Chaguzi ndogo na "ujinga" wetu watanzania

Bongolander

JF-Expert Member
Jul 10, 2007
5,067
2,197
Kwanza kwa unyenyekevu mkubwa naomba msinielewe vibaya kwa kuanza na kichwa chenye ukakasi kiasi, nikaonekana natumia lugha mbaya.Ujinga ni hali ambayo inaweza kuondolewa kwa kuelimishwa, so it is not a permanent condition na isieleweke kuwa ni tusi.

Nimekuwa naangalia chaguzi ndogo kwa jicho la pili, na kujaribu kuwa realists na sio idealist. Nimefanya hivi kwa kuangalia gharama na manufaa yake, na kufikia hitimisho kuwa hizi changuzi ni kama mtindo fulani wa kutwisha mzigo wavuja jasho kuwanufaisha wanasiasa, na kuwafurahisha wahisani na jumuiya ya nchi za magharibi. Yaani ni kama tunalipia bili ya mtu ambaye anajiburudisha kwa mchezo wa kisiasa.

Kwanza nimejiuliza: Kwanini kila uchaguzi mdogo unapotokea, fedha za kuugharamia hazijawahi kukosekana? Kila ukisikia uchaguzi mdogo katika jimbo fulani, fedha zinakuwa tele. Lakini kwenye majimbo hayo hayo ya uchaguzi, unaweza kusikia fedha ambazo ni pungufu ya zile zinazotumika kugharamia uchaguzi, zinakosekena kwenye miradi kama ya ujenzi wa zahanati, madaraja, barabara, umeme, maji, shule etc …

Najiuliza kama ni kweli huwa zinakosekana au si kweli, au hali halisi ni kuwa mambo hayo yanayowagusa wananchi sio kipaumbele kama ilivyo kwa mambo ya siasa. Inawezekana sina busara za kutosha kujua hekima iliyomo ndani ya jambo hili. But I do believe we can find our own formular which can be acceptable to vyama vyote bila kufuja hela kwenye bi-elections ambazo kimsingi hazibadilishi mwelekeo wa bunge.

Pili, kwa mtu mwenye akili timamu kwa sasa atajua kabisa kuwa chaguzi ndogo zote iwe kwa Nassari, kwa Lissu au kwingine kokote, mshindi atakuwa mgombea wa CCM. Matokeo yatakuwa hiyo… kama kuna mtu atabisha basi aseme… lakini swali langu ni kuwa kwa nini tutumie mapesa mengi kwenye kufanya kitu ambacho tayari matokeo yake tunayajua? Kwanini tuzitumie akili na busara ya kutafuta njia ya kuweka mtu wa CCM, halafu pesa zote hizo tutumie kwenye jambo la kijamii litakalowanufaisha wanajimbo wote kwa muda mrefu? Au ni kwamba tunafanya mizungu kuwafurahisha wazungu wakati tunaoumia ni walipa kodi? Ninachokiona ni kuwa chaguzi hizo hazifanywi kwa ajili ya wanajimbo, au kwa ajili ya Tanzania, ni chaguzi kwa ajili ya kufurahisha nchi za magharibi, lakini kwa gharama zetu. Kweli inauma sana.

Tatu, tukiangalia mbali zaidi…in realistic terms … 2020 mshindi atakuwa mgombea wa CCM kwenye kiti cha urais, labda Bunge litakuwa asilimia 90 CCM, asilimia 10 upinzani, more or less. Tujaribu kuangalia pesa zitakazotumika kwenye jambo hili ambalo tayari kimsingi liko wazi. Swali ni je, ina maana tumeshindwa kutafuta njia zetu wenyewe watanzania za gharama nafuu kufanikisha hilo? Hela ambazo zinagharamia uchaguzi zingeenda kwenye maendeleo ya jamii, naamini ingekuwa ni matumizi mazuri ya fedha kwa manufaa ya muda mrefu.

Mwanzo kabisa nimejitaja kuwa mimi ni realist na sio idealist. Kwa hiyo niseme wazi tu kuwa demokrasia ya uchaguzi hapa Tanzania naiona kama ni mizungu kwa ajili ya wazungu. Ni bora tufute ujinga, na hizo pesa tunazopeleka kwenye uchaguzi zitumike kwenye maendeleo kwenye majimbo. Bora mizungu kwa ajili ya maendeleo yetu, kuliko kwa wazungu.
 
Habari Mkuu,

Usemacho ni HAKIKA na KWELI kwamba mshindi wa uchaguzi bila kujali ni kihalali au sio kihalali atatoka "chama tawala" ila sababu ya kutotumia pesa kwa kigezo cha mkujua atakaye tangwaza ni kibaya sana maana hakuna kizuri kilicho rahisi.

Kumbuka "cheap is expensive",maana yake ni kwamba thamani ya Demokrasia ni zaidi ya PESA. Tatizo letu ni sheria yetu inasemaje inatasfiri vipi Demokrasia..?
 
Kwanza, nianze kwa kuwalumu watanzania wenyewe nikiwa miongoni mwao kwa sababu watanzania tumekuwa waoga, wanyonge sana hata pale tunapoona kodi zetu zinatumiwa vibaya. Tumenyamazishwa kiasi kwamba hata tukiambia kila siku tuwe tunaenda kupiga deki nyumbani kwa mfalme itawezekana.Watanzania tumekuwa ni watu wa kupokea tu amri, taratibu mbalimbali n.k pasipo hata kuhoji kitu chochote.

Haya yote yanatokea hivyo kwa sababu ya ukosefu wa elimu, kutokulelewa katika msingi ya kuhoji ndiyo maana tumekuwa watu wa kupokea tu amri etc.Kwa sababu viongozi wameishatambua kuwa watanzania hatuwezi kuhoji ndiyo maana huwa wanaenda mbali zaidi kwa kufanya maamuzi yao binafsi na kutuletea sisi wananchi maana wanajua tutayapokea bila pingamizi lolote.

Pia viongozi ambao wapewa dhamana ya kutuongoza wamekuwa waoga, watu ambao kazi yao kubwa ni kulinda maslahi ya matumbo yao na siyo maslahi ya wananchi wao kwa ujumla. Pia hawapo kwa ajili ya kulinda misingi ya demokrasia nchini bali kuwafurahisha mabeberu bila kuangalia/ kuzingatia mateso wanayoyapata wananchi wake.

Mwisho, utumiaji mbaya wa kodi za wananchi ni kwa sababu tu tuna katiba mbovu sana ambayo ni toothless dog. Katiba isiyo wabana viongozi wajikite katika miiko ifaayao. And that's why hawa viongozi wanafanya madudu kwa ujasiri mkubwa sana wakijua na kutambua kuwa nothing will happen to them.
 
Mkubwa joshydama kweli hili hata tukisema tulaumiane haitasaidia sana. Ni kuwashawishi wenzetu kukubaliana na ukweli kuwa tunapoteza pesa kwenye mambo ambayo hayana tija.

Pesa za uchaguzi zikijenga shule moja ya kisasa ni bora sana. Tunaweza kulaumu Katiba, lakini siamini kama ikibadilika itabadilisha jambo hili.
 
Habari Mkuu,

Usemacho ni HAKIKA na KWELI kwamba mshindi wa uchaguzi bila kujali ni kihalali au sio kihalali atatoka "chama tawala" ila sababu ya kutotumia pesa kwa kigezo cha mkujua atakaye tangwaza ni kibaya sana maana hakuna kizuri kilicho rahisi.

Kumbuka "cheap is expensive",maana yake ni kwamba thamani ya Demokrasia ni zaidi ya PESA. Tatizo letu ni sheria yetu inasemaje inatasfiri vipi Demokrasia..?
Cheap is expensive yes, but new is even more expensive. Ukweli ni kuwa ni hatari kuwanyima watu haki ya kuchagua kiongozi wanayemtaka.

Lakini kama kiongozi atakayechaguliwa tayari tunamfahamu, kwanini asisimikwe tu, na hizo hela tutumie kwenye mengine kama maji, dawa, barabara ... ?
 
Kwanza, nianze kwa kuwalumu watanzania wenyewe nikiwa miongoni mwao kwa sababu watanzania tumekuwa waoga, wanyonge sana hata pale tunapoona kodi zetu zinatumiwa vibaya. Tumenyamazishwa kiasi kwamba hata tukiambia kila siku tuwe tunaenda kupiga deki nyumbani kwa mfalme itawezekana.Watanzania tumekuwa ni watu wa kupokea tu amri, taratibu mbalimbali n.k pasipo hata kuhoji kitu chochote.

Haya yote yanatokea hivyo kwa sababu ya ukosefu wa elimu, kutokulelewa katika msingi ya kuhoji ndiyo maana tumekuwa watu wa kupokea tu amri etc.Kwa sababu viongozi wameishatambua kuwa watanzania hatuwezi kuhoji ndiyo maana huwa wanaenda mbali zaidi kwa kufanya maamuzi yao binafsi na kutuletea sisi wananchi maana wanajua tutayapokea bila pingamizi lolote.

Pia viongozi ambao wapewa dhamana ya kutuongoza wamekuwa waoga, watu ambao kazi yao kubwa ni kulinda maslahi ya matumbo yao na siyo maslahi ya wananchi wao kwa ujumla. Pia hawapo kwa ajili ya kulinda misingi ya demokrasia nchini bali kuwafurahisha mabeberu bila kuangalia/ kuzingatia mateso wanayoyapata wananchi wake.

Mwisho, utumiaji mbaya wa kodi za wananchi ni kwa sababu tu tuna katiba mbovu sana ambayo ni toothless dog. Katiba isiyo wabana viongozi wajikite katika miiko ifaayao. And that's why hawa viongozi wanafanya madudu kwa ujasiri mkubwa sana wakijua na kutambua kuwa nothing will happen to them.
Kwani elimu ni nini? ni upumbavu wetu tu na wala si elimu,fuatilia kinachoendelea Malawi kwa sasa,,wamalawi wanaelimu kutuzidi?Wamalawi walio wengi ni maskini kuliko sisi ila wanaipenda nchi yao.sisi hatujipendi wenyewe wala kuipenda nchi yetu na zaidi sisi ni wapumbavu,mfano Jeshi letu JWTZ au police wetu kufungamana na chama tawala au kudanganyana kwamba chama tawala au serikali ndo inawalipa mshahara nao ni kwa sababu hawana elimu?au ni upumbavu tu?
 
Mie naona nisichangie. ..uzi uende kistaarabu hv hv huenda labda watu tukaamka!jamani msichafue huu uzi kwa habari zenu za kutetea madhaifu ya serikali..kwenye udhaifu usemwe,ukemewe,ukataliwe..mie sina maneno ya busara kwa leo!

Mkuu changia tu as long as hakuna lugha mbaya, maoni tofauti au yanaoyofanana ndio motto ya JF. Unajua baadhi ya mambo tuwe tunaongea kwa kuzungatia hali hisi ya nchi yetu, na sio kutumia nadharia za kimagharibi ambazo zinaishia kutuumiza watanzania. Na
 
Tabia ya watanzania kuwa makondoo ni mifumo ya maisha inayowalea kuanzia kwenye familia hadi shuleni.

Mtoto anakulia katika mazingira ya kumjaza uoga hadi anakuwa mtu mzima ni mtu hasiyejiamini.

Ili kuweza kubadili huu ujinga wa watanzania wengi ni lazima mabadiliko yaanzie ngazi ya familia. Demokrasia ya kweli ianzie kwenye familia zetu.
 
Tabia ya watanzania kuwa makondoo ni mifumo ya maisha inayowalea kuanzia kwenye familia hadi shuleni.

Mtoto anakulia katika mazingira ya kumjaza uoga hadi anakuwa mtu mzima ni mtu hasiyejiamini.

Ili kuweza kubadili huu ujinga wa watanzania wengi ni lazima mabadiliko yaanzie ngazi ya familia. Demokrasia ya kweli ianzie kwenye familia zetu.


Wewe umemaliza..yaan sis ni woga sijapata ona...kuna upuuz fulan uko huku nakoishi..unakutaka uwe na vitambulisho viwili...uvilipie vyte .ss mie nilihoji kwakweli nieleweshwe..wakaniambia hv ww dada kwann kila kitu unahoji..eti jitu badala ya kunielewesha anaanza leta siasa..eti usilete siasa utamalizwa ww..eish...mie ngachoka kbs..!

On top of that watanzania tu WABINAFSI sana..yaan unajiangalia ww tu na familia yako..hatufikirii vizaz vijavyo..mie nekereka sana jaman
 
Watu weusi Ni vigumu Sana kuendelea, tunawangiziaga TU mabeberu kuwa ndo wanao tukwamisha ila tunasahau kuwa sisi wenyewe ndo tunajikwamisha big time.......
Mtoa mada umegusia kuwa tunafanya demokrasia kwa kuwa kuwafurahisha mabeberu/wahisani ila me Nadhani huwa wanatucheka Sana nakutuona sisi mapimbi, kuwafanya maigizo ya chaguzi kwa lengo la kuwafurahisha wao huku wenyewe tukiumia nakuzidi kuwa maskini ...
Hivi kweli hizo bilioni 2+ za uchaguzi jimbo la lissu si zinatosha KABISA kujenga shule moja ya a level ya sayansi na vifaa vya kisasa kwenye maabara zake.... Ili watoto watakao maliza shule za kata Jimbo Hilo mchepuo wa sayansi wachaguliwe hapo ikiwezekana wakasome bure kwa kipindi Cha miaka 5, ukizingatia mishaara ya ubunge wa lisu iliyo baki ya miezi 12+, na kiinua mgongo chake Cha ubunge zaidi ya miliono 200 zikatumike kulipa posho ya mazingira ya kazi ya walimu wa shule hiyo......

Inasikitisha Sana, ila "za kuambiwa........"
 
Watu weusi Ni vigumu Sana kuendelea, tunawangiziaga TU mabeberu kuwa ndo wanao tukwamisha ila tunasahau kuwa sisi wenyewe ndo tunajikwamisha big time.......
Mtoa mada umegusia kuwa tunafanya demokrasia kwa kuwa kuwafurahisha mabeberu/wahisani ila me Nadhani huwa wanatucheka Sana nakutuona sisi mapimbi, kuwafanya maigizo ya chaguzi kwa lengo la kuwafurahisha wao huku wenyewe tukiumia nakuzidi kuwa maskini ...
Hivi kweli hizo bilioni 2+ za uchaguzi jimbo la lissu si zinatosha KABISA kujenga shule moja ya a level ya sayansi na vifaa vya kisasa kwenye maabara zake.... Ili watoto watakao maliza shule za kata Jimbo Hilo mchepuo wa sayansi wachaguliwe hapo ikiwezekana wakasome bure kwa kipindi Cha miaka 5, ukizingatia mishaara ya ubunge wa lisu iliyo baki ya miezi 12+, na kiinua mgongo chake Cha ubunge zaidi ya miliono 200 zikatumike kulipa posho ya mazingira ya kazi ya walimu wa shule hiyo......

Inasikitisha Sana, ila "za kuambiwa........"

Mkuu ningependa wengi tuangalie hili kwa mtazamo huu. Kinachofanyika ni kupoteza pesa tu kwenye mchezo wa siasa. Ikijengwa shule au hospitali itakuwa na maana sana kwa wanajimbo, na hata watanzania wengine wasio wanajimbo kwa muda mrefu sana. Huu ni ukweli ambao ni kama hatuataki kuukubali.
 
Nadhani tuungane kupiga kelele tukiaanisha faida za uhakika zitakazo tokana na hela zitazo okolewa kwa kuachana na uchaguzi huu mdogo, kulinganisha na hasara/faida zisizo za uhalisia za kufanya uchaguzi huo kwakuzingatia muda uliobaki Hadi kufikia uchaguzi mkuu 2020.....

Ni zaidi ya 2.5 billion (gharama ya uchaguzi 2 bilioni, mishahara miezi 12+ zaidi ya milioni 100, kiinua mgongo 200+milioni) zinaweza kuokolewa na kupelekwa kwenye jimbo husika kufanya kitu chenye maendeleo chanya kwa haraka na kitakacho endelea kunufaisha wat kwa muda mrefu Sana.

Maji au Shule au kuboresha zahanati(vifaa tiba au hata Kujenga/kuboresha wodi za kinamama) au hata kuboresha miundo mbinu ya maji(vyoo) kwenye zahanati za Jimbo Hilo....
 
Tatizo kubwa linalotukumba sisi watanzania ni kutokuwa na elimu juu ya haki zetu. Na ninapo sema elimu simaanishi elimu ya shule ya msingi, sekondari wala chuo kikuu hapana namanisha, uelewa wa mambo mbalimbali yanayoikumba jamii yetu. Ukosefu huu wa elimu naona sasa unaendelea kudidimiza maisha ya watanzania kwa sababu watawala wanaendelea kufanya mambo ya hovyo sana bila sisi kuhoji kitu chochote.

Kwa ukosefu wa elimu, leo hii vinajana wa vyuo vikuu wanamini kuwa ili upate ajira ni lazima uwe na mwanachama na uwe na kadi ya chama tawala. Leo hii kijana anamini kuwa serikali haiwezi kukuletea maendeleo kwahiyo unatakiwa upambane wewe mwenyewe hata kama mazingira ya kupambania ni mabovu. Je, hapo nchi yetu tunaipeleka wapi?

Mi maoni yangu naomba kwa wote walio na uelewa juu ya mambo haya naomba tuongeze juhudi za kuamsha akili za wenzetu ambazo mpaka saivi zimelala. Kwa kufanya hivyo tutaweza kulikomboa taifa letu
 
Wewe umemaliza..yaan sis ni woga sijapata ona...kuna upuuz fulan uko huku nakoishi..unakutaka uwe na vitambulisho viwili...uvilipie vyte .ss mie nilihoji kwakweli nieleweshwe..wakaniambia hv ww dada kwann kila kitu unahoji..eti jitu badala ya kunielewesha anaanza leta siasa..eti usilete siasa utamalizwa ww..eish...mie ngachoka kbs..!

On top of that watanzania tu WABINAFSI sana..yaan unajiangalia ww tu na familia yako..hatufikirii vizaz vijavyo..mie nekereka sana jaman
Usiwalaumu
watanzania wengi ni wahanga wa maisha ya kidikteta kwenye ngazi ya familia. Kumbuka mtoto umleavyo ndivyo akuavyo
 
Kwani elimu ni nini? ni upumbavu wetu tu na wala si elimu,fuatilia kinachoendelea Malawi kwa sasa,,wamalawi wanaelimu kutuzidi?Wamalawi walio wengi ni maskini kuliko sisi ila wanaipenda nchi yao.sisi hatujipendi wenyewe wala kuipenda nchi yetu na zaidi sisi ni wapumbavu,mfano Jeshi letu JWTZ au police wetu kufungamana na chama tawala au kudanganyana kwamba chama tawala au serikali ndo inawalipa mshahara nao ni kwa sababu hawana elimu?au ni upumbavu tu?
Mkuu ni kwamba upumbavu ni zao la kutokuwa na maarifa. Maarifa yanakusaidia ujitambue kwa kiasi kikubwa sana. Ukikiosa maarifa hakika ndipo suala la ujinga na upumbavu huwa linakuja. Pindi utakapokuwa mjinga/mpumbavu hakika utashindwa kuhoji hata pale unapoona mambo hayaendi sawa kwa sababu ujinga na upumbuvu huambatana na uoga.
 
Back
Top Bottom