Chakula cha mchana kwa wafanyakazi kinaleta motisha kwenye ufanisi

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Chakula cha mchana makazini kina siri kubwa katika kuleta ufanisi. Wakati wa Ukoloni mashirika mengi ya watu binafsi yalitoa chakula cha mchana kwa wafanyakazi. Kwakua ubaguzi wakati ule ulikua ni wa wazi Wazungu ambao walikua ni wachache wenye nafasi za juu walitaarishiwa milo mizuri na kwa kiwango. Wazawa walitengenezewa wali maharage au ugali maharage.

Hata kama mfanyakazi atachangia kidogo katika chakula lakini ana uhakika wa kula mlo mmoja kwa siku. Wengine wana matatizo yao binafsi, nyumbani anaondoka hajakula kitu na mchana hana uwezo wa kununua chakula. Watu kama hawa wakipata mlo kazini mawazo yake yanakua katika uzalishaji.

Kupika chakula cha wafanyakazi si gharama kubwa kama kampuni inazalisha faida. Canteen unaweka wali nyama mchicha au ugali nyama mchicha, makande mchicha au chapati maharage au nyama.

Kibaruani kwetu kuna canteen ya wafanyakazi na wageni, bei si sawa na mtaani. Wamepunguza pakubwa, mfano wali nyama na mchicha 1,200.
Ingawa si shirika la mtu binafsi lakini nineona ni wazo zuri.

Waajiri mnapojaribu kutatua changamoto za maisha kwa wafanyakazi wenu inaleta tija. Wakoloni walijenga mpaka quarter’s na walivuna jasho la babu zetu kweli.
 
Hakika umesema kweli. Yule mkurugenzi mkuu au mtendaji mkuu wa DAWASCO Dar es salaam alikuwa mtendaji bora kitaifa alipokuwa anazungumzia siri ya mafanikio alisema, " anatoa chai kwa wafanyakazi wote asubuhi kabla ya kuanza kazi" ni kitu kidogo ila kina impact kubwa sana kwa ufanisi wa kazi.
 
Hakika umesema kweli. Yule mkurugenzi mkuu au mtendaji mkuu wa DAWASCO Dar es salaam alikuwa mtendaji bora kitaifa alipokuwa anazungumzia siri ya mafanikio alisema, " anatoa chai kwa wafanyakazi wote asubuhi kabla ya kuanza kazi" ni kitu kidogo ila kina impact kubwa sana kwa ufanisi wa kazi.
Ninakumbuka kampuni aliyofanya kazi marehemu baba yangu, yeye ni wale walioajiriwa kabla ya Uhuru. Anasema officers mess ilikua na vyakula vizuri lakini kulikuwa na mess ya wazawa pia. Huko kuna mpaka makande ya nazi.
 
Chakula cha mchana makazini kina siri kubwa katika kuketa ufanisi. Wakati wa Ukoloni mashirika mengi ya watu binafsi yalitoa chakula cha mchana kwa wafanyakazi. Kwakua ubaguzi wakati ule ulikua ni wa wazi Wazungu ambao walikua ni wachache wenye nafasi za juu walitaarishiwa milo mizuri na kwa kiwango. Wazawa walitengenezewa wali maharage au ugali maharage.

Hata kama mfanyakazi atachangia kidogo katika chakula lakini ana uhakika wa kula mlo mmoja kwa siku. Wengine wana matatizo yao binafsi, nyumbani anaondoka hajakula kitu na mchana hana uwezo wa kununua chakula. Watu kama hawa wakipata mlo kazini mawazo yake yanakua katika uzalishaji.

Kupika chakula cha wafanyakazi si gharama kubwa kama kampuni inazalisha faida. Canteen unaweka wali nyama mchicha au ugali nyama mchicha, makande mchicha au chapati maharage au nyama.

Kibaruani kwetu kuna canteen ya wafanyakazi na wageni, bei si sawa na mtaani. Wamepunguza pakubwa, mfano wali nyama na mchicha 1,200.
Ingawa si shirika la mtu binafsi lakini nineona ni wazo zuri.

Waajiri mnapojaribu kutatua changamoto za maisha kwa wafanyakazi wenu inaleta tija. Wakoloni walijenga mpaka quarter’s na walivuna jasho la babu zetu kweli.
Kuna taasisi kibao zinafanya kwa Arusha nimeona ila sijui Dar, Ila ni zile zilizoko nje sana ya Mji na ambazo zinaina kuruhu staff wakale warudi ni kupoteza muda
 
Hii sio kwa ngazi ya taasisi na makampuni tu hata kwenye ngazi za familia,we wahakikishie mafundi wako uhakika wa msosi uone watakavyokimbiza kazi yako
 
Hii sio kwa ngazi ya taasisi na makampuni tu hata kwenye ngazi za familia,we wahakikishie mafundi wako uhakika wa msosi uone watakavyokimbiza kazi yako
Ndiyo tunavyofanya kule bush, wakati wa kuvuna mahindi. Mnavuna na kusomba mahindi mpaka kwenye gari. Saa nane ugali dagaa na maharage vimeiva. Wanaume wanapiga msosi wakikunja na 10,000 mkononi ya day waka wanaondoka.
 
Back
Top Bottom