebisha sheria za nchi.
Hata hivyo, taarifa hiyo imesema kuwa Bunge halikuvunja kanuni wala sheria yoyote ya nchi wala sababu ya msingi kuzuia muswada huo usisomwe kwa mara ya pili, kwa kuwa ulikidhi mahitaji yote kikanuni.
Taarifa imesema kuwa muswada huo ni halali na ukiwekwa saini na Rais utaendelea kusimamiwa na kutekelezwa kama sheria nyingine yoyote.
Ilisema muswada huo ni kama mwingine wowote uliowahi kupitishwa na Bunge; na ni wa kawaida ambao unaweka utaratibu wa kuwafikia wananchi, kuwasikiliza, kupata utashi wao juu ya mapendekezo ya kuandika Katiba mpya ili kila Mtanzania aweze kushirikishwa kwa wakati husika moja kwa moja.
Taarifa hiyo imebainisha kuwa Bunge limewashangaa baadhi ya wabunge waliosusia kikao cha kujadili muswada huo kwani wamewanyima fursa wananchi hao kuwakilisha maoni yao.
Ilibainisha hakukuwa na sababu za msingi kwao kulalamika wakati ikizingatiwa kwamba kambi zote ziliwasilisha na kupitisha mapendekezo ya muswada huo ili wananchi waulizwe kuhusu wanachokitaka kiingizwe katika Katiba mpya.
Iliongeza kuwa muswada huo hauhitaji ushiriki wa moja kwa moja wa wananchi isipokuwa kupitia kwa wawakilishi wao.
Taarifa hiyo ilibainisha kuwa muswada huo ulilenga katika kuweka chombo ambacho kitafanya kazi ya kuchukua maoni ya wananchi ili kuyapeleka katika Bunge la Katiba, ambalo, litakuwa na nafasi ya uwakilishi wa kila mtu.
Imesema Bunge limeuchambua muswada wa sheria na kuupitisha kuwa sheria na sio muswada wa kubadilisha Katiba kwa kuwa Katiba sasa haitobadilishwa, bali itaandikwa upya na serikalil iliyo madarakani kwa sasa na Bunge lake.
Mapema wakichangia katika mjadala huo jana, wengi wa washiriki walielezea mapungufu ya sheria katika ugawaji na umilikaji wa ardhi kwenye maeneo ya wafugaji, wawindaji na waokota matunda ambapo walitaka haki zao ziainishwe kwenye Katiba tofauti na sasa ambapo mara kwa mara wamekuwa wakiondolewa kwenye maeneo yao kuwapisha wawekezaji kwa kile wanachoambiwa wanaondolewa kwa maslahi ya umma.
Aidha walitaka Katiba mpya itambue uwepo wa Wamasai ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na kuendesha kilimo cha kujikimu, kujenga zahanati na shule badala ya kuwaachia uhuru wageni kujenga mahoteli na nyumba nyingine katika hifadhi hizo.
Katika hatua nyingine Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), limemshukia Spika wa Bunge Anne Makinda, kutokana na kupitisha Muswada wa Sheria ya Kuunda Katiba Mpya ambao ni kandamizi kwa wanawake nchini.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Mwenyekiti wa baraza hilo, Susan Lyimo, alisema Spika yuko kimaslahi ya chama tawala (CCM), badala ya wanawake.
"Tunawaomba wanawake wote watuunge mkono kwani athari za muswada ni nyingi na muathirika mkubwa atakuwa mwanamke, kitendo cha Makinda sio cha kiungwana mbele ya wanawake na umma wa Watanzania," alisema.
Alisema uamuzi wa Spika Makinda na Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani, kukataa maoni ya wanawake na hatimaye kupitisha muswada huo ni jambo la kulaaniwa.
Susan alisema suala la Katiba ni nyeti, na si mali ya CCM bali ya Watanzania wote hivyo yasiruhusiwe makundi ya watu wachache wenye malengo ya kulinda maslahi yao kuamua mustakabali wa nchi.
Alisema muswada huo ni janga kwa taifa kwani unaweka wazi kwa mtu atakayetoa elimu ya uraia kuhusu sheria hiyo atafungwa miaka mitatu.
Akifafanua juu ya upotoshwaji na propaganda zilizofanywa na CCM na CUF alisema hali hiyo inaweza kuleta machafuko ambayo athari kubwa itakuwa kwa wanawake, watoto na wananchi wenye ulemavu. Na propaganda zilizofanywa na wabunge wanawake juu ya Muswada huo ni za kupuuzwa.
na Grace Macha, Arusha
Tanzania Daima
CHAMA cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kuwasikiliza wananchi wanaopinga Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 kwa madai kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa sheria za nchi, taratibu na kanuni za Bunge, na kimesema wataenda mahakamani kufungua kesi ya Kikatiba kuupinga iwapo Rais atausaini.
Rais wa chama hicho , Francis Stolla, aliyasema hayo juzi alipokuwa akitoa mada katika mjadala juu ya ushiriki wa wananchi wa jamii za wawindaji, wakulima, wafugaji, warina asali na waokota matunda asili kwenye mchakato wa uundwaji wa Katiba mpya ulioandaliwa na jukwaa la umoja wa mashirika yasiyo ya kiserikali ya wafugaji na wakusanya matunda ya asili (PING's Forum) uliofanyika mjini Arusha.
Alisema kuwa Rais Kikwete anapaswa kuliepusha taifa na vurugu kwa kusilikiliza maoni ya wananchi wengi kwa vile haikuwa haki kuchukua maoni ya wananchi wachache kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma na Zanzibar.
"Rais asisaini muswada huo kuwa sheria kwa sababu ni kweli kwamba maoni yaliyokusanywa kwenye mikoa ya Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar ni ya wachache tu na bado tulishuhudia vurugu kubwa hadi Katiba ikichanwa ….tunataka haki ya wananchi kutoa maoni iwe kweli si kwenye makaratasi na wala wananchi wasinyimwe kwa kuhisi kuwa wakipewa fursa hiyo hawataitumia," alisema Stolla.
Alisema kuwa wameunda kamati maalum ya wanasheria watano inayoongozwa na Prof. Angelo Mapunda wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam kwa ajili ya kufanya utafiti juu ya vipengele vya sheria vilivyokiukwa jambo litakalowawezesha kwenda mahakamani endapo Rais Kikwete ataamua kusaini mswada huo.
Rais huyo wa TLS alitaja baadhi ya mapungufu hayo kuwa ni suala la kuwapo kwa miswada miwili ambapo ule wa lugha ya Kiingereza uliowasilishwa bungeni mwezi wanne mwaka huu na kusomwa bungeni mara tatu wakati ule wa Kiswahili uliwasilishwa bungeni kwa mara ya kwanza mwezi Novemba mwaka huu na ukapitishwa ukiwa umesomwa mara mbili jambo alilodai kuwa ni kinyume cha sheria.
Alisema kuwa muswada huo uliopitishwa unaendelea kuminya haki ya wananchi katika kutoa maoni kwani kimewekwa kipengele ambacho endapo mwananchi atatoa maoni ya kupinga vipengele ndani ya muswada huo basi anaweza kushtakiwa kwa kutenda kosa la jinai ambalo adhabu yake itakuwa kifungo cha miaka mitatu jela.
Stolla alisema kuwa hata muundo wa Bunge la Katiba una kasoro kwa kile alichosema kuwa kwa namna lilivyoainishwa ndani ya muswada huo umekaa kisiasa zaidi kwani idadi ya watu kutoka makundi mengine mbali ya kuwa hawajaainishwa bayana lakini ni ndogo hivyo kuna hatari Katiba hiyo ikaundwa kwa kuzingatia na kukidhi matakwa ya wanasiasa zaidi.
Alisema kuwa baada ya kosa hilo kufanyika kimbilio pekee lililobaki kuhakikisha muswada huo unarudishwa bungeni kisha kwa wananchi ili wapatiwe fursa ya kusikilizwa ni kwa Rais Kikwete kutousaini.
"Hatutanyamaza tutasema mapungufu yaliyopo kisheria, sisi kama wanasheria na wanaharakati hatutengenezi fursa zozote za kiuongozi wa kisiasa, tunasema Rais awasikilize wananchi aurudishe muswada huo bungeni, lakini akikataa tutaenda mahakamani," alisema Stolla.
Bunge: Muswada wa Katiba unaweza kubadilishwa
Kwa upande wake Bunge limesema kuwa Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya mwaka 2011 unaweza kubadilishwa au kufutwa wote endapo itaonekana kuna sababu za msingi za kisheria kufanya hivyo.
Taarifa iliyotolewa jana na Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Ushirikiano wa Kimataifa ya Bunge, imebainisha kuwa ikiwa muswada huo utasababisha mtazamo tofauti, unaweza kufanyiwa marekebisho kwa kuzingatia kanuni na taratibu kama inavyokuwa wakati mwingine wowote linapokuja suala la kurekebisha sheria za nchi.
Hata hivyo, taarifa hiyo imesema kuwa Bunge halikuvunja kanuni wala sheria yoyote ya nchi wala sababu ya msingi kuzuia muswada huo usisomwe kwa mara ya pili, kwa kuwa ulikidhi mahitaji yote kikanuni.
Taarifa imesema kuwa muswada huo ni halali na ukiwekwa saini na Rais utaendelea kusimamiwa na kutekelezwa kama sheria nyingine yoyote.
Ilisema muswada huo ni kama mwingine wowote uliowahi kupitishwa na Bunge; na ni wa kawaida ambao unaweka utaratibu wa kuwafikia wananchi, kuwasikiliza, kupata utashi wao juu ya mapendekezo ya kuandika Katiba mpya ili kila Mtanzania aweze kushirikishwa kwa wakati husika moja kwa moja.
Taarifa hiyo imebainisha kuwa Bunge limewashangaa baadhi ya wabunge waliosusia kikao cha kujadili muswada huo kwani wamewanyima fursa wananchi hao kuwakilisha maoni yao.
Ilibainisha hakukuwa na sababu za msingi kwao kulalamika wakati ikizingatiwa kwamba kambi zote ziliwasilisha na kupitisha mapendekezo ya muswada huo ili wananchi waulizwe kuhusu wanachokitaka kiingizwe katika Katiba mpya.
Iliongeza kuwa muswada huo hauhitaji ushiriki wa moja kwa moja wa wananchi isipokuwa kupitia kwa wawakilishi wao.
Taarifa hiyo ilibainisha kuwa muswada huo ulilenga katika kuweka chombo ambacho kitafanya kazi ya kuchukua maoni ya wananchi ili kuyapeleka katika Bunge la Katiba, ambalo, litakuwa na nafasi ya uwakilishi wa kila mtu.
Imesema Bunge limeuchambua muswada wa sheria na kuupitisha kuwa sheria na sio muswada wa kubadilisha Katiba kwa kuwa Katiba sasa haitobadilishwa, bali itaandikwa upya na serikalil iliyo madarakani kwa sasa na Bunge lake.
Mapema wakichangia katika mjadala huo jana, wengi wa washiriki walielezea mapungufu ya sheria katika ugawaji na umilikaji wa ardhi kwenye maeneo ya wafugaji, wawindaji na waokota matunda ambapo walitaka haki zao ziainishwe kwenye Katiba tofauti na sasa ambapo mara kwa mara wamekuwa wakiondolewa kwenye maeneo yao kuwapisha wawekezaji kwa kile wanachoambiwa wanaondolewa kwa maslahi ya umma.
Aidha walitaka Katiba mpya itambue uwepo wa Wamasai ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na kuendesha kilimo cha kujikimu, kujenga zahanati na shule badala ya kuwaachia uhuru wageni kujenga mahoteli na nyumba nyingine katika hifadhi hizo.
Katika hatua nyingine Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), limemshukia Spika wa Bunge Anne Makinda, kutokana na kupitisha Muswada wa Sheria ya Kuunda Katiba Mpya ambao ni kandamizi kwa wanawake nchini.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Mwenyekiti wa baraza hilo, Susan Lyimo, alisema Spika yuko kimaslahi ya chama tawala (CCM), badala ya wanawake.
"Tunawaomba wanawake wote watuunge mkono kwani athari za muswada ni nyingi na muathirika mkubwa atakuwa mwanamke, kitendo cha Makinda sio cha kiungwana mbele ya wanawake na umma wa Watanzania," alisema.
Alisema uamuzi wa Spika Makinda na Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani, kukataa maoni ya wanawake na hatimaye kupitisha muswada huo ni jambo la kulaaniwa.
Susan alisema suala la Katiba ni nyeti, na si mali ya CCM bali ya Watanzania wote hivyo yasiruhusiwe makundi ya watu wachache wenye malengo ya kulinda maslahi yao kuamua mustakabali wa nchi.
Alisema muswada huo ni janga kwa taifa kwani unaweka wazi kwa mtu atakayetoa elimu ya uraia kuhusu sheria hiyo atafungwa miaka mitatu.
Akifafanua juu ya upotoshwaji na propaganda zilizofanywa na CCM na CUF alisema hali hiyo inaweza kuleta machafuko ambayo athari kubwa itakuwa kwa wanawake, watoto na wananchi wenye ulemavu. Na propaganda zilizofanywa na wabunge wanawake juu ya Muswada huo ni za kupuuzwa.