Chama cha Skauti Tanzania na VETA vinaweza kutekeleza majukumu ya JKT kwa ufanisi zaidi

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
36,283
43,720
Skauti ni mahali sahihi zaidi kwa vijana kujifunza uzalendo, uongozi, ushirikiano, umoja na mambo mengine muhimu ya kimaisha bila kuwapa vijana ambao ni washiriki wake hali ya ujivuni wa kijeshi kama walivyo wengi wa JKT.

Ningeshauri serikali iwekeze katika kuimarisha zaidi skauti kwa sababu ina gharama ndogo sana, iko katika sehemu kubwa ya nchi na italeta ufanisi zaidi katika kuwajengea vijana uzalendo bila kuwaweka mbali na raia.

VETA ni mahali sahihi zaidi pa kujifunza stadi za kazi kuliko sehemu nyingine yoyote kwa Tanzania hii. Huko kuna wataalamu wa ufundi wa kila aina, wa ujenzi n.k mambo ambayo yanahitajika zaidi katika jamii yetu badala ya kulima matikiti na kupasua mawe kwa nyundo na mikono.

Serikali iwekeze VETA kuwajengea vijana stadi za maisha na tofauti na JKT huko haitasumbuliwa kuwapatia ajira vijana wanaopitia huko.

Serikali inaweza kuangalia mambo gani muhimu yaliyopo katika mafunzo ya JKT yanayopungia Skauti na VETA ikayaongezea kwa maboresho zaidi.
 
Kwa sababu wengi wanaopelekewa JKT wamebaki wanalilia ajira za serikali hususani katika majeshi badala ya kurudi uraiani kutumia stadi walizopata kufanya kilimo, ujenzi, ufundi n.k

Halafu fikiria pia kwamba wanarejeshwa mtaani wakiwa na mafunzo ya kutumia silaha na mengine ya kijeshi kiasi bila uhakika wa ajira. Watu kama hawa wanapokosa kazi inaweza kuwa hatari sana kwa usalama wa raia na nchi.
Yote hayo yanakuja kwa sababu gani?
 
Kwa sababu wengi wanaopelekewa JKT wamebaki wanalilia ajira za serikali hususani katika majeshi badala ya kurudi uraiani kutumia stadi walizopata kufanya kilimo,ujenzi, ufundi n.k

Halafu fikiria pia kwamba wanarejeshwa mtaani wakiwa na mafunzo ya kutumia silaha na mengine ya kijeshi kiasi bila uhakika wa ajira. Watu kama hawa wanapokosa kazi inaweza kuwa hatari sana kwa usalama wa raia na nchi.
Kweli kabisa.
 
Skauti ni mahali sahihi zaidi kwa vijana kujifunza uzalendo, uongozi, ushirikiani, umoja na mambo mengine muhimu ya kimaisha bila kuwapa vijana ambao ni washiriki wake hali ya ujivuni wa kijeshi kama walivyo wengi wa JKT.

Ningeshauri serikali iwekeze katika kuimarisha zaidi skauti kwa sababu ina gharama ndogo sana, iko katika sehemu kubwa ya nchi na italeta ufanisi zaidi katika kuwajengea vijana uzalendo bila kuwaweka mbali na raia.

VETA ni mahali sahihi zaidi pa kujifunza stadi za kazi kuliko sehemu nyingine yoyote kwa Tanzania hii. Huko kuna wataalamu wa ufundi wa kila aina, wa ujenzi n.k mambo ambayo yanahitajika zaidi katika jamii yetu badala ya kulima matikiti na kupasua mawe kwa nyundo na mikono.

Serikali iwekeze VETA kuwajengea vijana stadi za maisha na tofauti na JKT huko haitasumbuliwa kuwapatia ajira vijana wanaopitia huko.

Serikali inaweza kuangalia mambo gani muhimu yaliyopo katika mafunzo ya JKT yanayopungia Skauti na VETA ikayaongezea kwa maboresho zaidi.

Namini hujuhi hata mana ya VATE na pia hujuhiu maana ya SCOUT bila kusahahu kuwa kuna IOGT.
 
The Scout movement, also known as Scouting or the Scouts, is a voluntary non-political educational movement for young people. Although it requires an oath of allegiance to a nation's leaders and, in some countries, to a god, it otherwise allows membership without distinction of gender, race or origin in accordance with the principles of its founder, Lord Baden-Powell. The purpose of the Scout Movement is to contribute to the development of young people in achieving their full physical, intellectual, emotional, social and spiritual potentials as individuals, as responsible citizens and as members of their local, national and international communities.
Namini hujuhi hata mana ya VATE na pia hujuhiu maana ya SCOUT bila kusahahu kuwa kuna IOGT.
 
Moja ya Kosa alilofanya Kiongozi wangu mpendwa JPM ni kuwafanya wanajeshi hasa JKT kuwa wajenzi badala ya walinzi wa mipaka na nchi swala la ujenzi haliitaji uzalendo ambao kwa Tanzania haupo kwa sasa

Veta ikiboreshwa na kuangaliwa kama taasisi ya kielimu ambayo naweza kusema inatija kuliko hata vyuo vikuu kwa maana inamfundisha mtu kujitegemea kiajira ikitokea akapata ajira sawa lakini ana uwezo wa kujiajiri tofauti na vyuo vikuu vinazalisha watumwa wategemea ajira na wamiliki wa vyeti tu
 
Moja ya Kosa alilofanya Kiongozi wangu mpendwa JPM ni kuwafanya wanajeshi hasa JKT kuwa wajenzi badala ya walinzi wa mipaka na nchi swala la ujenzi haliitaji uzalendo ambao kwa Tanzania haupo kwa sasa

Veta ikiboreshwa na kuangaliwa kama taasisi ya kielimu ambayo naweza kusema inatija kuliko hata vyuo vikuu kwa maana inamfundisha mtu kujitegemea kiajira ikitokea akapata ajira sawa lakini ana uwezo wa kujiajiri tofauti na vyuo vikuu vinazalisha watumwa wategemea ajira na wamiliki wa vyeti tu
Unaijua jkt na malengo yake
 
Skauti sijawahi kuielewa zaidi inapotezea wanafunzi muda tu !!! Wa masomo ......
 
Umepita Scout?
Scout hawana, sehemu za kuwaweka vijana mahali pamoja na kwa muda mrefu, scout , wakati wa likizo tu ndio vijana wanawekwa pamoja, na haizidi wiki 2 wakati JKT ni kuanzia miezi 3 mpaka hiyo miaka 2, na wana kambi Rasmi za kuwezesha hizo shughuli kufanyika, na sio uzalendo tu, bali pia kukuza umoja Kati ya vijana ns shughuli za uzalishaji mfo, mboga mboga, ufugaji , Veta nayo inaweza kutumika kwa kuongezea somo la utaifa
 
Kwa sababu wengi wanaopelekewa JKT wamebaki wanalilia ajira za serikali hususani katika majeshi badala ya kurudi uraiani kutumia stadi walizopata kufanya kilimo, ujenzi, ufundi n.k

Halafu fikiria pia kwamba wanarejeshwa mtaani wakiwa na mafunzo ya kutumia silaha na mengine ya kijeshi kiasi bila uhakika wa ajira. Watu kama hawa wanapokosa kazi inaweza kuwa hatari sana kwa usalama wa raia na nchi.
Kwa mfumo wa Ulinzi na usalama wa nchi hii,vijana hawa kutumika mitaani kwa uvunjifu wa amani ni ngumu. Kumbuka tangu kuasisiwa kwa JKT, tumekuwa na Askari wa akiba walio na mafunzo ya siraha mnbalimbali haikupata kutokea uasi mitaani. Kuanzia Mgambo, JKT, achilia mbali wastaafu kibao wa vyombo vya ulinzi na usalama lakini bado mfumo wa ulinzi haukuwahi kuruhusu kuwa na uwezo wa kumiliki silaha za uasi.
 

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom