Elections 2010 CHADEMA yatoa tamko: Hatumtambui Kikwete kama rais

CHADEMA ina wabunge wa kuchaguliwa na kuteuliwa na wote waliapa mbele ya Spika kuwa "watatii sheria za Jamhuri ya Muungnao wa TZ";kwa kiapo hicho si ni wazi basi wametambua na wametii mamlaka tatu za dola ambazo ni Rais,Bunge na Mahakama au mimi ndiyo sipo sahihi?Je ina maana sasa Wabunge wa CHADEMA hawatachukua posho na mishahara itolewayo na serikali inayoongozwa na Rais wasiyemtambua?Au hawamtambui tu Rais lkn wanazitambua posho na mishahara inayotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu-mamlaka ya Bunge?

Kama tunakumbuka vyema kule ZNZ baada ya uchaguzi wa mwaka 1995 chama cha CUF kilisusia matokeo na hakikumtambua Rais Salmin kama Rais halali wa ZNZ kulikopeleka uongozi wa juu wa CUF kuwapiga marufuku Wawakilishi na Wabunge wa CUF kuingia barazani;tamko la CUF lilikuwa na nguvu miongoni mwa watu kwani hakuna Mbunge wake aliyeapa kuiheshimu serikali wala hakuna aliyepokea hata senti toka Barazani kama posho ya kuhudhuria vikao na baadae wakavuliwa nyadhifa zao za kuchaguliwa!

Tuanze maandalizi sasa ya kuiondoa CCM mwaka 2015 na huku tukikazania kwenye mabadiliko ya kikatiba hasa hiki kipengele kisemacho NEC ikitangaza matokeo hayapingwi popote pale.Siku za kuwepo madarakani CCM zinahesabika na hili sakata la Spika ni ongezeko lingine la kura wa wapinzani mwaka 2015.

Mimi nimeanza tayari maandalizi ya kuichukua Kyela yetu inayozidi kudorora,mwanzoni tu mwakani nitawaita waandishi wa habari na wana JF waje kijijini kwangu Talatala-Kyela waione 'manifesto'yangu kuhusu 'take back our Kyela'!
 
Sawa,

Lakini kama alivyokuuliza William hapo juu, wananchi wanafanya nini? Wanaandamana? Na kama hawaandamani CHADEMA watasemje kwamba Kikwete ni mwizi wa kura ambaye wananchi hawamtaki? Tutajuaje kama CHADEMA si walalmishi tu wsiokubali kushindwa?

Natetea mabadiliko ya katiba ili haya mambo yote yawe addressed formally kisheria, sio kwa ulalamishi ambao hauwezi hata kuwa proven.

Tubadilishe katiba, NEC isiwe inachaguliwa na rais, rais asiwe sehemu ya bunge -tayari Waziri Mkuu anaiwakilisha serikali bungeni- then katika situation kama hii wbunge wa CHADEMA na CUF na wangeweza kuendelea kuwa wabunge bila kumtambua rais.

Lakini sasa hivi kukubali ubunge ni kumtambua rais.

Ama sivyo wabunge wajaribu kumpigia rais kura ya no confidence, bunge liwe dissolved na chaguzi zote a ubunge na urais zirudiwe.

Kama wana huo moyo na wanaweza kupata support ya CCM.

Ninakubaliana na wewe kuwa Katiba inatakiwa kubadilishwa. Nikwambie kuwa watawala wa sasa wananufaika na katiba kama ilivyo. Hawatakubali katiba ibadilishwe. Njia pekee ya kuibadilisha katiba ni wananchi kuiamuru serikali kupanga utaratibu wa kuibadilisha. Na hapa napo serikali itataka kujitutumua kuonyesha kuwa ipo juu ya wananchi, wakati ni kinyume chake. Kubadilisha katiba kutafanikiwa tu ikiwa wananchi kwanza wataonyesha kumkataa rais aliyewaibia kura, halafu kuilazimisha serikali kubadilisha katiba wakati huo huo. Chadema wanafanya kazi ya wananchi, wanawakilisha wananchi kwa sababu wameshaonyesha kuwa kura zao zinaibiwa ndiyo maana watu walilala vituoni mpaka siku mbili kuzilinda. Kwa hiyo mambo mawili yafanyike kwa pamoja, yaani wananchi kumkataa rais aliyechaguliwa kwa kuiba kura na wakati huo huo kuilazimisha serikali iliyoingia kwa wizi wa kura ibadilishe katiba. Kuandamana wananchi kunahitajika kuratibiwa, na ndiyo maana wapiga kura wanasubiri Chadema waratibu kazi ya kumkataa rais aliyechaguliwa kwa wizi wa kura
 
Tatizo la katiba kwa sababu katiba inampa nguvu rais kama mungumtu, rais anateua kuanzia wabunge, majaji mpaka mawaziri.Kwa maana nyingine mihimili mitatu hii inatakiwa kuweka checks and balances, lakini rais ndiye anayeisimamisha, sasa checks and balances zitatoka wapi?

Rais huyo huyo ni sehemu ya bunge.

Rais huyo huyo practically yuko juu ya sheria.

Rais huyo huyo akitaka kumfunga mtu yeyote bila maelezo yoyote kwa kipindi chochote anachotaka kama rais anaweza.

Rai huyo huyo akitaka kuchukua ardhi yoyote ya Jamhuri, na kuitumia kwa sababu zozote anazotaka yeye anaruhusiwa kisheria.

Wewe unaona katiba sawa hii?

- Well, ninakubali kwamba katiba yetu ina mapungufu sana, lakini hapa tungejaribu kuonyesha mapungufu ya katiba na matokeo ya uchaguzi ya sasa, je ni kweli matatizo ya NEC kwenye huu uchaguzi yanalalia mapungufu ya katiba? Maana mimi nina wasi wasi sana na matatizo ya kiufundi na utaalamu zaidi na hasa incompetence ya viongozi wake!

- Otherwise, Rais anatakiwa kuchagua mawaziri na majaji, kinachokosekana katika katiba yetu ni approval ya bunge ambayo hata hivyo watapitishwa tu na majority yaani CCM wale wale, tuzidishe nguvu ya kuvijenga vyama vya siasa ili siku moja tuwe na upinzani wa kweli bungeni, tufike siku Spika atoke Upinzani na watawala wengine, otherwise tutabadili mvinyo ule ule tu toka chupa ya zamani hadi mpya,

- Kama matatizo ya NEC ni ya kikatiba tuyachambue hapa moja hadi la mwisho!


William
 
Ninakubaliana na wewe kuwa Katiba inatakiwa kubadilishwa. Nikwambie kuwa watawala wa sasa wananufaika na katiba kama ilivyo. Hawatakubali katiba ibadilishwe. Njia pekee ya kuibadilisha katiba ni wananchi kuiamuru serikali kupanga utaratibu wa kuibadilisha. Na hapa napo serikali itataka kujitutumua kuonyesha kuwa ipo juu ya wananchi, wakati ni kinyume chake. Kubadilisha katiba kutafanikiwa tu ikiwa wananchi kwanza wataonyesha kumkataa rais aliyewaibia kura, halafu kuilazimisha serikali kubadilisha katiba wakati huo huo. Chadema wanafanya kazi ya wananchi, wanawakilisha wananchi kwa sababu wameshaonyesha kuwa kura zao zinaibiwa ndiyo maana watu walilala vituoni mpaka siku mbili kuzilinda. Kwa hiyo mambo mawili yafanyike kwa pamoja, yaani wananchi kumkataa rais aliyechaguliwa kwa kuiba kura na wakati huo huo kuilazimisha serikali iliyoingia kwa wizi wa kura ibadilishe katiba. Kuandamana wananchi kunahitajika kuratibiwa, na ndiyo maana wapiga kura wanasubiri Chadema waratibu kazi ya kumkataa rais aliyechaguliwa kwa wizi wa kura

Sawa kabisa,

CHADEMA inaweza kuwahamasisha wananchi kwa hili? Mbona inaonekana kama baada ya uchaguzi wananchi washapoa ?

Better yet, wananchi wenyewe wanataka kufanya nini sasa hivi?
 
Ninakubaliana na wewe kuwa Katiba inatakiwa kubadilishwa. Nikwambie kuwa watawala wa sasa wananufaika na katiba kama ilivyo. Hawatakubali katiba ibadilishwe. Njia pekee ya kuibadilisha katiba ni wananchi kuiamuru serikali kupanga utaratibu wa kuibadilisha. Na hapa napo serikali itataka kujitutumua kuonyesha kuwa ipo juu ya wananchi, wakati ni kinyume chake. Kubadilisha katiba kutafanikiwa tu ikiwa wananchi kwanza wataonyesha kumkataa rais aliyewaibia kura, halafu kuilazimisha serikali kubadilisha katiba wakati huo huo. Chadema wanafanya kazi ya wananchi, wanawakilisha wananchi kwa sababu wameshaonyesha kuwa kura zao zinaibiwa ndiyo maana watu walilala vituoni mpaka siku mbili kuzilinda. Kwa hiyo mambo mawili yafanyike kwa pamoja, yaani wananchi kumkataa rais aliyechaguliwa kwa kuiba kura na wakati huo huo kuilazimisha serikali iliyoingia kwa wizi wa kura ibadilishe katiba. Kuandamana wananchi kunahitajika kuratibiwa, na ndiyo maana wapiga kura wanasubiri Chadema waratibu kazi ya kumkataa rais aliyechaguliwa kwa wizi wa kura

- Lakini mkuu hawa wananchi si walikuwa wanalinda kura za wabunge waliowapigia kura, maana hatukusikia wananchi wakidai hawaondoki mpaka kura za Rais zimetangazwa, wabunge 22 hawakipi Chama chochote cha siasa Tanzania, mandate ya kuwakilisha wananchi 45 Millioni, please!

- Mkuu hoja zako nyingi ni nzito sana lakini kwenye the heart of the argument ya Chadema wanamuwakilisha nani na wanapigania nini! on this ishu ya kutomtambua Rais zinapwaya kidogo!


William
 
- Well, ninakubali kwamba katiba yetu ina mapungufu sana, lakini hapa tungejaribu kuonyesha mapungufu ya katiba na matokeo ya uchaguzi ya sasa, je ni kweli matatizo ya NEC kwenye huu uchaguzi yanalalia mapungufu ya katiba? Maana mimi nina wasi wasi sana na matatizo ya kiufundi na utaalamu zaidi na hasa incompetence ya viongozi wake!

- Otherwise, Rais anatakiwa kuchagua mawaziri na majaji, kinachokosekana katika katiba yetu ni approval ya bunge ambayo hata hivyo watapitishwa tu na majority yaani CCM wale wale, tuzidishe nguvu ya kuvijenga vyama vya siasa ili siku moja tuwe na upinzani wa kweli bungeni, tufike siku Spika atoke Upinzani na watawala wengine, otherwise tutabadili mvinyo ule ule tu toka chupa ya zamani hadi mpya,

- Kama matatizo ya NEC ni ya kikatiba tuyachambue hapa moja hadi la mwisho!


William

Ukishakubali katiba ina mapungufu, na kwamba kwa mfano mwenyekiti wa NEC kuteuliwa na rais si sawa, tayari ushawekea shaka uhalali wa matokeo kabla hata kura hazijapigwa. Huwezi kumchagua refa halafu ukasema ushindi ni halali.

Ukisema rais anatakiwa kuchagua majaji wabunge na mawaziri unaondoa maana yote ya checks and balances. Rais hawezi kuwa na say kubwa katika mihimili yote halafu tukabaki na checks and balances.
 
Sawa kabisa,

CHADEMA inaweza kuwahamasisha wananchi kwa hili? Mbona inaonekana kama baada ya uchaguzi wananchi washapoa ?

Better yet, wananchi wenyewe wanataka kufanya nini sasa hivi?

Nafikiri waliopoa ni Chadema, wananchi wanataka waendelee kumzomea hadharani aliyeiba kura na njia mojawapo ni ya kutomtambua kama rais. Pia kama nilivyokubaliana na wewe katiba pia ibadilishwe. Kwa leo naishia hapa.
 
Nafikiri waliopoa ni Chadema, wananchi wanataka waendelee kumzomea hadharani aliyeiba kura na njia mojawapo ni ya kutomtambua kama rais. Pia kama nilivyokubaliana na wewe katiba pia ibadilishwe. Kwa leo naishia hapa.

Kuzomea hakutoshi, unataka kumpa mtu sababu ya kutumia FFU. Tuambie kuhusu legal strategy ya kubadili katiba.
 
Better yet, wananchi wenyewe wanataka kufanya nini sasa hivi?

CHADEMA na upinzani kwa ujumla walionyesha udhaifu mkubwa kwenye chaguzi ya mwaka huu hasa kwenye vitu hivi 2;

Mosi,kutoweka wagombea kwenye baadhi ya majimbo ya uchaguzi ilikuwa ni kosa kubwa sana maana una mpa nguvu CCM atumie wale waliopita bila kupingwa kuongeza nguvu za kampeni kwenye majimbo yenye nguvu kwa wapinzani;kwa mfano Mbunge wa Simanjro Mzee Sendeka kwa sababu hakuwa na mpinzani jimboni akawa anakuja Arusha mjini kumpigia kampeni Mama Batilda!

Pili,CHADEMA na baadhi ya vyama vya upinzani hawaku-screen na wala hawakuwa na established candidates kwenye majimbo mengi na kupelekea kwa baadhi yao kujitoa au kutorudisha fomu kabisa,kwa maoni yangu upinzani lzm wawe na established candidates miaka mingi kabla ya uchaguzi mkuu;kwa mfano kule Nkenge mgombea mwenye nguvu wa CHADEMA alijitoa bila sababu za msingi zinazonuka rushwa na kule Musoma Vijijini wapinzani wote hawakurudisha fomu kumpinga mwanasheria Mkono!

Kwa sasa wananchi na viongozi wa upinzani ni kujipanga upya kwa uchaguzi mkuu ujao,kwa kushirikiana na viongozi wananchi wa eneo husika waanze leo kutafuta established candidates na wapate kila jimbo mtu competitive;bila long term preparation itakuwa ni kuota ndoto huku unatembea kuiondoa CCM madarakani!
 
Kwa mtazamo wangu, walichofanya viongozi wa CHADEMA jana si kitu kingene ila ni kushusha uzito wa maana ya kutokumtambua Rais, kwa sababu zifuatazo:

1. Kutomtambua Rais wamekutangaza katika sherehe yao ya kujipongeza huku wakiwa na vinywaji "changamfu" mezani. Swala zito kama hili lilipaswa kuelezwa katika mazingira maalum yaliyoandaliwa kwa ajili ya Taifa kupokea ujumbe huu mzito.

2.Unapotangazwa swala nyeti kama kutokumtambua Rais, unawajibika kutoa mwongozo kwa wale wataokubaliana na maamuzi hayo. je, wanachama baada ya kukataa matokeo wameelekezwa kufanya nini? au wameachwa waamue wenyewe cha kufanya? am sorry to say this is irresponsible behaviour. Ukipita mitaa ya Manzese ukamuita mtu mwiiiiizi huuuuyo, unategemea nini?jekama viongozi wa CHADEMA wako radhi kuwaacha wananchi waamue wenyewe katika swala nyeti kama hili, uongozi wao uko wapi?

3. Baada ya muda mrefu wa kimya ambacho kiliezewa kuwa ni kwa vile viongozi "wanakusanya data", statement inayotoka ndio hii ambayo haiambatani na data yoyote. Huu ni utani jamani toka kwa viongozi hawa wa CHADEMA!
 
Ukishakubali katiba ina mapungufu, na kwamba kwa mfano mwenyekiti wa NEC kuteuliwa na rais si sawa, tayari ushawekea shaka uhalali wa matokeo kabla hata kura hazijapigwa. Huwezi kumchagua refa halafu ukasema ushindi ni halali.

Ukisema rais anatakiwa kuchagua majaji wabunge na mawaziri unaondoa maana yote ya checks and balances. Rais hawezi kuwa na say kubwa katika mihimili yote halafu tukabaki na checks and balances.

- Rais kuchagua wabunge kumi as it pleases him, ni moja ya mapungufu ya katiba yetu ingawa in the process huwa anachagua na wabunge wa upinzani, Rais kumchagua anybody mimi sioni tatizo la kikatiba tatizo ni aliyechaguliwa kupata approval ya wananchi yaani bunge, unless kuna model nyingine unaijua ambayo inaweza kuwa ni the answer to the this question, maana nchi zote zilizoendelea ninamini wanatumia model hiyo hiyo, the winner takes all lakini viongozi wakuu wote wa serikali huteuliwa na Rais na kupitishwa na bunge!

- Na siku zote majority ya bunge ikiwa ni chama cha Rais anayetawala ni yale yale tu hata awe vipi mteuliwa atapita tu, checks and balance tunayo sana ingawa ina mapungufu, lakini ukweli ni kwamba uoga wetu ndio umeishia kumfanya Rais wetu awe na nguvu za ajabu sana!


William.
 
Kipenzi chako? ni padri huyo soma thread ya habari mchanganyiko kuwahusu watu hao, na Tz wameanza

acha udini wewe ,,kama huna cha kuongea basi piga kimya.udini na ulafi wako wa madaraka haukupeleki kokote zaidi ya kugalagaza P lako tu wewe na dokta wako feki.
 
Wakaongezea ata kama mmoja wao atateuliwa kuwa waziri hawako tayari kuchangamana na serikali ya uchakachuaji according to Mbowe

Hakuna kitu kama waziri kuteuliwa kutoka CHADEMA hapo tunajidanganya!
 
- Rais kuchagua wabunge kumi as it pleases him, ni moja ya mapungufu ya katiba yetu ingawa in the process huwa anachagua na wabunge wa upinzani, Rais kumchagua anybody mimi sioni tatizo la kikatiba tatizo ni aliyechaguliwa kupata approval ya wananchi yaani bunge, unless kuna model nyingine unaijua ambayo inaweza kuwa ni the answer to the this question, maana nchi zote zilizoendelea ninamini wanatumia model hiyo hiyo, the winner takes all lakini viongozi wakuu wote wa serikali huteuliwa na Rais na kupitishwa na bunge!

- Na siku zote majority ya bunge ikiwa ni chama cha Rais anayetawala ni yale yale tu hata awe vipi mteuliwa atapita tu, checks and balance tunayo sana ingawa ina mapungufu, lakini ukweli ni kwamba uoga wetu ndio umeishia kumfanya Rais wetu awe na nguvu za ajabu sana!


William.
mheshimiwa William nakubaliana na wewe kwenye hichi kipengere kuwa uwoga wetu ndio umemfanya rais awe na nguvu za ajabu,ila nina uhakika kutokana na makovu ambayo tunayo sasa hivi huu woga ushatutoka na kitaeleweka kama Mungu akipenda
 
There is a clear line in the Constitution (74(12)) which forbids any legal actions on this. I quote the constitution:

74(12) "Hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya
kuchunguza jambo lolote lililotendwa na Tume ya Uchaguzi katika
kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
(13) Katika utekelezaji wa madaraka yake kwa mujibu wa katiba hii"

This is the so called "inconvenient truth" - katiba imetufunga mikono!

Kwa kuongezea...41 (7)

"Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi
kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi
hakuna Mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya
kuchunguza kuchaguliwa kwake."


KWA HIYO SUALA LA KWENDA MAHAKAMANI ITAKUWA NI KUPOTEZA MUDA!
 
Kwa mtazamo wangu, walichofanya viongozi wa CHADEMA jana si kitu kingene ila ni kushusha uzito wa maana ya kutokumtambua Rais, kwa sababu zifuatazo:

1. Kutomtambua Rais wamekutangaza katika sherehe yao ya kujipongeza huku wakiwa na vinywaji "changamfu" mezani. Swala zito kama hili lilipaswa kuelezwa katika mazingira maalum yaliyoandaliwa kwa ajili ya Taifa kupokea ujumbe huu mzito.

2.Unapotangazwa swala nyeti kama kutokumtambua Rais, unawajibika kutoa mwongozo kwa wale wataokubaliana na maamuzi hayo. je, wanachama baada ya kukataa matokeo wameelekezwa kufanya nini? au wameachwa waamue wenyewe cha kufanya? am sorry to say this is irresponsible behaviour. Ukipita mitaa ya Manzese ukamuita mtu mwiiiiizi huuuuyo, unategemea nini?jekama viongozi wa CHADEMA wako radhi kuwaacha wananchi waamue wenyewe katika swala nyeti kama hili, uongozi wao uko wapi?

3. Baada ya muda mrefu wa kimya ambacho kiliezewa kuwa ni kwa vile viongozi "wanakusanya data", statement inayotoka ndio hii ambayo haiambatani na data yoyote. Huu ni utani jamani toka kwa viongozi hawa wa CHADEMA!

Mazee hawa CHADEMA wanahitaji watu kama wewe zaidi. Huwezi kutangaza kutomtambua rais huku unasherehekea ushindi wa wabunge, kusheherekea ushindi wa wabunge ni kumtambua rais kwa minajili ya kulitambua bunge ni kumtambua rais kama nilivyosema hapo juu.

Halafu wengine wanaweza kujiuliza kutomtambua huku rais kumetoka katika vichwa vikiwa sober au watu walizidisha champagne tu wakaamua kusema chochote kilichowajia kichwani? I might be joking a bit on this, lakini kama mkuu ZeMarcopolo alivyosema, hii ni statement ya kuitiwa press conference ya nguvu, watu wakatoa official statement, mkakati, the way forward, legal strategy with hunger strike options, maandamano, mikutano ya hadhara etc.

Sio mnakunywa champagne huku mnajipongeza kuingia bunge ambalo sehemu yake ni huyo huyo rais halafu mnasema hamumtambui rais.
 
This is the so called "inconvenient truth" - katiba imetufunga mikono!

Kwa kuongezea...41 (7)

"Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi
kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi
hakuna Mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya
kuchunguza kuchaguliwa kwake."


KWA HIYO SUALA LA KWENDA MAHAKAMANI ITAKUWA NI KUPOTEZA MUDA!

Hii part ya katiba mimi sina matatizo nayo, kwa sababu essentially unaipa Tume mamlaka ya mwisho. Ni sawa na kusema katika mpira refarii ndiye muamuzi wa mwisho, you need someone kuwa muamuzi wa mwisho ama sivyo utakuwa na chaos kila siku.

Sina tatizo na hii part ya katiba, kwa sababu kama si hivyo kila mtu atakayeshindwa urais ataenda mahakamani, halafu urais utakuwa a joke, utakuwa paralysed. This is not the way to go.

Tatizo langu mimi si kwamba refarii ndiye muamuzi wa mwisho, tatizo langu ni kwamba timu moja inachagua refarii. Rais anachagua Tume ya uchaguzi, hapa ndipo nilipo na tatizo napo. Kama tungekuwa na tume iliyo impartial hata kusingekuwa na issue.
 
Hii part ya katiba mimi sina matatizo nayo, kwa sababu essentially unaipa Tume mamlaka ya mwisho. Ni sawa na kusema katika mpira refarii ndiye muamuzi wa mwisho, you need someone kuwa muamuzi wa mwisho ama sivyo utakuwa na chaos kila siku.

Sina tatizo na hii part ya katiba, kwa sababu kama si hivyo kila mtu atakayeshindwa urais ataenda mahakamani, halafu urais utakuwa a joke, utakuwa paralysed. This is not the way to go.

Tatizo langu mimi si kwamba refarii ndiye muamuzi wa mwisho, tatizo langu ni kwamba timu moja inachagua refarii. Rais anachagua Tume ya uchaguzi, hapa ndipo nilipo na tatizo napo. Kama tungekuwa na tume iliyo impartial hata kusingekuwa na issue.

well said Kiranga..ni kama umelima shamba lakoa la mahindi ukamwambia nyani akutafutie walinzi walilinde , ni lazima ata wachagua nyani wenzake waje walilinde au mingedere na hata sku moja hawezi kumteua binadamua au simba aje alinde pale
 
Well Said. Kwanini Wananchi Wamtambue Kikwete Wakati Hii Tume ni Msemaji wa Mwisho. Tume Imeteuliwa na Mgombea Uraisi na Wanachama wa CCM. Hakuna Nafasi ya kuchallange Matokeo Kwenye Vituo na Majibu Kutoelewa Baada ya Wiki. Uchaguzi ni nini? Tanzania Imejiunga na Mataifa Haya Yafuatayo: Zimbabwe, Uganda, Rwanda, Kenya, Egypt, Libya, Burma, North Korea na Venezuela. Kwa Hili Tunawapongeza CCM. Wananchi Nje ya Inchi Tafuteni Schedule ya Kikwete kisafiiri Nje ya Inchi, Tutampa Habari Yake.
 
...................wabunge wajaribu kumpigia rais kura ya no confidence, bunge liwe dissolved na chaguzi zote a ubunge na urais zirudiwe......................

Baada ya Chadema kutoa tamko lao la kutomtambua JK...............inabidi sasa waandae hoja ya vote of no confidence.................safi kabisa....

Si sahihi kusema ukikubali kuwa mbunge..................then umemkubali Rais..............na ndio maana kuna nafasi kama ya vote of no confidence.............

ni sahihi kusema......itakuwa difficult ku-operate kama mbunge usipomtambua Rais.............
 
Back
Top Bottom