Hapanabila shaka ukiwa unasoma advance
hamna uchafu nyie mliozoea mbogs saba kujisevia watoto wa mama mtajulia wap? jarbu siku 1 tena kina afyaKubali tu huu ni uchafu.
Hivi utapikaje ugali na nyama sufuria moja?
Ingekua wali ningekuelewa,ila ugali hapana.
Watoto wa kishua bana.. ugali kabichi una shida gani? Kabichi ni dawa ya kansa na mambo mengi. Tatizo wabongo siku hizi tunaona kula mboga za majani ni umasikini, wakati ndo mambo yote
Nilienda kwenye nyumba ya WA Congo nikakaribishwa ugali WA Dona na kisamvu kilichokatwa makubwa makubwa kama tembele limekaangwa Tu ni kama unakula majani mabichi
Afu kadri kimo chako kinavokuwa kidogo na umbile dogo,ndo akili inakuwaga ndogo ndogo hasa ya utatuzi wa matatizo na uvumbuzi sijui kwanini.Lakini cha kushangaza ndio tunaongoza kuwa na maumbo madogo compared to hao wanaokula vitu vya ajabu ajabu.
Mchongo Gani huko pori masta.Nlikuwa NAKONDE pori nkakuta watu wa nakula panya na viazi vya kuchoma.
Nkatulia ku soma mchezo
Nilishaalikwa na watu wa Sierra Leone msosi, Ile nakoroga naibua nyama mkono wa nyani, sijui ngedere, sikuchukua mchuzi hata wa kuku, hata samaki niliogopa waweza kulishwa nyoka, nikala mlenda walipika na ugali wao mchungu!
Aisee nikaapa sili nyama nyumbani Kwa wasio watz!
Dagaa mwanza mixe mchicha,kwa anko,
Yaani nilikuwa nakula ugali nawaza kumeza,chakula kinajaa mdomoni,aisee halafu mchicha silagi
Chakula kilinishinda,nusunusu nitapikie kwenye sahani ya chakula.
Sent using Jamii Forums mobile app
Umenikumbusha nilishawahi kukaribishwa chakula af ikawa ugali na mtindi af mi mtindi sijawahi kuuelewa hata robo, aloooo nilipata wakati mgumu balaaNikienda kwa mtu huwa napenda kwenda nikiwa nimeshiba kabisa kuondoa adha.Nilishawahi kula ugali na maziwa mtindi nikiwa nasoma,hiyo ilikuwa ni baada ya kumtembelea ndugu baada ya kutoka shule,nilikuwa na ubao balaa ila nilishhiba baada ya tonge tatu.Mtindi ulikuwa mchungu alafu jikoni walikuwa wanakaanga samaki.
Mlenda naukupenda Sanaa yaaniMlenda, duuu hapana kwa kweli hiki chakula wanaokula sijui hata wanakulaje, nahisi hata chombo changu sitaki kiguse hiki chakula
Yaan ww bimdashi kila kitu unasema kimekushinda sasa unakula nini mwenzetu?Mie zimenishinda wallah,
Maana watu wanazisifia sana eti,nikasema ninunue nami nione, loooh wala sikumeza.
Sent using Jamii Forums mobile app
Masai akila samaki?Mchaga akila mihogo anakufa aisee