Chama cha Madaktari Tz chawasilisha maombi UN ya ulinzi kwa viongozi wake

kuna mijitu ilikuwa inabisha juuya dr ulimboka kumtaja msangi ...sasa barua hii nayo imesema ni kwelim msangi alitajwa kuhusika.....

Kama kuna fedheha kubwa katika serikali hii hakuna inayoizidi hii ya wananchi kuomba ulinzi wa UN baada ya vyombo vya usalama kutishia usalama wao. Hivi wanastahili kweli kuwepo na uendeshaji wake kutegemea kodi zetu? What a shame!
 
Kama kuna fedheha kubwa katika serikali hii hakuna inayoizidi hii ya wananchi kuomba ulinzi wa UN baada ya vyombo vya usalama kutishia usalama wao. Hivi wanastahili kweli kuwepo na uendeshaji wake kutegemea kodi zetu? What a shame!

Kwani lengo ni kuiletea serikali fedheha?
 
Go back to ur constitutional copy if u have any
The gov is responsible for providing health services to her citizen and not otherwise...
Doctors are just employees as any other employees ....
Try to think big and do some analysis before you post in here.....

This is sad! Mate tell you what? I trully respect your right to hold forth your view - eh, please respect the right of others, "dismal analytical MIND" notwithstanding!

May I remind you politely that you can fool 'em MARINES butnot a level headed TANZANIANS - Cheers.
 
OH! God, tunaomba utukomboe tunakokwenda siko! Tusiombe tufike wanakotaka kutupeleka yaani watanzania ninao wafahamu ndo wamefikia hapa kweli tumekwisha. Ila hakuna linalomshinda Mungu nikusali kila wakati maana sasa shetani ameingia nchini. God come come!
HII NCHI HAITAKI HATA USHAURI WA VIONGOZI WA DINI, LAKINI KWENYE KUAPISHANA, WALIITWA. Ama kweli tumefika pabaya!
 
2719468_orig.png

647529_orig.png

Tuna matatizo ya kiuongozi na kiutaalam katika taasisi nyingi, za kisiasa na kiraia. Barua ya MAT inaanza kwa kusema kinachowasibu ni kwamba wanahofia hatari za kiusalama na vitisho kwa Dr. Ulimboka.

Well, Dr. Ulimboka hajatishwa, amesulubiwa nusu ya kufa, utasemaje suala hapa ni vitisho? Sijui tatizo ni lugha za kigeni?

Barua inalalamika kwamba akiwa polisi Dr.Ulimboka hakupewa msaada wa kitabibu. Watu wa UN lazima wawashangae sana, mmemuokota mtu kwenye mitaro vichakani, yuko taabani hana meno anachuruzika midamu, mnampeleka polisi! Polisi wafanyeje, wamhoji kuchukua statement au wampe muarobaini apone?

MAT wanasema Dr. Ulimboka alitekwa mbele ya Ofisa wa Ofisi ya Rais. Nani? Wanafyata kumtaja!
 
Tuna matatizo ya kiuongozi na kiutaalam katika taasisi nyingi, za kisiasa na kiraia. Barua ya MAT inaanza kwa kusema kinachowasibu ni kwamba wanahofia hatari za kiusalama na vitisho kwa Dr. Ulimboka.

Well, Dr. Ulimboka hajatishwa, amesulubiwa nusu ya kufa, utasemaje suala hapa ni vitisho? Sijui tatizo ni lugha za kigeni?

Barua inalalamika kwamba akiwa polisi Dr.Ulimboka hakupewa msaada wa kitabibu. Watu wa UN lazima wawashangae sana, mmemuokota mtu kwenye mitaro vichakani, yuko taabani hana meno anachuruzika midamu, mnampeleka polisi! Polisi wafanyeje, wamhoji kuchukua statement au wampe muarobaini apone?

MAT wanasema Dr. Ulimboka alitekwa mbele ya Ofisa wa Ofisi ya Rais. Nani? Wanafyata kumtaja!
Kwa mtazamo wangu nadhani hapo in pekundu ni sahihi:
Dhumuni ya barua hii sio kuripoti kilicho tokea
bali ni kuonesha, kutakana na yale yalio jiri
kua bado kuna SECURITY THREAT inayo endelea
Wamehadithia walio pita ili tu kufafanua mazingira
ila wanahofia kua walioanza kazi hawakumaliza
talking about the threat in introduction is appropriate
 
Mnaopinga mgomo mna haki ya kuvaa gloves na kwenda kuwasaidia wagonjwa.
Hakuna ulazima wa watu wasiotaka kazi kulazimishwa. Nani aliwazuia nyie nanyi msisomee udaktari?
After all wananchi hawana mikataba na madaktari wala madaktari hawana mikataba na wananchi bali serikali.
Nao wananchi wana mkataba wa kupata matibabu toka kwa serikali na si madaktari.
hivyo kama wananchi wanahitaji matibabu wana haki ya kukamatana na serikali yao! Fungukeni muwe na akili

wakiacha kazi ndo tutawaelewa!
 
Kwa hiyo our government is a liar? Je wananchi nao hawana akili na ni dhaifu!!! Ni kitu gani kinaweza kuleta ile amani na furaha na upendo wakati wa awamu ya kwanza ya urais wa Tanzania!!! Aliyempinga marehemu baba wa taifa nitamlaumu sana!!! Alifanya mazuri kwa kiasi chake na tunategemea mazuri zaidi maana kwa sasa tunawapa madini wawekezaji, na gas, na sasa uranium na mafuta!!!!! Looooo this .................so sad!![/QU NI KWELI WANANCHI WAWEZA KUWA DHAIFU KWA KUKOSA pesa za kwenda private na nje ya nchi kujitibia kama hao serikali na madactari na kubaki kuumizwa na migogoro ya hao mafahari wawili. Ukiangalia muhimbili wagonjwa maskini wanagomewa lakini wagonjwa fast truck wanahudumiwa. Ina maana fast truck kuna vifaa vya kutendea kazi na mashine sio mbovu wakati hospitali ni moja? Madoctor siasa, serikali siasa plus dhaifu. Wananchi umaskini unawaua bila hatia. Wacha maskini wafe, wabaki taifa la matajiri wenye uwezo wa kujitibu private. Ila damu ya raia wasio na hatia atawatafuna.
 
Mpaka sasa tumeshapewa uongo wa kutoosha kuhusu hili sakata la Dr Ulimboka. KWakuwa nina hasira kali, naomba nisiongee sana.

Ninachowaomba ni nyie kama watu makini msome barua ya Chama cha madaktari halafu mniambie kivipi serikali ipo innocent katika umafia huu. Gazeti la Jamhuri lililotafuta kumuosha ACP Msangi kutoka kwenye unyama huu lina hoja za kujibu pia.

Nasema hivi, aishie kwa upanga atakufa kwa upanga. Yeyote aliyeshiriki moja kwa moja, yeyote aliyewatuma wauaji akina ACP Msangi na yeyote aliyefaidika na unyama ule MUNGU WANGU ALIYE HAI ATAMLIPIA ZAIDI.

Maana Biblia yangu inasema "kipimo kilekile mpimacho ndicho mtakachopiwa" tena cha kwenu kitakuwa "kimejaa na kushindiliwa hata kumwagika". Your days, CCM are numbered. You got to see the writings on the wall.
 

Attachments

  • TUNAPOKWENDA KUBAYA.pdf
    935.7 KB · Views: 805
ACP msangi auawe km kibaka! Siku za ukombozi zaja na zahesabika Pinda mzee wa liwalo na liwe
 
Aise inasikitisha, inauma, inatia hasira ya kuua mtu. Huyo ACP Msangi anacheleweshwa nini naye kuuawa?
 
BAADA ya kutekwa, kupigwa na kutelekezwa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, viongozi wa vyama vya madaktari wamedai maisha yao yako hatari hali iliyowalazimu kuomba ulinzi Umoja wa Mataifa na makundi mbalimbali ya kutetea haki za binadamu.

Madaktari hao wamesema hawana imani na maofisa wa serikali ya Rais Jakaya Kikwete, wanaotishia usalama wa maisha yao kwa namna tofauti hasa baada ya tukio la Dk. Ulimboka la Juni 27 mwaka huu.

Barua ya madaktari hao kwenda kwa Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa hapa nchini ya Julai 7, 2012, madaktari wameeleza namna maofisa wa serikali wanavyotishia usalama wa maisha yao hao na kuwaeleza namna walivyowatuma wenzao Afrika Kusini kuhakikisha Dk. Ulimboka anapoteza maisha.

Pia barua hiyo yenye kumb. Na.MAT/UN/SU/01, imetumwa kwa Mwenyekiti wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi, Shirika la Human Rights Watch na Amnesty International.

Taasisi nyingine zilizopelekewa nakala ya barua hiyo ambayo Tanzania Daima ina nakala yake ni Kituo cha Haki za Binaadam (LHRC), SIKIKA Tanzania, Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA).

“Hata hivyo, watu kutoka serikalini waliihakikishia MAT kwamba timu ya wasaidizi wao imeenda Afrika Kusini kuhakikisha Dk. Ulimboka anarudi nyumbani akiwa maiti.

“Kwa kuongezea hapo, viongozi wa MAT tunapokea vitisho kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi kwenye simu na wakati mwingine tunapigiwa simu na namba zisizopatikana tukitishiwa maisha,” ilieleza sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na Dk. Mkopi.

Aidha, barua hiyo imeuomba Umoja wa Mataifa kuwahakikishia madaktari usalama wa Dk. Ulimboka kwenye hospitali anayotibiwa na kuwalinda madaktari wengine hasa viongozi wa vyama na jumuiya ya madaktari.

Kadhalika barua hiyo imeuomba umoja huo kuushauri mfumo wa sheria za Tanzania kutokubali kutumika kwa faida za kisiasa na kulitaka Bunge kubaki na majukumu yake ya Kikatiba ya kuiwajibisha serikali kwa vifo vya watu kama matokeo ya mgomo unaoendelea.

Katika barua hiyo madaktari hao wameeleza namna Dk. Ulimboka alivyoteswa na watekaji hao kwa kung’olewa kucha, meno na kuumizwa sehemu mbalimbali za mwili wake huku akimtambua ACP Msangi kuwa miongoni mwa watekaji hao.

Walieleza namna polisi wa kituo cha Bunju walivyoshindwa kuwapa ushirikiano kwa haraka ili kumuwahisha majeruhi huyo kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili na jinsi walivyokuwa wakizuiwa na magari ya askari kwa lengo la kumchelewesha asipate huduma za kitabibu.

“Akiwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI), Dk. Ulimboka licha ya maumivu makali aliyokuwa nayo alimtambua ACP Msangi kuwa ni miongoni mwa waliomteka na kumtesa,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo na kubainisha kwamba ACP Msangi ni kiongozi wa tume iliyoundwa kuchunguza suala hilo.

Ikulu yasononesha viongozi wa dini

Baadhi ya viongozi wa dini waliojitolea kusuluhisha mgogoro baina ya madaktari na serikali, wameeleza kusononeshwa na jibu la Ikulu la kukataa kuonana nao huku wakibainisha kwamba jukumu lao kubwa ni kuhakikisha amani inatawala.

Akizungumza kwa niaba ya viongozi hao, Msemaji wa Kamati ya Vijana wa Baraza Kuu la Waislamu (Bakwata), Said Mwaipopo, alisema licha ya jibu hilo wanaendeleza juhudi za kuhakikisha mgogoro huo unamalizika kwa njia za amani.

“Hatukatishwi tamaa na jibu la Ikulu kazi yetu kubwa ni kuhakikisha amani inakuwepo… ndiyo maana jana tulikutana na viongozi wa madaktari tukawaeleza kwamba njia bora ya kufanya ni kuandika barua na kuieleza jamii kupitia vyombo vya habari kwamba wanaomba msamaha kwa Rais, wananchi na serikali.

“Kitu kinachotusikitisha vijana wale walikataa ushauri wetu tukagundua kwamba inawezekana nyuma yao kuna siasa zinaingia,” alisema Mwaipopo.

Akijibu suala hilo Katibu wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Edwin Chitage, alikiri kukutana na viongozi hao jana na kueleza kwamba walichokubaliana ni kusubiri barua rasmi kutoka Ikulu ikiwataka madaktari hao kuandika barua kuomba msamaha kwa Rais, Watanzania na serikali.

“Ni kweli lakini alichokisema Mwaipopo ni kwamba alipigiwa simu na watu waliodai kwamba wako Ikulu, hivyo wakawaambia viongozi hao wa dini watuambie madaktari tuandike barua ya kuomba msamaha.Tunaomba msamaha kwa nini,” alihoji.

Dk. Mkopi aliongeza kuwa madai yao hayajatekelezwa licha ya kuwepo kwa muda mrefu tangu mwaka 2005 na kwamba kama serikali haina dhamira ya kweli ya kumaliza mgogoro huo utaendelea hata baada ya miaka 10.

Kukutana na Dk. Mwinyi

Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Dk. Godbless Chale alisema walipokea simu kutoka kwa Waziri mpya ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi ikiwataka kwenda kumweleza sababu za mgomo wao.

“Kweli Dk. Mwinyi alitupigia simu akatuita alisema hajui madai yetu hivyo twende tukamweleze hivi kwa akili ya kawaida kweli ofisi inakosa nyaraka za kumbukumbu?!! Tunaona hayupo ‘serious’.

“Kabla hajatuita wizara yake iliteua wajumbe watatu Naibu Katibu Mkuu, Naibu Mganga Mkuu Dk. Donald Mbando na Mkurugenzi wa Rasilimali tukaketi nao kuwaeleza siku chache baadaye waziri anasema hajui madai yetu hii tumeona ni ‘kamchezo’ wanataka kutufanyia,” alisema Dk. Godbless.

Concern
Sasa leo serikali inawajibu hivyo viongozi wa Dini, ngoja kesho mtajutia maamuzi yenu ya kihuni
 
Yalimshinda ya mbagala ataweza ya madaktari kweli, ona kauli yake:

"Kweli Dk. Mwinyi alitupigia simu akatuita alisema hajui madai yetu hivyo twende tukamweleze hivi kwa akili ya kawaida kweli ofisi inakosa nyaraka za kumbukumbu?!! Tunaona hayupo ‘serious'.
 
"Mungu akiwa upande wetu ni nani aliye juu yetu?HAKUNA!!!!!!"Itadhihirika yupo Mungu
Tanzania na wala hii nchi si mali yao mafisadi na wauaji"
 
Back
Top Bottom