Challenge ya 2011; matches na results

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
leo mashindano ya challenge yanatarajiwa kuanza leo ni timu yetu ya taifa itatimuana na Zambia katika ufunguzi wa mashindano haya

Tanzania itawakilishwa na zanzibar heroes na kilimanjaro heroes

dua na kila la heri kwa timu zetu

hiki ni kipimo chengine kwa timu zetu za taifa

ijapokua wataaluma wa soka wanabashiri kua timu zetu zitafanya vizuri

tufuatilie na kupashana habari hizo kupitia hapa
 
Hao Somalia vipi wameingiza timu? maana kulikuwa na tetesi kuwa tangu jana walikuwa bado hawajawasili japo ratiba inaonyesha wao wataanza kukipiga na Burundi leo.
 
hakuna mtu mwenye update ya mechi ya kilimanjaro stars na zambia, kama kuna mwenye matokeo mpaka sasa atujuze
 
mpaka half time walikuwa wameshalambwa 1-0.
washangiliaji walikuwa wanawazomea wachezaji na kocha paulsen
 
Kwa style hii sishangai kuona watanzania wengi wakiwa hawana mpango wa kuifuatilia hii timu maana inawaongezea pressure tu wakati umaskini tayari umeshawapiga kikumbo.
 
naam matokeo ya mwisho timu yetu imelala bao 1 bila ila inasemekana wamejitahidi sana

leo ndugu zao zanzibar stars inatupa karata yake tujitahidini kuiombea ifanye vyema
 
Katika mashindano haya kuna makundi matatu A,B na C kama ilivyo hapo chini
Jana tarehe 27/11/2010 yalianza na kwa bahati mbaya timu yetu imelala bao moja na zambia
Kundi A
Kilimanjaro Stars - Tanzania
Chipolopolo ya Zambia
Intamba ya Burundi
Somalia
Kundi B
Amavubi ya Rwanda
Ivory Coast
Sudan
Zanzibar Heroes
Kundi C
Uganda Cranes,
Harambee Stars ya Kenya,
Flames ya Malawi
Ethiopia.

 
leo kuna mitanange miwili

Sudan Vs zanzibar heroes (sijui kama watanzania wa visiwani wala supu ya pweza wanaweza kutufuta machozi ya kilimanjaro jana?)

na mtanange wa pili ni

Rwanda (sijui ndio ile Amavubi ?) Vs Ivorycoast

zote zitakuwa saa kumi za jioni
 
Match ya Zanzibar na "Southern" Sudan ipo LIVE Supersports9,TBC1 n KBC1 Ni Half time sasa Zanzibar wanaongoza kwa goli 1 "Southern" Sudan

MY TAKE; Naiita "SOUTHERN SUDAN" kwani hakuna Mwarabu hata mmoja!!!
 
Samahani kwani jana wasomali matokeo yao yalikuwaje, au hawakuingiza timu uwanjani?
 
Back
Top Bottom