BWANKU M BWANKU
JF-Expert Member
- Jan 12, 2019
- 328
- 414
CHALINZE YAONGOZA UKUSANYAJI MAPATO NCHINI. YATIA FORA PIA UPELEKAJI WA FEDHA NYINGI ZA MIRADI YA MAENDELEO.
Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani inayoongozwa na Mbunge Mhe. Ridhiwani Kikwete ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeongoza katika Halmashauri zote nchini kwa ukusanyaji wa Mapato kwa kuwa Namba 1 kati ya Halmashauri zote nchini huku ikiwa ya pili pia nchini kwa kupeleka fedha nyingi za miradi ya maendeleo kwa mapato ya ndani baada ya Dodoma. Hii ni kwa Mujibu wa Taarifa kuhusu Mapato na Matumizi ya ndani ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 iliyosomwa Jana Jumanne Agosti 02, 2022 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR- TAMISEMI).
Chalinze imekusanya Jumla ya Bilioni 10.2 kati ya Bilioni 10.7 ilizopanga kukusanya kwenye Mwaka wa Fedha 2021/2022 huku ikishika nafasi ya pili nchini kwa kupeleka fedha nyingi zaidi za miradi ya maendeleo baada ya Dodoma. Halmashauri ya Chalinze imepeleka fedha za miradi ya maendeleo kwa asilimia 60 kupitia mapato ya ndani.
Akitoa pongezi kwa kazi kubwa iliyofanywa na Uongozi mzima wa Halmashauri ya Chalinze, Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema:-
"Niwapongeze sana Mwenyekiti wangu wa Halmashauri, Madiwani wenzangu, Mkurugenzi wetu na watendaji wote wa Halmashauri yetu ya Wilaya ya Chalinze Kwa kuwa Halmashauri No.1 kwa upande wa Halmashauri zote za Wilaya nchini. Tumekusanya kiasi cha bilioni 10.2 kati ya billion 10.7 tulizokuwa tumepanga kukusanya. Na pia kuwa Halmashauri No. 2 Nchini kwa upelekaji wa fedha za Miradi ya maendeleo kwa mapato ndani kwa 60% baada ya Dodoma CC."
Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani inayoongozwa na Mbunge Mhe. Ridhiwani Kikwete ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeongoza katika Halmashauri zote nchini kwa ukusanyaji wa Mapato kwa kuwa Namba 1 kati ya Halmashauri zote nchini huku ikiwa ya pili pia nchini kwa kupeleka fedha nyingi za miradi ya maendeleo kwa mapato ya ndani baada ya Dodoma. Hii ni kwa Mujibu wa Taarifa kuhusu Mapato na Matumizi ya ndani ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 iliyosomwa Jana Jumanne Agosti 02, 2022 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR- TAMISEMI).
Chalinze imekusanya Jumla ya Bilioni 10.2 kati ya Bilioni 10.7 ilizopanga kukusanya kwenye Mwaka wa Fedha 2021/2022 huku ikishika nafasi ya pili nchini kwa kupeleka fedha nyingi zaidi za miradi ya maendeleo baada ya Dodoma. Halmashauri ya Chalinze imepeleka fedha za miradi ya maendeleo kwa asilimia 60 kupitia mapato ya ndani.
Akitoa pongezi kwa kazi kubwa iliyofanywa na Uongozi mzima wa Halmashauri ya Chalinze, Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema:-
"Niwapongeze sana Mwenyekiti wangu wa Halmashauri, Madiwani wenzangu, Mkurugenzi wetu na watendaji wote wa Halmashauri yetu ya Wilaya ya Chalinze Kwa kuwa Halmashauri No.1 kwa upande wa Halmashauri zote za Wilaya nchini. Tumekusanya kiasi cha bilioni 10.2 kati ya billion 10.7 tulizokuwa tumepanga kukusanya. Na pia kuwa Halmashauri No. 2 Nchini kwa upelekaji wa fedha za Miradi ya maendeleo kwa mapato ndani kwa 60% baada ya Dodoma CC."