The Sunk Cost Fallacy
JF-Expert Member
- Dec 1, 2021
- 19,589
- 14,137
Habari Wana JF,
Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Albert Chalamila Amesema alikuwa likizo tuu kama Injini ya gari lililoharibika..
Kuharibika kwa Board haimaanishi Injini ni mbovu.👇
===
MKUU wa Mkoa wa Kagera Albert Chalamila amesema alikuwa likizo kama injini ya gari lililoharibika.
Ameyasema hayo leo Agosti 4, 2022 wakati akikabidhiwa ofisi na aliyekuwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Charles Mbuge.
Amesema kwa sasa amerudi kama gari jipya na yuko tayari kufanya kazi kwa bidii ili kuwaletea wananchi maendeleo.
Aidha, amewetaka Wakuu wa Wilaya mkoani humo kufanya kazi kwa bidii kwani vyeo vya kuteuliwa ni vya mzunguko na kila mmoja Mungu umpa kwa wakati wake.
Amesema kama watafanya kazi kwa hofu ya kutoteuliwa tena basi wataaribu kazi na kushindwa kuwatumikia wananchi.
Amesema utekelezaji ambao ataanza nao ni maagizo ya Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu,wakati alipofanya ziara yake mkoani Kagera na kuwataka viongozi kuhakikisha wanatafuta njia ya kuufanya mkoa wa Kagera kuwa mkoa mwenye uchumi wa juu kwa sababu unakila kigezo cha kuwa Mkoa wenye uchumi mkubwa.
Awali akikabidhi ofisi Jenerali Mbuge alimuomba mkuu huyo wa mkoa kufanikisha maswala ya kitaifa kwa kuanza na Sensa ya watu na makazi, kufanikisha kuhitimisha mbio za mwenge kitaifa, kuhakikisha mradi wa bomba la mafuta unafanikiwa na wananchi wanalipwa fidia.
Chanzo: Habari Leo
Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Albert Chalamila Amesema alikuwa likizo tuu kama Injini ya gari lililoharibika..
Kuharibika kwa Board haimaanishi Injini ni mbovu.👇
===
Ameyasema hayo leo Agosti 4, 2022 wakati akikabidhiwa ofisi na aliyekuwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Charles Mbuge.
Amesema kwa sasa amerudi kama gari jipya na yuko tayari kufanya kazi kwa bidii ili kuwaletea wananchi maendeleo.
Aidha, amewetaka Wakuu wa Wilaya mkoani humo kufanya kazi kwa bidii kwani vyeo vya kuteuliwa ni vya mzunguko na kila mmoja Mungu umpa kwa wakati wake.
Amesema kama watafanya kazi kwa hofu ya kutoteuliwa tena basi wataaribu kazi na kushindwa kuwatumikia wananchi.
Amesema utekelezaji ambao ataanza nao ni maagizo ya Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu,wakati alipofanya ziara yake mkoani Kagera na kuwataka viongozi kuhakikisha wanatafuta njia ya kuufanya mkoa wa Kagera kuwa mkoa mwenye uchumi wa juu kwa sababu unakila kigezo cha kuwa Mkoa wenye uchumi mkubwa.
Awali akikabidhi ofisi Jenerali Mbuge alimuomba mkuu huyo wa mkoa kufanikisha maswala ya kitaifa kwa kuanza na Sensa ya watu na makazi, kufanikisha kuhitimisha mbio za mwenge kitaifa, kuhakikisha mradi wa bomba la mafuta unafanikiwa na wananchi wanalipwa fidia.
Chanzo: Habari Leo