Rose Mayemba
JF-Expert Member
- May 7, 2012
- 721
- 1,017
Huyu Msigwa ni mzee wa kukomaa kama wamwitavyo wananchi wake katika nchi yake, alikimaliza chama cha magamba kwa kukiita ni chama kilichojaza panya serikalini. JK na wafuasi wake wote ni panya kwa mujibu wa hotuba yake, aliidhihirishia Tz kwamba hata kusini wameamka na wanatambua wajibu wao.ZAIDI ya wanachama 1300 wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kutoka mikoa ya Simiyu, Morogoro na Njombe wamekihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Katika mkoa wa Njombe pekee, wana CCM 600 walijiunga na CHADEMA na wengine 421 kutoka mkoa wa Simiyu wakati wa ziara iliyofanywa na timu ya baadhi ya wabunge wa chama hicho.
Katika mkoa wa Njombe, licha ya kufungua matawi matatu na ofisi moja ya kata.
Huko Simiyu, wanachama waliojiunga wanatoka katika wilaya za Maswa na Meatu juzi katika mikutano tofauti ya hadhara iliyofanyika katika mji wa Nyalikungu wilayani Maswa na Mwanhuzi wilayani Meatu iliyohudhuriwa na maelfu ya wananchi.
Mikutano hiyo ilihutubiwa na wabunge, Meshack Opulukwa wa jimbo la Meatu na Slivester Kasulumbayi wa Maswa.
Ni baada ya kuhamasisha mchango kufanyika kwa dk 7 na kupatikana kwa zaidi ya mil moja. Kwa mvuto wake wa kichungaji aliwabatiza wazee 3 kwa maji matakatifu ya CHADEMA na kuwavua magamba yaliyowatesa kwa miaka mingi.
Be blessed mzee