CHADEMA yatoa ubani kwa kada wake

Mungi

JF Gold Member
Sep 23, 2010
16,975
9,566




na Andrew Chale



CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa ubani wa sh milioni moja kwa familia ya Masoud Mbwana, aliyeuawa kikatili huko Igunga wakati wa uchaguzi mdogo huku kikitaka uchunguzi wa suala hilo ushughulikiwe haraka.

Akihutubia waombolezaji nyumbani kwa marehemu Mburahati juzi jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, alisema kuwa wamepata pigo kubwa ndani ya chama kuondokewa na kada huyo kwani alikufa akisimamia haki.
“CHADEMA tumesikitishwa na kifo hiki, hivyo tumeweza kutoa rambirambi yetu kiasi cha sh milioni moja kwa familia na pia tutaendelea kushirikiana na familia katika kuhakikisha haki inapatikana na hatutaishia hapa tutaendeleza yale yote marehemu aliyoyaacha,” alisema Dk.Slaa.
Dk. Slaa aliitupia lawama idara ya usalama kuwa ndiyo inatoa mafunzo kwa vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM) maarufu kama Green Guard waliohusika katika vitendo vya vurugu huko Igunga, yakiwemo matukio ya kuwamwagia watu tindikali.
Kwa upande wa familia ya marehemu kupitia kaka mkubwa wa marehemu, Ally Matumla, aliishukuru CHADEMA na kutangaza rasmi kuwa kuanzia sasa familia yao inajiunga na chama hicho.
“Kwa niaba ya familia ya Mbwana tunashukuru kwa kila jambo na tumeamini CHADEMA si chama cha udini kama inavyovumishwa na vyama vingine, hivyo tunatumia fursa hii bila kushurutishwa, tunajiunga na CHADEMA kuanzia sasa,” alisema kaka wa marehemu.
Naye mbunge wa jimbo hilo la Ubungo, John Mnyika, alisema kuwa atahakikisha analifuatilia suala hilo akiwa kama mbunge kwa mwanachama wake huyo sambamba na kusaidiana na familia kwa hali na mali katika kipindi chote.
Kifo cha kada huyo ambaye alienda Igunga kama wakala kililipotiwa kutokea Oktoba 2 mwaka huu na mwili wake kuokotwa Agosti 9, mjini Igunga, mkoani Tabora, ukiwa umeharibika vibaya na kutobolewa macho na hivyo kulazimika kuzikwa huko.



 
Prosecution for all involved will come...it is unfortunate that it will be later than sooner because of impunity attitude of our Political Leaders.
 
Atakumbukwa kama shujaa,siku ikifika na wakati ccm aitakuwepo madarakani,Pia damu yake aimwagiki bule wale waliousika itawasulubu wakati ukifika.Alaze pema peponi mwili wa marehemu.AMENI
 
Pole kwa wafiwa na wanachadema wote,tuelewe ukombozi una gharama zake.Yatokeayo yatupe ya kuwa jasir zaid,ipo siku ukomboz utapatikana.Tumwombe Rab atupe nguvu ya kupambana na haya majambaz ya mali za umma,damu ya mwanachadema haipotei bure. Na wote walofanya ukatili huo watajulikana tu.
 
What special did he do for the party? I only started to hear about him immeditely after his demise and I can't remember his name mentioned before that.
 
What special did he do for the party? I only started to hear about him immeditely after his demise and I can't remember his name mentioned before that.
Does any party member have to report to you what he/she does for the party? What would your knowledge of what he did change if anything? How many individual names do you remember being mentioned anyway?
Regardless of his contribution to the party, the fact that he was a member is sufficient to warrant such a gesture; we recognise humanity before anything else.
 
Good move by CDM. Pole nyingi kwa familia ya mpiganaji Masoud.

Nimefurahishwa na hatua sahihi ya wanafamilia hiyo kujiunga na wapiganaji wengine wazalendo kuleta ukombozi kwa Tz, kwani ndio njia pekee ya kumuenzi ndugu yenu na mwenzetu marehemu Masoud.

Kwa trend ilivyo kuna kina Masoud wengine wengi, sasa naomba kupendekeza kuwa CDM hasa BAVICHA waangalie namna ya kuwa na siku na njia ya kuwaenzi na kuwakumbuka mashujaa waliopoteza/watakaopoteza maisha kwa ajili ya ukombozi wa nchi hii.
 
What special did he do for the party? I only started to hear about him immeditely after his demise and I can't remember his name mentioned before that.

Wewe ni nanga sana kiingereza chak.Ficha upumbavu na bora ungalikuwa mjinga ingakikuwa nafuu sana .Poleni sana wafiwa wote Mungu ni mwema daima .
 
rest in peace comrade! your struggle will be intensified to honour what you stood for. we are sad but we wont rest untill killers pay for what they did.
 
RIP Kamanda, hakika tutakukumbuka kutokana na huu uchaguzi wa Igunga uliojaa mizengwe ya akina Wasirra, NEC, Nape kupigwa marufuku kufika Igunga, wazee wengi wa CCM kushirikishwa kwenye kampeni nk.

Haki itendeke kama si leo ipo siku itatendeka tu.
 
Amekufa Kishujaa!!! Lakini ipo sababu, nia na uwezo wa kupambana na wadhalimu hawa ccm. Mungu ibariki Chadema! Mungu Ibariki Tanzania! Mungu ilazi roho ya marehemu huyu shujaa mahali pema peponi na damu yake na ya wazalendo wengine wote wanaouwawa kwa matukio mbalimbali ya namna hii chini ya itawala wa Kikwete ambaye ni matumaini yasiyokutana ya watanzania!!! ikazidishe mapambano dhidi ya udhalimu huu nje na ndani ya ccm na Tanzania, na wote tuseme, Amen!! "Emancipate yourselves from mental slavery; None but ourselves can free our minds. Have no fear for atomic energy, 'Cause none of them can stop the time. How long shall they kill our prophets, While we stand aside and look? Ooh! Some say it's just a part of it: We've got to fulfill the Book. Won't you help to sing These songs of freedom? 'Cause all I ever have:
Redemption songs, Redemption songs, Redemption songs. Emancipate yourselves from mental slavery; None but ourselves can free our mind.
Wo! Have no fear for atomic energy, 'Cause none of them-a can-a stop-a the time. How long shall they kill our prophets, While we stand aside and look? Yes, some say it's just a part of it: We've got to fulfill the book. Won't you have to sing These songs of freedom? - 'Cause all I ever had: Redemption songs - All I ever had: Redemption songs: These songs of freedom, Songs of freedom. Amen!!!!!!!!!!!!
 
What special did he do for the party? I only started to hear about him immeditely after his demise and I can't remember his name mentioned before that.

That's a very stupid question cant you see he has died in the front line! what else you want?, despite that do you know for sure who in the party or ccm or in farms doing what? for the freedom of this country? oh my God, why among us such blind people!!!!???????
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom