Chama Cha Malaya?

Status
Not open for further replies.

Asha Abdala

JF-Expert Member
Mar 21, 2007
1,130
44
Moderator, usichanganye thread hii na ile nyingine ya Burudani ya Richard- hii ni SIASA kabisa.

WanaCCM wenye maadili naowaombeni radhi, msinilaumu- kosa ni letu kukubali kuongozwa na Malaya.

Spana ikifungua kokote huitwa Spana Malaya, Mwanamke au Mwanaume akifanya ngono ovyo ovyo huitwa Malaya, CCM kwa kuwa na viongozi wanaopenda kudandia matukio kujipatia umaarufu wa kisiasa ni vyema kikaitwa Chama Cha Malaya(CCM).

Hivi Chiligati Waziri wa Vijana na Katibu wa Uenezi CCM anataka tuamini kwamba ushindi wa CCM ni sera ya malezi ya Vijana ya Chama Cha Malaya(CCM)?

Na huu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Malaya(UVCCM) nao umesahau kabisa misingi ya TANU Youth League(TYL)? Nakumbuka enzi zetu umalaya uliadhibiwa kwa bakora leo unaenziwa kama ushujaa!

Hebu msome hapa:

“Kati ya waliokuwa wa kwanza kumtumia salamu za pongezi ni CCM, ambacho Katibu wake wa NEC (Itikadi na Uenezi), Kapteni Mstaafu John Chiligati alimpongeza Richard kwa ushindi huo.
"Chama Cha Mapinduzi kinauona ushindi huo kuwa ni ushindi wa Watanzania wote. hali hii inatokana na malezi mazuri wanayopewa vijana wa Tanzania hasa kwa kuzingatia sera nzuri za Chama Cha Mapinduzi kuhusu vijana," inasema taarifa yake kwa vyombo vya habari.
Umoja wa Vijana wa CCM pia umeandaa mapokezi makubwa ya shujaa huyo wa BBA ll.


Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=2886

Chiligati, unakubali Makamba akufanye nawe uonekane Malaya?

Dada Asha
 
Dada Asha naona una hasira sana pole,

Lakini hii jana watu tuliisemea habari ya kumparamia Richard ushindi wa BBA na kuufanya kete ya kisiasa!! ama eti mafanikio ya JK na chama tawala huu ni upuuzi perse!
 
Dada Asha naona una hasira sana pole,

Lakini hii jana watu tuliisemea habari ya kumparamia Richard ushindi wa BBA na kuufanya kete ya kisiasa!! ama eti mafanikio ya JK na chama tawala huu ni upuuzi perse!

In fact nilishunganisha kipande hicho na ile topik ya richard kule kwen burudani, kwa sababu watu walishapredict kuwa litatokea

Pole dada Asha naona umekasirika kweli leo!
 
Duh! Hawa CCM watadandia chochote chenye umaarufu ili waonekane na wao wanahusika kwa namna moja au nyingine! wakati wamejaa kashfa chungu nzima dhidi ya viongozi wao mbali mbali. Inawezekana kabisa huyo Richard hajawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa Tanzania, au labda ni mwanachama wa chama kingine tofauti. Kweli CCM imefilisika kabisa kimawazo! maana huku sasa ni kutapatapa ili kutafuta umaaufu wasiokuwa nao.
 
Pambaf...kuna siku atapatikana Mr Gay-Africa, kutoka Tanzania. Bunge letu litapenda kumuona bungeni apewe hongera zake kwa kutwaa taji hilo.
 
Jamani mbona pongezi za namna hiyo zinazohusisha ushindi wa Richard na Itikadi nzuri ya CCM zilitolewa na mzee ES jana?
 
Kuna usemi/utani usemao``ukitaka kumjua Mchaga dondosha shilling`` hata makaburi ya wachaga yanajua fedha.

Ukitaka kujua mafisadi kina nani shinda hela nyingi kama Richie
 
Sasa kumbe kama hawana cha kujivunia wafanye nini zaidi ya kudandia kila kinachojitokeza? Na umalaya ndio jina pekee linalowfaa, maana malaya hachagui mwanamke/mwanamume, yeyote anayejitokeza ni halali yake. Ndio wamefika hapo.
 
kwa namna serikali ya jk ilivyokosa mafanikio ya kuringia[kwenye sekta ya barabara et al]sintashangaa wakidandia jambo lolote ambalo angalao litawapa umaarufu kwa siku moja..SINTAKUWA KATI YA WATAKAOSHANGAA KUWAONA WAFURUKUTWA WA CCM HIYO KESHOKUTWA NA MAGWANDA YAO NA BENDERA UWANJA WA NDEGE KUMLAKI RICH....JAMANI SIMBORESHE HAYO MAISHA TUWASIFU!!!!!????
 
Huenda nayo ni sera ya CCM chini ya UVCCM kufundisha vijana kufanya mavituz. kwani hujui wamebobea kwenye hilo somo? rejea kashfa ya ngono ya JK.

Sasa Chiligati hajakosea, anatimiza wajibu wake kama kungwi wa vijana.
 
ccm itasimama imara achilia mbali na matusi wanayomwagiwa, ccm itatenda haki na kamwe haitosubiri shukrani zenu !
so wewe uliyeanzisha hii mada, endelea hivyo hivyo !
 
Bibi Asha,

Heshima mbele, kwenye hii forum ya kimataifa kuna watoto wa shule za msingi pia wanaosoma hii forum, huwezi kuchambua siasa na hasira za namna hiyo bro, siasa ni mchezo mchafu tu, na sio mchezo wa matusi,

CCM ni chama kinachotawala Tanzania kwa ridhaa ya wananchi, ambao hata majuzi tu pamoja na uchafu wote ulitolewa against CCM lakini bado wananchi wakaichagua CCM anyway, na kuwakataa wapinzani, sasa huwezi kuwaita wananchi wa Tanzania na hata wazazi wetu walioichagua CCM ni malaya, maana huwezi kuchagua chama cha malaya kama na wewe sio malaya,

Wakuu tunajua kuwa mnaimiliki hiii forum, na mnaweza kufanya mnalotaka, if that is the case basi muwe mnawaacha kina Brazameni, lakini kuruhusu vicha vya topic ambavyo ni low kama hiki cha hii topic, ni kutushusha heshima wote tunaoshiriki humu, CCM wametoa hoja ambayo huipendi basi jibu hoja, usilete viroja,

Marais wote wa East Africa and Central, betweeen jana na leo wamemtumia Rais Kikwete, salaam za hongera za ushindi wa m-Tanzania Richie, ndivyo siasa zilivyo mkuu, sasa huwezi kuwaita hao marais ni CCM, au ni malaya, ukitukanwa na mtu hapa I can understand kuwa unajibu, lakini kukiita chama kinachotawala kinachokubalika na wananchi wengi, kwa majina ya matusi inakuwa ni aibu ya wana-forum wote tunaoshiriki hapa!

Ningemuomba Admin, akifute au akirekebishe hiki kichwa cha topic hiii, na aondoe hilo neno malaya maana ni too low kwa forum kubwa kama hiii!

Ahsanteni!
 
Mwasisi wa CCM, Baba wa Taifa alishawahi kuikosoa CCM mara nyingi tu kwa sababu alishaona kuna kasoro nyingi ndani ya CCM. Inakuwa vizuri CCM na wana CCM wakawa tayari kukosolewa kwa manufaa ya chama hicho na Tanzania, kwani hali ndani ya CCM si shwari hata kidogo. Mwalimu alisema, "CCM si mama yangu" hivyo kwa wana CCM itakuwa vizuri mkiwa mstari wa mbele kukemea uozo ulio ndani ya chama hicho vinginevyo kutakuwa na matatizo makubwa ndani ya CCM na Tanzania maana CCM ndio chama tawala, au utamaduni wa kukosoana ndani ya CCM umeshawekwa kapuni na Mtandao?
 
Ushwari wa ndani ya CCM, unakuwaje ishu ya taifa? Hivi CCM inatakiwa kuwa na ushwari upi huo baada ya kumaliza uchaguzi juzi bila matatizo, hivi ushwari unatakiwa uwe wa aina gani zaidi ya wananchi kuweza kukutana chini ya chama chao na kufanya uchaguzi mzito wa kujiongoza as mujibu wa sheria ya nchi yetu?
 
Waswahili walisema mficha ugonjwa kifo kitamuumbua. Ushwari wa CCM siku zote utakuwa ni issue ya Taifa kwa sababu CCM ndio chama kilicho madarakani. Mambo yakiwa shakalabaghala ndani ya CCM hivyo hivyo ndio yatakavyokuwa ndani ya serikali. CCM kama iko shwari kusingekuwa na haja wakongwe wa chama hicho akina Mwinyi, Malecela, Butiku na sasa Mwakawago kuongea yale ambayo viongozi wa juu ndani ya CCM hawataki kuyasikia. Au sauti za wakongwe hawa ambao bado ni wanachama hai wa CCM zimeshadharauliwa na viongozi wa juu wa CCM!?

Uchaguzi umekwisha, lakini haukuwa wa kidemokrasia. Tulisikia toka kwenye vyanzo vya habari mbali mbali hata makada wa CCM kwamba kungekuwa na wagombea mbali mbali katika nafasi ya makamu wa mwenyekiti. Wanachama wengi wa CCM hata wasio wanachama walijua fika kwamba nafasi hiyo ingepatikana kwa wajumbe kuwapigia kura wagombea mbali mbali na hatimaye kumpata mmoja ambaye ndiye angeshika nafasi hiyo.

Kumalizika kwa uchaguzi ndani ya CCM kamwe hakuashirii kwamba hali ndani ya chama hicho ni shwari, bado kuna wanamtandao na kundi lao na wale wasio wana mtandao na kundi lao. Nasikia hili la makundi linampa wakati mgumu jamaa kufanya mabadiliko ya mawaziri maana ukishakuwa na makundi basi kufanya maamuzi ya muhimu kwa ajili ya Taifa siku zote yanakuwa magumu mno, amwache nani amweke nani? Na anajua fika kama si wana matandao basi asingekuwa hapo alipo leo hii. Wakati mwingine tuwe wakweli hata inapobidi kuvikosoa vyama vyetu.

Nafurahi sana pale ninaposikia wana CCM ambao ni wakweli wa nafsi zao ambao wanasema wazi kabisa hawako tayari kukihama chama hicho wakati huo huo hawako tayari kuwapigia kura wagombea wa CCM kwa kuwa hawaridhiki na mwenendo ndani ya chama hicho. Wengi wanadhani labda CCM ikiteleza kwenye uchaguzi, basi labda mabadiliko ya kweli yanaweza kutokea ndani ya chama hicho ili kuinusuru CCM na Tanzania pia.

CCM mambo si shwari na kuendelea kuyaficha maovu yaliyo katika chama hicho ni kuipeleka CCM na Tanzania pabaya.

http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/11/11/habari1.php
 
ccm itasimama imara achilia mbali na matusi wanayomwagiwa, ccm itatenda haki na kamwe haitosubiri shukrani zenu !
so wewe uliyeanzisha hii mada, endelea hivyo hivyo !

Yes Kada siku zote tumekuwa kupo pamoja katika hoja lakini kwa hili sikubaliani nawe. Siku CCM wakichemsha tuseme wamechemsha mkuu siku wakifanya vizuri tuseme wamefanya vizuri. Sawa mkuu? najua CCM bado ni chama imara na ndio maana akina mwanakijiji wameamua kutangaza rasimi kujiunga nacho. Ila kumbuka kama CCM itaendelea kuchemsha ipo siku itaanguka tuu mkuu. Utawala wa roma ulianguka na sidhani kwanini a CCM wasianguke.

Hivi hiyo kesho kutwa ukienda Airport kumpokea Rich na magwanda yako ya kijani au unaangalia TV na vijana wako wankuuliza "Baba huyo watu wenye nguo za kijani wamembeba amefanya ushujaa gani kwa taifa"? Mkuu bila shaka hutawaambia alikuwa maarufu wa kufanya ngono na kuonyesha kadudu kake hadharani. Au kijana wako akikuambia baba kwanini na sisi Huku nyumbani kwetu tusianzishe BBA au BBHouse ili tuwe na uzoefu kama Richie kwani ni role model kwa vijana sijui utakuwa je.
 
Pole sana dada Asha, ndiyo watanzania tulivyo tunaanza ku-adopt mambo ya magharibi kwa speed ya aina yake sijui ndiyo sababu ya hii karne ya science and tekelinalokujia!!!!????
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom