Chama cha mauaji ni kipi?

Bill

JF-Expert Member
Oct 5, 2007
8,232
8,429
Kumekuwepo na matukio mengi ya mauaji ya raia wasio na hatia. Mauaji Arusha yametokea mara 3 sasa ukijumuisha na yale ya Kanisani, kisha Igunga, Mwanza, Morogoro, Iringa na Singida. Lakini hakuna majibu ya nini kilitokea.

Achilia mbali mauaji, utekaji pia umeshamiri.

Haya yote yanatendeka chini ya utawala wa CCM na pia kuinuka kwa Chadema na harakati zake.

CCM ina dola lakini imeshindwa kutoa majibu ya nani anatenda mauaji haya.

Chadema wamekuwa wakiidai CCM na dola lake kufanya uchunguzi huru lakini haitaki.

Je kati ya hawa ni nani muuaji ana hataki madhambi yake yajulikane?

Tafakari!!!!!
 
" Matebele Land Massacre"
Kule Zimbabwe kulitokea mauaji yanayo itwa " Matebele Land Massacre" Kanisa Katoliki, NGO'S, CSO na wapenda maendeleo walihmasishana zikatafutwa fedha wakawaajiri wachunguzi binafsi ambao walitoa ripoti ya nini kilichotokea na ushiriki wa serikali ya Mugabe kwenye sakata hilo.

Kama viongozi wetu wa dini wangekuwa sio partisan na serikali ya mafisadi tungewaomba washirikiane na wanaharakati wa haki za binadamu kuwaomba wadau wao wa maendeleo watafute fedha ili kuwatafuta wataalamu wa ndani na nje wakafanye uchunguzi wa mauaji mbalimbali hapa nchini. Lakini tukiendelea na huu wimbo wa Amani na Utulivu tutaisha.

Ukiona watawala wameanza kumwaga damu mpaka za watoto ujue roho wa Mungu hayupo tena hapo, na kwa vile kuna raslimali basi ni raisi sana kuungana na hawa mabeberu wanaochukua madini na raslimali zetu kuingiza vikundi vya kimafia vinavyolindwa na wenye mamlaka ili waendelee kutawala na kufaidika na rslimali zetu.

Hao wadau na wapenda haki wote wakae na watafute fedha za kuchunguza jambo hili, watawala kuwmbia waunde tume ya kijaji hawatakubali ni sawa na mtu kuamua kujikata mkono wake.

Nawasilisha
 
Tunasubiri kampeni za urais 2015 zianze ili tuCOMIT GENOIDE kwa ccm members na kuitikisa dunia, hizi ni rasharasha tu!
 
Tunasubiri kampeni za urais 2015 zianze ili tuCOMIT GENOCIDE kwa ccm members na kuitikisa dunia, hizi ni rasharasha tu!
 
chama cha mauaji ni chadema ambacho kila mara watu wanakufa kwenye mikutano na maandamano yao
 
Tunasubiri kampeni za urais 2015 zianze ili tuCOMIT GENOCIDE kwa ccm members na kuitikisa dunia, hizi ni rasharasha tu!
utakufa wewe utawaacha hao unawakusudia kuwauwa wakidumu kwa sababu mungu atakupiga kofi na kuwainua hao unaowadhamiria vibaya.,shetani ww
 
nyerere,kolimba,kombe,sokoine,na wengineo wameuwawa na chadema.tendwa anasubiri nini kuifuta?
 
nakilaani chama ambacho mauaji yanatokea kila mara kwenye mikutano na maandamano yake
 
Mkuu Chikaka Sumuni hata ikiwa taasisi za ndani zitaajiri wachunguzi binafsi haitasaidia kwani dola ni lazima iwape ushirikiano.
 
mti wenye matunda daima hushambuliwa, ww na ccm ni kizazi cha LAANA, MASABURISM inatawala vichwani, KIYAMA chenu chaja.
 
nyerere,kolimba,kombe,sokoine,na wengineo wameuwawa na chadema.tendwa anasubiri nini kuifuta?

Like. Sikioni kitufe cha like. Hivi vifo vinahitaji majibu. Nani anayo? Hakika dola inaweza kutuambia, mbona kifo cha Barlow hatukuambiwa mwenye ushahidi alete? Naamini safari hii dola inaenda kukomesha na kuja na majibu ya mauaji na kutujuza ni kipi CHAMA CHA MAUAJI
 
chama cha mauaji ni chadema ambacho kila mara watu wanakufa kwenye mikutano na maandamano yao

utakufa wewe utawaacha hao unawakusudia kuwauwa wakidumu kwa sababu mungu atakupiga kofi na kuwainua hao unaowadhamiria vibaya.,shetani ww

nakilaani chama ambacho mauaji yanatokea kila mara kwenye mikutano na maandamano yake

huna hoja wewe kaa chini..lwakatare anakusalimia

Paw, Invisible, uhuru mnaotoa kwa watu wasio na lengo la kujadili bali kuvuruga umefanya watu waliokuwa na mchango chanya kama akina Mkandara, Mchambuzi, n.k. kukimbia jukwaa hili. Kwa kuwa mmeachia watu wasio na nia ya kujadili bali kukejeli na kuvuruga watawale majukwaa yetu. Huyo hapo juu ni mfano wa watu hao. They are a liability to JF.

JF inabidi tufanye upya tathmini ya mwenendo wetu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom