beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa), wamepinga kanuni za sheria ya usafirishaji iliyoweka masharti mbalimbali ikiwamo kuwataka wamiliki kuwajibika pindi mizigo ya abiria inapopotea.
Wakizungumza wakati wa mkutano wa wamiliki hao kujadili kanuni za sheria hiyo zilizotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchikavu Tanzania (Latra) na kutoa maamuzi, walisema hawakubaliani na uwajibikaji huo kwa kuwa dhamana ya mizigo ya ndani ya basi ipo kwa abiria.
Walisema kwa kanuni hizo mpya, itakuwa ni wajibu wa mmiliki wa basi kutunza mizigo iliyolipiwa na isiyolipiwa (ya mkononi) ya abiria, jambo ambalo alisema ni gumu kwao, kwa kuwa mizigo isiyolipiwa abiria na thamani yake haijasajiliwa popote, hivyo ni ngumu kujua kiwango cha mizigo aliyonayo.
“Wewe umepanda gari kuna mizigo imewekwa kwenye buti, hivyo tuna rekodi zake kuwa ipo wapi na imelipiwa, tatizo ni wewe umepanda ndani ya gari una mizigo mingine ikiwamo vitu vya thamani kama simu halafu vikaibiwa baadaye unasema umepoteza simu ya Sh. milioni 2 kumbe ni Tecno ya Sh. 300,000,” alisema mmoja wa wasafirishaji.
Jingine wanalopinga ni gari ikiharibikia njiani mmiliki atatakiwa kuleta gari lingine ndani ya saa nane, jambo ambalo ni gumu kwa kuwa kanuni hazijaangalia uharibifu huo utakuwa umetokea wapi.
Wasafirishaji hao walisema watatumia njia mbili, mojawapo ni ya kisiasa kwa kuwasiliana na viongozi wa kisiasa na wakiona hawapati msaada watakwenda mahakamani kudai mabadiliko.
Aidha, wasafirishaji hao walisema kanuni hizo ni ngumu na zenye vikwazo vingi kwa ustawi wa kiuchumi wa wamiliki hao.
Awali, Katibu Mkuu wa chama hicho, Enea Mrutu, alisema kanuni hizo mpya zilizo katika Sheria ya Usafirishaji ya Mwaka 2019 ya Mamlaka hiyo sio rafiki na zina mazingira ya kuwakandamiza wamiliki wa mabasi.
“Kanuni mpya za usafirishaji za mwaka 2020 zilizowekwa sisi hatukushirikishwa na kwa kweli ni kandamizi na zisizo tekelezeka,” alisema Mrutu.
Alisema kwamba chini ya kanuni hizo mpya, Latra ndiyo yenye jukumu la kuidhinisha mtoa huduma ya vidhibiti mwendo katika mabasi (VTS), jambo ambalo limepingwa vikali na wamiliki hao wa mabasi kwa maelezo kuwa gharama zitakazotozwa zitakuwa kubwa kupita kiasi, hivyo kutaka uhuru katika kuamua mtoa huduma hiyo.
“Tunalazimishwa mtu atakayetufungia VTS (vidhibiti mwendo) awe ameidhinishwa na Latra, na pia sasa wanataka mtu atakayefungu mifumo ya kukata tiketi kwa njia ya mtandao amwidhinishe yeye, kitu ambacho kinafanya wasafirishaji kupata ugumu kwenye kufanya kazi,” aliongeza.
IPP MEDIA
Wakizungumza wakati wa mkutano wa wamiliki hao kujadili kanuni za sheria hiyo zilizotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchikavu Tanzania (Latra) na kutoa maamuzi, walisema hawakubaliani na uwajibikaji huo kwa kuwa dhamana ya mizigo ya ndani ya basi ipo kwa abiria.
Walisema kwa kanuni hizo mpya, itakuwa ni wajibu wa mmiliki wa basi kutunza mizigo iliyolipiwa na isiyolipiwa (ya mkononi) ya abiria, jambo ambalo alisema ni gumu kwao, kwa kuwa mizigo isiyolipiwa abiria na thamani yake haijasajiliwa popote, hivyo ni ngumu kujua kiwango cha mizigo aliyonayo.
“Wewe umepanda gari kuna mizigo imewekwa kwenye buti, hivyo tuna rekodi zake kuwa ipo wapi na imelipiwa, tatizo ni wewe umepanda ndani ya gari una mizigo mingine ikiwamo vitu vya thamani kama simu halafu vikaibiwa baadaye unasema umepoteza simu ya Sh. milioni 2 kumbe ni Tecno ya Sh. 300,000,” alisema mmoja wa wasafirishaji.
Jingine wanalopinga ni gari ikiharibikia njiani mmiliki atatakiwa kuleta gari lingine ndani ya saa nane, jambo ambalo ni gumu kwa kuwa kanuni hazijaangalia uharibifu huo utakuwa umetokea wapi.
Wasafirishaji hao walisema watatumia njia mbili, mojawapo ni ya kisiasa kwa kuwasiliana na viongozi wa kisiasa na wakiona hawapati msaada watakwenda mahakamani kudai mabadiliko.
Aidha, wasafirishaji hao walisema kanuni hizo ni ngumu na zenye vikwazo vingi kwa ustawi wa kiuchumi wa wamiliki hao.
Awali, Katibu Mkuu wa chama hicho, Enea Mrutu, alisema kanuni hizo mpya zilizo katika Sheria ya Usafirishaji ya Mwaka 2019 ya Mamlaka hiyo sio rafiki na zina mazingira ya kuwakandamiza wamiliki wa mabasi.
“Kanuni mpya za usafirishaji za mwaka 2020 zilizowekwa sisi hatukushirikishwa na kwa kweli ni kandamizi na zisizo tekelezeka,” alisema Mrutu.
Alisema kwamba chini ya kanuni hizo mpya, Latra ndiyo yenye jukumu la kuidhinisha mtoa huduma ya vidhibiti mwendo katika mabasi (VTS), jambo ambalo limepingwa vikali na wamiliki hao wa mabasi kwa maelezo kuwa gharama zitakazotozwa zitakuwa kubwa kupita kiasi, hivyo kutaka uhuru katika kuamua mtoa huduma hiyo.
“Tunalazimishwa mtu atakayetufungia VTS (vidhibiti mwendo) awe ameidhinishwa na Latra, na pia sasa wanataka mtu atakayefungu mifumo ya kukata tiketi kwa njia ya mtandao amwidhinishe yeye, kitu ambacho kinafanya wasafirishaji kupata ugumu kwenye kufanya kazi,” aliongeza.
IPP MEDIA