Mpingamkoloni
Member
- Feb 14, 2021
- 13
- 32
Mheshimiwa Samia!
Ninakubaliana na uteuzi wako kwa Mhe. Chalamila kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza. Kijana mdogo, mchapakazi, lakini mara nyingi huwa anakuwa moto na kukosa busara, kitu ambacho kwa umri wake bado ana muda mwingi wa kujifunza.
Lakini taarifa zinasema, kwa muda mrefu sana Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Chalamila, ameshindwa kutatua mgogoro wa Bajaj na Daladala barabarani. Taarifa zaidi zinasema Mkuu wa Mkoa amekuwa akiegemea sana upande wa bajaj na kuwajibu hovyo waendesha daladala, huku tetesi zikidai hii inatokana na mmoja wa wanasiasa mashuhuri hapo Mbeya kuwa na taasisi inayokopesha bajaj ambazo zimetapakaa katikati ya mji.
Mpaka sasa ninapoongea wananchi wanaotegemea usafiri wa daladala jijini Mbeya wanahaha kutafuta usafiri.
Chalamila kijana mzuri sana, ila asiache tatizo kwa Mkuu wa Mkoa Homera. Alimalize. Pia, wanasiasa waache kuleta migongano ya kimaslahi.
Ninakubaliana na uteuzi wako kwa Mhe. Chalamila kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza. Kijana mdogo, mchapakazi, lakini mara nyingi huwa anakuwa moto na kukosa busara, kitu ambacho kwa umri wake bado ana muda mwingi wa kujifunza.
Lakini taarifa zinasema, kwa muda mrefu sana Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Chalamila, ameshindwa kutatua mgogoro wa Bajaj na Daladala barabarani. Taarifa zaidi zinasema Mkuu wa Mkoa amekuwa akiegemea sana upande wa bajaj na kuwajibu hovyo waendesha daladala, huku tetesi zikidai hii inatokana na mmoja wa wanasiasa mashuhuri hapo Mbeya kuwa na taasisi inayokopesha bajaj ambazo zimetapakaa katikati ya mji.
Mpaka sasa ninapoongea wananchi wanaotegemea usafiri wa daladala jijini Mbeya wanahaha kutafuta usafiri.
Chalamila kijana mzuri sana, ila asiache tatizo kwa Mkuu wa Mkoa Homera. Alimalize. Pia, wanasiasa waache kuleta migongano ya kimaslahi.