Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 2,204
- 4,695
Chama tawala cha Jubilee nchini Kenya kimependekeza kuondolewa kwa naibu wa rais Willima Ruto kutoka kwa wadhfa wake kama naibu kiongozi wa chama hicho.
Katibu mkuu wa chama hicho Raphael Tuju amemshutumu bwana Ruto kwa kuwa 'mjeuri, mwenye madharau na asiyemheshimu Rais Uhuru Kenyatta".
Je, Katibu Mkuu wa Jubilee amesema nini?
Taarifa iliosomwa hii leo imezungumzia kuhusu matusi ya hivi karibuni yaliotolewa na wandani wa naibu huyo wa rais yakimlenga mamake Uhuru{ seneta mmoja tayari ameshtakia kwa kutoa matamshi ya chuki} walipokuwa wakimuunga mgombea wao katika uchaguzi wa marudio ambapo chama hicho kilikuwa kimeamua kutowakilishwa mbali na kutokuwepo kwa naibu huyo wa rais katika mkutano wa Jumatatu kuhusu corona wakati abapo rais alilegeza baadhi ya masharti ya kukabiliana na ugonja huo.
Kiti chake kilikuwa kimehifadhiwa katika mkutano huo. Taarifa hiyo inajiri siku moja baada ya naibu huyo wa rais kutembelea makao makuu ya chama hicho na zaidi ya wabunge 35 wanaounga mkono ugombea wake wa urais.
Chama hicho kimeshtumu kwa kujaribu kfanya mapinduzi huku rais akiwa Ufaransa. Hapo Jana bwana Ruto alijibu katika mtandao wake wa Twitter kwamba ameshangaa kwamba ziara yake ya makao makuu ya chama hicho cha Jubilee ilikuwa habari kuu.
Uongozi wa chama hicho hivi sasa umesema kwamba hautamruhusu kuingia katika makao hayo, ukisema kwamba hautamruhusu kuendesha kampeni zake za urais kutoka katika afisi hiyo ili kuwatishia wapinzani wake.
View attachment 1588617View attachment 1588618View attachment 1588619View attachment 1588620
Katibu mkuu wa chama hicho Raphael Tuju amemshutumu bwana Ruto kwa kuwa 'mjeuri, mwenye madharau na asiyemheshimu Rais Uhuru Kenyatta".
Je, Katibu Mkuu wa Jubilee amesema nini?
Taarifa iliosomwa hii leo imezungumzia kuhusu matusi ya hivi karibuni yaliotolewa na wandani wa naibu huyo wa rais yakimlenga mamake Uhuru{ seneta mmoja tayari ameshtakia kwa kutoa matamshi ya chuki} walipokuwa wakimuunga mgombea wao katika uchaguzi wa marudio ambapo chama hicho kilikuwa kimeamua kutowakilishwa mbali na kutokuwepo kwa naibu huyo wa rais katika mkutano wa Jumatatu kuhusu corona wakati abapo rais alilegeza baadhi ya masharti ya kukabiliana na ugonja huo.
Kiti chake kilikuwa kimehifadhiwa katika mkutano huo. Taarifa hiyo inajiri siku moja baada ya naibu huyo wa rais kutembelea makao makuu ya chama hicho na zaidi ya wabunge 35 wanaounga mkono ugombea wake wa urais.
Chama hicho kimeshtumu kwa kujaribu kfanya mapinduzi huku rais akiwa Ufaransa. Hapo Jana bwana Ruto alijibu katika mtandao wake wa Twitter kwamba ameshangaa kwamba ziara yake ya makao makuu ya chama hicho cha Jubilee ilikuwa habari kuu.
Uongozi wa chama hicho hivi sasa umesema kwamba hautamruhusu kuingia katika makao hayo, ukisema kwamba hautamruhusu kuendesha kampeni zake za urais kutoka katika afisi hiyo ili kuwatishia wapinzani wake.
View attachment 1588617View attachment 1588618View attachment 1588619View attachment 1588620