Chama cha ACT - Wazalendo chajiondoa kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Tumejitahidi kufuata njia zote za kisheria Lakini CCM na Serikali yake wameamua vinginevyo kwa kutuondoa katika Uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji. Tumeamua kutafuta njia nyingine za kulinda demokrasia yetu. TUSILAUMIANE.

Mwisho; Kumekuwepo na vitendo viovu vinavyofanywa na Jeshi la Polisi na watendaji wa Serikali kuwabughudhi Wagombea wetu, wanachama na viongozi wetu maeneo mbalimbali nchini. Serikali ya Rais Magufuli isitufikishe kuvuka mstari wa Uvumilivu.
Ni bahati mbaya sana kwamba lugha hii ndio inaanza kuwa kawaida yetu, na muda si muda, itazoeleka.

Serikali wao wanaamini kwa kuwa wana vyenzo zote, hawawezi kujisumbua kwa kuzitafakari kauli kama hizi. Wanachojua wao ni kwamba 'hawajaribiwi', hakuna mwenye uthubutu/ujasiri wa kuhoji utashi wao. Waziri Lugola shasikika akitamka hata kabla ya kusikia maneno kama haya toka kwa vyama vya upinzani. Maana yake ni kwamba wapo tayari kupambana.

Binaadam sio ng'ombe au mfugo unaoweza kuamua lolote juu yake. Hawa viongozi serikalini ni mhimu watambue hilo na waheshimu haki za wananchi waliowaweka madarakani.

Wananchi hawa ndio waliotumia haki yao kuwaweka madarakani; sasa wanatumia nafasi hiyo kuwanyima haki hiyo hiyo kuwaondoa madarakani? Wataweza kweli?
 
Kufuatia hujuma za kila aina zilizofanywa na serikali ya ccm dhidi ya vyama vya upinzani kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa, chama cha Chadema kiliamua kujitoa na kutoshiriki uchaguzi huo haramu ili kutouhalalisha uonekane ni uchaguzi halali. Wiki hii niliandika nyuzi tatu 1.Chadema wamekwepa mtego wa kuwa wasaliti wa watanzania. Je Zitto Kabwe na Act yake wataukwepa huu mtego Au ndio tutaijua rangi halisi ya Zitto. 2.Vyama vya upinzani vitakavyoshiriki uchaguzi wa serikali za mitaa ni wasaliti wa watanzania. 3.Wapinzani watakaoshiriki uchaguzi wa serikali za mitaa ni wasaliti wa watanzania. Napenda kuchukua fursa hii kumpongeza Zitto Kabwe na Act Wazalendo yake kwa uamuzi mgumu na busara waliouchukua . Laiti Zitto Kabwe na Act Wazalendo yake wangeshiriki watanzania tusingewaelewa, yaani kwa figisu zote hizo, hila, hujuma unashiriki uchaguzi huu ili upate nini? Maana mpaka matokeo yameshapangwa. Mungu akubaliki sana Zitto na viongozi wenzako ili tupambane pamoja kuikomboa hii nchi toka mikononi mwa Bahima empire.Naomba huu uzi usiunganishwe.
 
Kususa nako kuna kanuni zake, wewe ukisusa, wenzio twala.
.
P
 
Hayo yametangazwa na kiongozi wa chama hicho Mh Zitto Kabwe.

ACT WAZALENDO CHAIFUATA CHADEMA, CHAJITOA KUSHIRIKI UCHAGUZI. Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ametangaza kuwa chama hicho kimejitoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 24, 2019 kwa sababu kuwa wagombea wa chama hicho wengi wameenguliwa.
View attachment 1257821
ACT-WAZALENDO IMEJIONDOA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA:

MILANGO YA DEMOKRASIA IMEFUNGWA: TUSILAUMIANE

MSIMAMO WA ACT WAZALENDO KUHUSU UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, VIJIJI NA VITONGOJI WA NOVEMBA 24, 2019:

Chama cha ACT Wazalendo, kikiwa Chama cha siasa makini chenye usajili wa kudumu nchini, kiliitikia wito wa kushiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji uliokuwa ufanyike tarehe 24 Novemba 2019, tukiamini kuwa ni nafasi nyeti ya kuimarisha ushindani wa kisiasa nchini.

Licha ya miaka minne ya changamoto kubwa, na licha ya wananchi wengi kutuonya mapema kuwa hapatakuwa na Uchaguzi wa Haki, bado tuliamua kushiriki kikamilifu tukiamini kuwa taratibu, sheria na Katiba ya nchi itaheshimiwa na wahusika wote wa mchakato huu.

Wanachama wetu 173,593 walijitokeza kugombea nafasi mbalimbali za Uongozi kwa kujaza fomu za uteuzi na kuzirejesha na wengine wengi kwa maelfu walikataliwa kupewa fomu na au ofisi kufungwa kwa wakati wote. Wagombea Uenyekiti wa Mitaa walikuwa 2,481 kati ya Mitaa yote 4,264 nchini, Uenyekiti wa Vijiji walikuwa 8,218 katika ya Vijiji vyote 12,316 nchini, na uenyekiti wa Vitongoji walikuwa 35,457 kati ya Vitongoji vyote 64,384 nchini. Kwa upande wa Wagombea wa nafasi za Ujumbe wa Halmashauri za Vijiji na Kamati za Mtaa (wajumbe wa kawaida na wajumbe Wanawake) wanaACT 135,675 walijitokeza kuomba nafasi hizo.

Takribani, wananchi 173,593. Hata hivyo, kati ya wagombea wetu hao 173,593 waliochukua na kurejesha fomu za uteuzi, 166,649 walienguliwa katika mchakato wa Uchaguzi nchi nzima kwa sababu mbalimbali za kipuuzi na zisizo na mashiko kabisa kama ilivyoelezwa na Viongozi wetu katika nyakati mbalimbali za mchakato huu. Wanachama wa ACT waliobakizwa kwenye Uchaguzi mpaka saa Sita kamili mchana leo ni 6,944 tu sawa na 4% ya wagombea wote tulioweka.

Sababu zote zilizotolewa na Serikali na Chama cha Mapinduzi kuondoa wanachama wetu katika kinyanganyiro cha Uchaguzi hatukubaliani nazo. Kamati ya Uongozi ya Chama taifa iliyoketi leo imeelekeza kuwa wanachama wetu wote waliobakizwa katika Uchaguzi WAJIONDOE katika Uchaguzi huo kwani kushiriki kwao ni kuhalalisha ubakaji wa Demokrasia uliofanywa na Serikali. Kwani kwa uenguaji huu wa wagombea kwa kutumia sababu zisizo na mantiki, si tu wamenyima wagombea wetu haki yao kikatiba, bali wamewanyima Wananchi wote wa Tanzania waliotimiza miaka 18 na zaidi haki yao, iliyopo katika Ibara ya 5 ya Katiba, ya kupiga kura. KWA KUWA CCM IMEONDOA WAGOMBEA WETU asilimia 96%, na sisi TUMEWASAIDIA KUONDOA asilimia 4% ya WALIOBAKIA.

Kamati ya Uongozi ya Chama Taifa inaona kuwa Dola imeshatuamulia vyama makini vya upinzani tusishiriki kwenye uchaguzi huu. Hawataki ushindani. Wanaogopa ushindani. Wanaogopa sanduku la kura. Wanawaogopa Watanzania. Kwa msingi huo, Kamati ya Uongozi inaona hakuna mantiki ya kushiriki uchafuzi ambao asilimia 96 ya wagombea wetu wameenguliwa. Unashiriki vipi uchaguzi ambao wagombea wako wameondolewa? Kamati ya Uongozi imeamua kuwaachia CCM uchafuzi wao na kwa hivyo ACT - Wazalendo inajiondoa kwenye uchafuzi huo.

Mwaka jana mwishoni, baada ya majadiliano marefu na wenzetu katika Upinzani, tulipitisha na kulitangza Azimio la Zanzibar, ambalo liliutangaza mwaka 2019 kuwa ni “MWAKA WA KUDAI DEMOKRASIA”, mwaka ambao tungepambana kuzidai haki zetu zote tunazonyimwa kinyume na sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hatujalitekeleza hilo, kwa matendo ya sasa ya CCM na Serikali, tumepewa nafasi ya kutekeleza Azimio la Zanzibar. ACT-Wazalendo tutakwenda kwa wenzetu wa Upinzani, ili kurudi kutekeleza Azimio la Zanzibar.

TUNAWAPA ARI wanachama na wafuasi wetu, pamoja na wananchi wote kwa ujumla, wakati ni sasa wa kuondoa hofu, kushikamana nasi katika kulinda Demokrasia ya nchi yetu. Hatupaswi kuwa waoga, hatupaswi kujisalimisha katika kudai haki zetu kama mtu mmoja mmoja na kama KUNDI ZIMA LA KIJAMII.

Tumejitahidi kufuata njia zote za kisheria Lakini CCM na Serikali yake wameamua vinginevyo kwa kutuondoa katika Uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji. Tumeamua kutafuta njia nyingine za kulinda demokrasia yetu. TUSILAUMIANE.

Mwisho; Kumekuwepo na vitendo viovu vinavyofanywa na Jeshi la Polisi na watendaji wa Serikali kuwabughudhi Wagombea wetu, wanachama na viongozi wetu maeneo mbalimbali nchini. Serikali ya Rais Magufuli isitufikishe kuvuka mstari wa Uvumilivu.

Kabwe Z, Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo
Dar es Salaam.

Novemba 8, 2019
MUVI ipo mwishoni saivi staring CCM ,ndiyo anaenda kukomboa majimbo take
Ndo ndindi
 
Kususa nako kuna kanuni zake, wewe ukisusa, wenzio twala.
.
P
Vingine haviliki.
Achana na haki za watu mkuu. Huwa haziombwi. Ipo siku watazidai.
Haya sio mambo ya kushabikia hata kidogo.
Mambo ya kugusa jamii moja kwa moja ni ya kuyaogopa kabisa
 
Kususa nako kuna kanuni zake, wewe ukisusa, wenzio twala.
.
P
Pascal Mayalla ifikie pahali tuukubali ukweli...wewe unaona haya yaliyotokea ni mazuri?
Kwa nini chama kiogope ushindani huru?
Maaana yake chama hakijiamini.fujo zilizofanywa safari hii ni aibu kubwa..
Pascal hili si swala la kulichukulia juu juu ujue athari zake ni kubwa mno na huenda zikadumu hadi 2025.
Niseme tu kama ni amani ya nchi hii watakaoivuruga ni hiki hiki chama chenye nguvu.
 
Tunaunga mkono juhudi ya serikali ya awamu yatano chini ya uongozi wa daktari kuwezesha Samata kuifunga goli livapuuli
 
Hayo yametangazwa na kiongozi wa chama hicho Mh Zitto Kabwe.

ACT WAZALENDO CHAIFUATA CHADEMA, CHAJITOA KUSHIRIKI UCHAGUZI. Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ametangaza kuwa chama hicho kimejitoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 24, 2019 kwa sababu kuwa wagombea wa chama hicho wengi wameenguliwa.
View attachment 1257821
ACT-WAZALENDO IMEJIONDOA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA:

MILANGO YA DEMOKRASIA IMEFUNGWA: TUSILAUMIANE

MSIMAMO WA ACT WAZALENDO KUHUSU UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, VIJIJI NA VITONGOJI WA NOVEMBA 24, 2019:

Chama cha ACT Wazalendo, kikiwa Chama cha siasa makini chenye usajili wa kudumu nchini, kiliitikia wito wa kushiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji uliokuwa ufanyike tarehe 24 Novemba 2019, tukiamini kuwa ni nafasi nyeti ya kuimarisha ushindani wa kisiasa nchini.

Licha ya miaka minne ya changamoto kubwa, na licha ya wananchi wengi kutuonya mapema kuwa hapatakuwa na Uchaguzi wa Haki, bado tuliamua kushiriki kikamilifu tukiamini kuwa taratibu, sheria na Katiba ya nchi itaheshimiwa na wahusika wote wa mchakato huu.

Wanachama wetu 173,593 walijitokeza kugombea nafasi mbalimbali za Uongozi kwa kujaza fomu za uteuzi na kuzirejesha na wengine wengi kwa maelfu walikataliwa kupewa fomu na au ofisi kufungwa kwa wakati wote. Wagombea Uenyekiti wa Mitaa walikuwa 2,481 kati ya Mitaa yote 4,264 nchini, Uenyekiti wa Vijiji walikuwa 8,218 katika ya Vijiji vyote 12,316 nchini, na uenyekiti wa Vitongoji walikuwa 35,457 kati ya Vitongoji vyote 64,384 nchini. Kwa upande wa Wagombea wa nafasi za Ujumbe wa Halmashauri za Vijiji na Kamati za Mtaa (wajumbe wa kawaida na wajumbe Wanawake) wanaACT 135,675 walijitokeza kuomba nafasi hizo.

Takribani, wananchi 173,593. Hata hivyo, kati ya wagombea wetu hao 173,593 waliochukua na kurejesha fomu za uteuzi, 166,649 walienguliwa katika mchakato wa Uchaguzi nchi nzima kwa sababu mbalimbali za kipuuzi na zisizo na mashiko kabisa kama ilivyoelezwa na Viongozi wetu katika nyakati mbalimbali za mchakato huu. Wanachama wa ACT waliobakizwa kwenye Uchaguzi mpaka saa Sita kamili mchana leo ni 6,944 tu sawa na 4% ya wagombea wote tulioweka.

Sababu zote zilizotolewa na Serikali na Chama cha Mapinduzi kuondoa wanachama wetu katika kinyanganyiro cha Uchaguzi hatukubaliani nazo. Kamati ya Uongozi ya Chama taifa iliyoketi leo imeelekeza kuwa wanachama wetu wote waliobakizwa katika Uchaguzi WAJIONDOE katika Uchaguzi huo kwani kushiriki kwao ni kuhalalisha ubakaji wa Demokrasia uliofanywa na Serikali. Kwani kwa uenguaji huu wa wagombea kwa kutumia sababu zisizo na mantiki, si tu wamenyima wagombea wetu haki yao kikatiba, bali wamewanyima Wananchi wote wa Tanzania waliotimiza miaka 18 na zaidi haki yao, iliyopo katika Ibara ya 5 ya Katiba, ya kupiga kura. KWA KUWA CCM IMEONDOA WAGOMBEA WETU asilimia 96%, na sisi TUMEWASAIDIA KUONDOA asilimia 4% ya WALIOBAKIA.

Kamati ya Uongozi ya Chama Taifa inaona kuwa Dola imeshatuamulia vyama makini vya upinzani tusishiriki kwenye uchaguzi huu. Hawataki ushindani. Wanaogopa ushindani. Wanaogopa sanduku la kura. Wanawaogopa Watanzania. Kwa msingi huo, Kamati ya Uongozi inaona hakuna mantiki ya kushiriki uchafuzi ambao asilimia 96 ya wagombea wetu wameenguliwa. Unashiriki vipi uchaguzi ambao wagombea wako wameondolewa? Kamati ya Uongozi imeamua kuwaachia CCM uchafuzi wao na kwa hivyo ACT - Wazalendo inajiondoa kwenye uchafuzi huo.

Mwaka jana mwishoni, baada ya majadiliano marefu na wenzetu katika Upinzani, tulipitisha na kulitangza Azimio la Zanzibar, ambalo liliutangaza mwaka 2019 kuwa ni “MWAKA WA KUDAI DEMOKRASIA”, mwaka ambao tungepambana kuzidai haki zetu zote tunazonyimwa kinyume na sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hatujalitekeleza hilo, kwa matendo ya sasa ya CCM na Serikali, tumepewa nafasi ya kutekeleza Azimio la Zanzibar. ACT-Wazalendo tutakwenda kwa wenzetu wa Upinzani, ili kurudi kutekeleza Azimio la Zanzibar.

TUNAWAPA ARI wanachama na wafuasi wetu, pamoja na wananchi wote kwa ujumla, wakati ni sasa wa kuondoa hofu, kushikamana nasi katika kulinda Demokrasia ya nchi yetu. Hatupaswi kuwa waoga, hatupaswi kujisalimisha katika kudai haki zetu kama mtu mmoja mmoja na kama KUNDI ZIMA LA KIJAMII.

Tumejitahidi kufuata njia zote za kisheria Lakini CCM na Serikali yake wameamua vinginevyo kwa kutuondoa katika Uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji. Tumeamua kutafuta njia nyingine za kulinda demokrasia yetu. TUSILAUMIANE.

Mwisho; Kumekuwepo na vitendo viovu vinavyofanywa na Jeshi la Polisi na watendaji wa Serikali kuwabughudhi Wagombea wetu, wanachama na viongozi wetu maeneo mbalimbali nchini. Serikali ya Rais Magufuli isitufikishe kuvuka mstari wa Uvumilivu.

Kabwe Z, Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo
Dar es Salaam.

Novemba 8, 2019
Kwa wale wenye upeo wa kuona parefu hususani kwenye mambo ya kisiasa,naomba kuwauliza nini hatima ya vyama vya upinzani kujitoa katika chaguzi kama hivi?
 
Back
Top Bottom