Chaguo la Mungu mwaka 2010 huyu hapa

Watanzania

JF-Expert Member
Jul 7, 2009
727
42
Ni wakati sahihi kwetu watanzania kujichagulia wenyewe chaguo la Mungu na si kuchaguliwa na wachache. Tumepata fundisho kuwa aliyedhaniwa kuwa chaguo la Mungu 2005 kumbe hakuwa. Si chaguo la Mungu kwa vile hasikii kilio cha watanzania walio wengi, haachani na mafisadi na haashi safari nyingi za nje kana kwamba maendeleo yetu yataletwa kwa safari zake. Rais wetu wa sasa afike mahali atambue kwamba nadharia ya maendeleo ya misaada imepitwa na wakati. Sayansi imekataa kuwa misaada kutoka nje inaleta maendeleo ya nchi.

Hatukupata chaguo la Mungu mwaka 2005 kwa vile tuliangalia sura ya mtu, tulisikiliza maneno matupu ya mgombea, hatukutafuta historia ya Mgombea, tulidanganywa na watu wachache kuwa tuna chaguo la Mungu kumbe la. Sasa nani changu la Mungu mwaka huu 2010. Ni huyu hapa:

1. Aliyethibitika wazi si kwa hisia kuwa amelinda maliasili ya nchi- Maliasili
2. Aliyethibitika wazi si kwa hisia kuleta maendeleo ya nchi yetu kwa ujumla wake
si kuiba huku na kupeleke kwa wapiga kura-
Maendeleo ya kweli
3. Aliyethibitika kuwa hakuiba pesa za Watanzania ili kununua uongozi-
Si mtoa
rushwa wala hakutumia pesa za wizi
4. Aliyethibitika wazi si kwa hisia kuwa ametetea katiba ya nchi yetu-
Katiba
5. Alitethibitika wazi kuwa anaipenda nchi yetu si kuleta wezi Tanzania kwa jina la
wawekezaji-
Mpenda nchi
6. Aliyethibitika wazi kuwa ana dira sahihi ya elimu- si ubabaishaji wa maboma ya
shule za kata-
Elimu bora
7. Aliyethibitika wazi kuwa anajali utu wa Watanzania si muigizaji huku anaenda
safari akiacha watanzania wakilipukiwa na mabomu, wakifukiwa na milima,
wakisombwa na mafuriko, wakifa njaa-
Anayejali utu si msanii
 
Na wale watanzania wasioamini Mungu, wao inakuwaje?

Nimeipenda hii sentensi yako

''tulisikiliza maneno matupu ya mgombea, hatukutafuta historia ya Mgombea''

aibu ya vizazi kwa CCM !
 
Dk.Slaa anafaulu katika vigezo vyote saba ulivyoweka hapo juu..kwa mtazamo wangu.
 
Dk.Slaa anafaulu katika vigezo vyote saba ulivyoweka hapo juu..kwa mtazamo wangu.

nani, slaa, thubutu........................ ni JK kwa kwenda mbele................. rekodi yake ya utendaji inajieleza..................... napendekeza mgombea mwenza awe sophia simba ili amshauri kwa karib zaidi kuhusu uharaka wa kuchukua hatua inapolazimu kufanya maamuzi magumu................................
 
Mkuu sema chaguo letu! linakuwa la mungu pale tunapolichagua sisi
kwa hiyo la akili kichwani ni SS??!! au
 
nani, slaa, thubutu........................ ni JK kwa kwenda mbele................. rekodi yake ya utendaji inajieleza..................... napendekeza mgombea mwenza awe sophia simba ili amshauri kwa karib zaidi kuhusu uharaka wa kuchukua hatua inapolazimu kufanya maamuzi magumu................................

Onyesha hapa ni kwa namna gani huyo unayempigia upatu anakidhi kigezo kimoja baada ya kingine. Thibitisha kwa hakika bila kuleta hisia.
 
Slaa si chaguo la mungu bali ana uelekeo mzuri wa kutufikisha tunapotaka. Naamini tukimpa tunaweza kumshuhudia Mkapa kizimbani. Atakayeweza kumfikisha Mkapa,Edrew Chenge, Edward Luasa, Kalamagi, Lostam, Edward Hosea ndilo litakuwa chaguo la Mungu .Vinginevyo halitokuwapo kabisa.
 
Hakuna chaguo la MUNGU katika kizazi hiki cha nyoka...wote wanachaguliwa na wanadamu,hata hao viongozi wa dini wenyewe hawachaguliwi na MUNGU sembuse kwenye siasa.
 
Alitethibitika wazi kuwa anaipenda nchi yetu si kuleta wezi Tanzania kwa jina la
wawekezaji- Mpenda nchi

Ok. Hata chaguo la "Mungu" tuliyo naye saaivi ni mpenda "uchi" pia (kama ule wa "dokta" Kigoda...)
 
Slaa si chaguo la mungu bali ana uelekeo mzuri wa kutufikisha tunapotaka. Naamini tukimpa tunaweza kumshuhudia Mkapa kizimbani. Atakayeweza kumfikisha Mkapa,Edrew Chenge, Edward Luasa, Kalamagi, Lostam, Edward Hosea ndilo litakuwa chaguo la Mungu .Vinginevyo halitokuwapo kabisa.

Mkuu lazima ujue kuwa kama akimaliza kazi hiyo basi aondoke madarakani. Kama kweli mtu akiingia madarakani kwa ajili hiyo tu, akimaliza hiyo atafanya nini? au ndio ataanza kusafiri kila siku kwenda nje.

Kingozi amabaye ni chaguo la Mungu huwa anafanya yale ambayo mungu atanataka, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kondoo wake wanapata malisho ya kutosha. Huyo ndio tunayemtaka, so far hatuna.
 
Ok. Hata chaguo la "Mungu" tuliyo naye saaivi ni mpenda "uchi" pia (kama ule wa "dokta" Kigoda...)

Swali lako ni zuri sana, na la pekee kabisa yafaa ukilipost kwenye thread inayojitegemea ili kuwe na mtiririko mzuri wa mawazo kuhusu Mungu ni nani, asili yake, tabia yake, n.k.
 
Ukiwa na mambo yafuatayo unashinda:

1. Chama kinachokubalika na wapiga kura wengi.
2. Ndani ya chama hicho wewe unakubalika na wengi.
3. Fedha ya kutosha kupiga kampeni rasmi na zisizo rasmi
4. Upepo.

Haya manne yanatosha kuchaguliwa kuwa Rais wetu 2010. Ukishachaguliwa hata bila yoote yaliyoandikwa sijui maliasili, sijui ukaribu na wananchi, tayari wewe ni chaguo la Mungu. Kwa sababu usingeweza kuchaguliwa bila kuwa chaguo la Mungu.

CCM wanalijua hili na ndiyo maana mgombea wa CCM ndiye atakayeshinda uchaguzi 2010, kwa hiyo mgombea wa CCM ndiye chaguo la Mungu. Hii ndiyo Tanzania leo.

Kwa wale mnaotaka kula miaka mitano ijayo ya uongozi, jipendekezeni mapema CCM, acheni longolongo na migogoro ya kijinga ooh ufisadi ooh BOT, vinginevyo umri unakwenda huo hamna mali, hamna chochote. Acheni kusubiri mkono udondoke kama fisi.

Msiwe wajinga, Kikwete atashinda uchaguzi huu hata Dr Slaa analijua hilo, siyo siri, sasa jipendekezeni mapema ili mfaidi matunda ya uhuru, acheni kusuasua, mtakufa maskini.

Chadema msitumie ruzuku yenu kugombea urais kwa nguvu, mtapoteza hela bure, tumieni fedha yenu kugombea ubunge, Urais mwachieni Kikwete. Hamtamweza Kikwete nyinyi, Kikwete ni chaguo la Mungu. Kama mnabisha subirini muone.
 
Back
Top Bottom