Sami Omary Khamis
Member
- Sep 8, 2020
- 67
- 133
Ni uchaguzi rahisi kwa CCM, uchaguzi mwepesi kuwahi kutokea katika historia ya nchi hii. Ni uchaguzi wa mafanikio ya CCM dhidi ya ahadi za Wapinzani.
CCM inakwenda ktk uchaguzi huu kuonesha mafanikio iliyoyafanya kwa miaka mitano iliyopita (ambayo kimsingi ni mengi) wakati wapinzani wanakwenda kutoa ahadi.
Kwa asili ya watu ni rahisi kuchagua kitu kinachoonekana kuliko ahadi tupu.
Hapa CCM inayo nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi huu kuwa kuwa inakwenda kuonesha matokeo ya uongozi wake.
Watu wenye kumbukumbu sawa watakubaliana nami kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni uchaguzi ambao Chama tawala kinakwenda kushinda kwa kishindo. Sababu kubwa za ushindi huo wa kishindo ni hizi zifuatazo;
1. Utekelezaji wa Ilani 2015-2020.
Kwa kulinganisha awamu mbili zilizotangulia, awamu hii CCM imetekeleza kwa vitendo na kwa kiwango kikubwa zaidi Ilani yake ya Uchaguzi 2015-2020. CCM imetenda mambo mengi makubwa, kuyataja machache ktk makundi yake;
Serikali ya CCM imeboresha miundombinu ya ardhini (barabara, madaraja na reli) kwa kiwango cha juu kupita wakati wote.
Imejenga barabara za juu na baharini kwa kiwango cha juu kupita wakati wowote katika historia ya nchi hii. Barabara ya juu ya Tazara, Ubungo interchange, Barabara nane Kimara -Kibaha Dsm, daraja la New Salenda (Tanzanite), daraja la Magufuli Kilombero, daraja la Furahisha Mwanza, daraja la Busisi Kigongo Mwanza nk. hii yote ni mifano ya wazi kabisa ktk eneo hili.
CCM imejenga vivuko vikubwa na vya kisasa baharini ( Kivuko cha Kilwa), ziwa Victoria na Nyasa. Inajenga reli ya kisasa ya mwendo wa haraka, hii ni ya kwanza ktk nchi yetu.
Imeimarisha usafiri wa anga, ununuzi wa Ndege, kuboresha na kujenga viwanja vya Ndege nchini. Inajenga mradi mkubwa wa kufua umeme mwingi na wa kutosha, imeimarisha nidhamu kazini, imeboresha maslahi ya watumishi kwa kupunguza kodi katika pato halisi hivo kuongeza kiwango cha pato halisi la mtumishi (take home).
Serikali ya CCM imeongeza bajeti ya afya, elimu, maji, utawala bora, nk.
Imeimarisha mifumo ya utoaji haki kwa kuajiri nguvu kazi ktk mahakama zetu, kuboresha miundo mbinu ya mahakama na kurekebisha sheria zetu kwendana na wakatiwa sasa.
CCM imepandisha hadhi ya nchi mbele ya uso wa dunia, sasa Tanzania sio shamba la bibi kama ilivyiotafsirika awali. Tanzania sasa inaheshimika kwa watu wote, Serikali imerekebisha sheria za madini kwa manufaa ya nchi yetu.
Serikali imefanya mambo mengi makubwa kwa kipindi kifupi kuliko wakati mwingine wowote. Imetekeleza kwa kishindo, Imefanikiwa! Huu ni ushahidi kuwa awamu ya pili itafanya mambo mengi makubwa zaidi, tuichague tena CCM.
2. Skendo za Rushwa na Ufisadi.
Huu ndio uchaguzi ambao CCM inaufanya kwa mara ya kwanza katika miongo mitatu bila Serikali yake kuwa na skendo yoyote ya rushwa na ufisadi.
Maana ya jambo hili ni kuwa, kwa miaka mitano Serikali ya CCM imefanikiwa kudhibiti rushwa na ufisadi nchini. Hakuna hoja ya msingi eneo hili kama kashfa kulinganisha na chaguzi zingine. Wenye kumbukumbu watakumbuka skendo za RADA, MEREMETA, EPA, RICHMOND, KAGODA nk.
Ni kweli yote haya yametokea ktk Serikali za CCM zilizotangulia ndio maana kwa kutambua dosari hiyo awamu hii kumefanyika marekebisho makubwa ktk usimamizi wa sheria za nchi.
Huu ni ushindi mkubwa kwa CCM, ni ushindi kwa Tanzania. Ni mafanikio makubwa kwa Serikali! Serikali yenye uadilifu haipaswi kupanguliwa, ichagueni tena. Kazi kubwa iliyo mbele ya Wana-CCM nchi nzima ni kuwafahamisha watu juu ya mambo haya mazuri yaliyofanyika ili waichague tena. Huu ni uchaguzi wa mafanikio ya CCM dhidi ya ahadi za wapinzani, watu watachagua mafanikio yanayoonekana.
3. Uwajibikaji.
Imeandikwa, usiposema wewe mawe yatapaza sauti. Watu wote wanajua kuwa uwajibikaji wa Serikali kwa sasa ni wa mfano. Tanzania inajua, Afrika Mashariki inapigia mfano kwa Tanzania na Dunia inachagiza.
Serikali imesimamia kwa kiwango kikubwa uwajibikaji na nidhamu ktk ofisi za umma. CCM inakwenda katika uchaguzi huu nchi ikiwa imepunguza mizaha katika uwajibikaji. Kila mmoja anatimiza wajibu wake kama inavyomstahili, uzembe kazini na urasimu vimepungua sana. Tuichague tena CCM tumalizie kabisa mambo haya. Haya ni mafanikio ya hali ya juu kwa Chama na Serikali.
Tunakusudia kujenga nchi yenye nidhamu ya hali ya juu, yenye kuwajibika kwa ajili ya maendeleo ya watu. Tanzania inapaswa kusonga mbele zaidi ya ilivyo sasa, ni uchaguzi wa mafanikio dhidi ya ahadi. CCM inaeleza mafanikio, wengine wanaeleza ahadi. ChagueniMafanikio,#ChaguaCCMOctoba28.
#MitanoTena!
MenukaJr.
CCM inakwenda ktk uchaguzi huu kuonesha mafanikio iliyoyafanya kwa miaka mitano iliyopita (ambayo kimsingi ni mengi) wakati wapinzani wanakwenda kutoa ahadi.
Kwa asili ya watu ni rahisi kuchagua kitu kinachoonekana kuliko ahadi tupu.
Hapa CCM inayo nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi huu kuwa kuwa inakwenda kuonesha matokeo ya uongozi wake.
Watu wenye kumbukumbu sawa watakubaliana nami kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni uchaguzi ambao Chama tawala kinakwenda kushinda kwa kishindo. Sababu kubwa za ushindi huo wa kishindo ni hizi zifuatazo;
1. Utekelezaji wa Ilani 2015-2020.
Kwa kulinganisha awamu mbili zilizotangulia, awamu hii CCM imetekeleza kwa vitendo na kwa kiwango kikubwa zaidi Ilani yake ya Uchaguzi 2015-2020. CCM imetenda mambo mengi makubwa, kuyataja machache ktk makundi yake;
Serikali ya CCM imeboresha miundombinu ya ardhini (barabara, madaraja na reli) kwa kiwango cha juu kupita wakati wote.
Imejenga barabara za juu na baharini kwa kiwango cha juu kupita wakati wowote katika historia ya nchi hii. Barabara ya juu ya Tazara, Ubungo interchange, Barabara nane Kimara -Kibaha Dsm, daraja la New Salenda (Tanzanite), daraja la Magufuli Kilombero, daraja la Furahisha Mwanza, daraja la Busisi Kigongo Mwanza nk. hii yote ni mifano ya wazi kabisa ktk eneo hili.
CCM imejenga vivuko vikubwa na vya kisasa baharini ( Kivuko cha Kilwa), ziwa Victoria na Nyasa. Inajenga reli ya kisasa ya mwendo wa haraka, hii ni ya kwanza ktk nchi yetu.
Imeimarisha usafiri wa anga, ununuzi wa Ndege, kuboresha na kujenga viwanja vya Ndege nchini. Inajenga mradi mkubwa wa kufua umeme mwingi na wa kutosha, imeimarisha nidhamu kazini, imeboresha maslahi ya watumishi kwa kupunguza kodi katika pato halisi hivo kuongeza kiwango cha pato halisi la mtumishi (take home).
Serikali ya CCM imeongeza bajeti ya afya, elimu, maji, utawala bora, nk.
Imeimarisha mifumo ya utoaji haki kwa kuajiri nguvu kazi ktk mahakama zetu, kuboresha miundo mbinu ya mahakama na kurekebisha sheria zetu kwendana na wakatiwa sasa.
CCM imepandisha hadhi ya nchi mbele ya uso wa dunia, sasa Tanzania sio shamba la bibi kama ilivyiotafsirika awali. Tanzania sasa inaheshimika kwa watu wote, Serikali imerekebisha sheria za madini kwa manufaa ya nchi yetu.
Serikali imefanya mambo mengi makubwa kwa kipindi kifupi kuliko wakati mwingine wowote. Imetekeleza kwa kishindo, Imefanikiwa! Huu ni ushahidi kuwa awamu ya pili itafanya mambo mengi makubwa zaidi, tuichague tena CCM.
2. Skendo za Rushwa na Ufisadi.
Huu ndio uchaguzi ambao CCM inaufanya kwa mara ya kwanza katika miongo mitatu bila Serikali yake kuwa na skendo yoyote ya rushwa na ufisadi.
Maana ya jambo hili ni kuwa, kwa miaka mitano Serikali ya CCM imefanikiwa kudhibiti rushwa na ufisadi nchini. Hakuna hoja ya msingi eneo hili kama kashfa kulinganisha na chaguzi zingine. Wenye kumbukumbu watakumbuka skendo za RADA, MEREMETA, EPA, RICHMOND, KAGODA nk.
Ni kweli yote haya yametokea ktk Serikali za CCM zilizotangulia ndio maana kwa kutambua dosari hiyo awamu hii kumefanyika marekebisho makubwa ktk usimamizi wa sheria za nchi.
Huu ni ushindi mkubwa kwa CCM, ni ushindi kwa Tanzania. Ni mafanikio makubwa kwa Serikali! Serikali yenye uadilifu haipaswi kupanguliwa, ichagueni tena. Kazi kubwa iliyo mbele ya Wana-CCM nchi nzima ni kuwafahamisha watu juu ya mambo haya mazuri yaliyofanyika ili waichague tena. Huu ni uchaguzi wa mafanikio ya CCM dhidi ya ahadi za wapinzani, watu watachagua mafanikio yanayoonekana.
3. Uwajibikaji.
Imeandikwa, usiposema wewe mawe yatapaza sauti. Watu wote wanajua kuwa uwajibikaji wa Serikali kwa sasa ni wa mfano. Tanzania inajua, Afrika Mashariki inapigia mfano kwa Tanzania na Dunia inachagiza.
Serikali imesimamia kwa kiwango kikubwa uwajibikaji na nidhamu ktk ofisi za umma. CCM inakwenda katika uchaguzi huu nchi ikiwa imepunguza mizaha katika uwajibikaji. Kila mmoja anatimiza wajibu wake kama inavyomstahili, uzembe kazini na urasimu vimepungua sana. Tuichague tena CCM tumalizie kabisa mambo haya. Haya ni mafanikio ya hali ya juu kwa Chama na Serikali.
Tunakusudia kujenga nchi yenye nidhamu ya hali ya juu, yenye kuwajibika kwa ajili ya maendeleo ya watu. Tanzania inapaswa kusonga mbele zaidi ya ilivyo sasa, ni uchaguzi wa mafanikio dhidi ya ahadi. CCM inaeleza mafanikio, wengine wanaeleza ahadi. ChagueniMafanikio,#ChaguaCCMOctoba28.
#MitanoTena!
MenukaJr.