security guard
JF-Expert Member
- Sep 27, 2011
- 799
- 603
Zikiwa zinahesabika siku za kufanya uchaguzi wa mwakilishi wa Jimbo la Kiembe Samaki,Chama Cha Demokrasia na Mandeleo ( CHADEMA) kimeonekana kuweweseka kwa kushindwa kumsimamisha Mgombea wao mpaka sasa .
Jimbo hilo ambalo lipo wazi baada ya Halmashauri Kuu ya CCM kumvua uanachama aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo hilo Ndugu.Mansour Yusuf Himid kwa makosa mbali mbali ikiwemo kushindwa kusimamia malengo ya CCM na kutelekeza masharti ya Uanachama,Kushindwa kutekeleza wajibu wa mwanachama na kukiuka maadili ya kiongozi wa CCM na Kuikana Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010-2015 na kuisaliti CCM.
Wakati CUF ilitaka kumsimamisha Ndugu Mansour Yusuf Himid kugombea nafasi hiyo kwa tiketi ya chama chao ,Mansour amekataa kata kata kugombea hivyo mpaka sasa wameshindwa kufanya mchakato wa kura za maoni na kumsubiri Maalim Seif atoe jina mfukoni Chadema wameshindwa kabisa na kubaki kuweweseka.
CCM kwa upande wake imeendesha mchakato vizuri na mpaka sasa katika kura za maoni mshindi alishafahamika .
Ni vikao vya juu vinatakiwa kubariki jina la Mahmoud Thabit Kombo kuwania nafasi hiyo kwa tiketi ya CCM.
"Chadema ipo kwenye wakati mgumu kiasi kama tunajidanganya hasa tunapozungumzia kukiimarisha chama kwani muelekeo umeshapotea na hatujajipanga vizuri kwa upande wa Zanzibar" alisema hayo mmoja wa viongozi wa Chadema ambaye hakutaka jina lake litajwe.
Jimbo hilo ambalo lipo wazi baada ya Halmashauri Kuu ya CCM kumvua uanachama aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo hilo Ndugu.Mansour Yusuf Himid kwa makosa mbali mbali ikiwemo kushindwa kusimamia malengo ya CCM na kutelekeza masharti ya Uanachama,Kushindwa kutekeleza wajibu wa mwanachama na kukiuka maadili ya kiongozi wa CCM na Kuikana Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010-2015 na kuisaliti CCM.
Wakati CUF ilitaka kumsimamisha Ndugu Mansour Yusuf Himid kugombea nafasi hiyo kwa tiketi ya chama chao ,Mansour amekataa kata kata kugombea hivyo mpaka sasa wameshindwa kufanya mchakato wa kura za maoni na kumsubiri Maalim Seif atoe jina mfukoni Chadema wameshindwa kabisa na kubaki kuweweseka.
CCM kwa upande wake imeendesha mchakato vizuri na mpaka sasa katika kura za maoni mshindi alishafahamika .
Ni vikao vya juu vinatakiwa kubariki jina la Mahmoud Thabit Kombo kuwania nafasi hiyo kwa tiketi ya CCM.
"Chadema ipo kwenye wakati mgumu kiasi kama tunajidanganya hasa tunapozungumzia kukiimarisha chama kwani muelekeo umeshapotea na hatujajipanga vizuri kwa upande wa Zanzibar" alisema hayo mmoja wa viongozi wa Chadema ambaye hakutaka jina lake litajwe.