Binti Magufuli
JF-Expert Member
- Apr 2, 2011
- 7,484
- 5,142
Jamani mimi naandika hili nikiwa na machungu kutoka moyoni. Tarehe 19/05/2011 Chalz baba alihojiwa kuhusu tetesi za yeye kurudiana na Wema Sepetu, lakini majibu aliyojibu kwa kweli ilikuwa ni zaidi ya udhalilishwaji wa mwanamke (specifically Wema). Alisema eti Wema ni kama mfereji, daraja, malaya ambaye anajirahisha kwa wanaume ili aendeshe maisha yake kwani ni mvivu na hana bidii katika maisha. Na hivo kwa maneno hayo chalz baba akasema hawez kurudiana na malaya kama Wema.
Lengo la kuleta uzi huu si kwa ajili ya kumtetea Wema lakini kama a gender sensitive person chalz baba hakuwa sahihi kuongea maneno kama haya tena mazito kwenye chombo cha habari tena ambacho kinasikilizwa ulimwengu mzima. Baada ya yeye kumaliza shida zake ndo leo anamuona malaya?? kwani malaya anafanya hiyo tabia peke yake?? Ina maana hata yeye chalz baba inabidi aitwe hvo. Huyu mwanamume akumbuke kuwa na yeye ana mama, dada, na hata shangazi zake ambao ni wanawake na siku ya siku yanaweza kuwapata haya anayomfanyia wema leo. Je yakitokea kwa familia yake atafurahi??
Natoa wito kwa wanaume wooote kuweza kuepukana na udhalilishaji wa kijinsia kama huu ambao unaweza kuepukika. Angeweza kusema tu kwamba hana mpango wa kurudiana na wema bila kutamka hayo matusi.
Hakuna kama mama jamani, mwanamke yeyote ni mama. tuheshimianeni pamoja na kasoro tulizonazo.
MWISHO
Kama kawaida masharobaro wataniuliza source, source ni Clouds FM tar 19/5/2011 kipindi cha movie leo
Lengo la kuleta uzi huu si kwa ajili ya kumtetea Wema lakini kama a gender sensitive person chalz baba hakuwa sahihi kuongea maneno kama haya tena mazito kwenye chombo cha habari tena ambacho kinasikilizwa ulimwengu mzima. Baada ya yeye kumaliza shida zake ndo leo anamuona malaya?? kwani malaya anafanya hiyo tabia peke yake?? Ina maana hata yeye chalz baba inabidi aitwe hvo. Huyu mwanamume akumbuke kuwa na yeye ana mama, dada, na hata shangazi zake ambao ni wanawake na siku ya siku yanaweza kuwapata haya anayomfanyia wema leo. Je yakitokea kwa familia yake atafurahi??
Natoa wito kwa wanaume wooote kuweza kuepukana na udhalilishaji wa kijinsia kama huu ambao unaweza kuepukika. Angeweza kusema tu kwamba hana mpango wa kurudiana na wema bila kutamka hayo matusi.
Hakuna kama mama jamani, mwanamke yeyote ni mama. tuheshimianeni pamoja na kasoro tulizonazo.
MWISHO
Kama kawaida masharobaro wataniuliza source, source ni Clouds FM tar 19/5/2011 kipindi cha movie leo