Elections 2010 CHADEMA yatoa tamko: Hatumtambui Kikwete kama rais

Kama CHADEMA hawamtambui Rais:
1. Watashiriki kupiga kura za kumpitisha/kutompitisha waziri mkuu? Waziri mkuu hupendekezwa na Rais, kushiriki katika kumpigia kura ni kutambua huyo aliyemleta ni Rais halali.

2. Baada ya waziri mkuu kupitishwa, wataweza kumuuliza mwaswali yeye pamoja na mawaziri wengine, ambao wote wameteuliwa na Rais wasiyemtambua?

Ndugu zangu wana JF, tamko hili la CHADEMA ni la kisiasa tu na halitekelezeki. Sababu kubwa ni kwamba wabunge wa CHADEMA hawawezi kugive-up ubunge wao - kwa katiba ya Tanzania kama humtambui Rais huwezi kuwa mbunge.

- Great post bro!, Chadema wamefanya kazi nzuri sana kwenye huu uchaguzi kwa sababu wame-expose weaknesess za uongozi wa CCM kila kona kitu ambacho kitawapa nafasi CCM kujirekebisha au huenda ukawa ndio mwisho wa empire,

- Binafsi siamini kwamba Chadema watasimamia msimamo wa kutomtambua Rais aliyeapishwa tayari, kwa sababu itaishia kuvuruga kazi kubwa na nzuri waliyoifanya tayari, kwa maoni yangu ni kwamba kwa msimamo kama huu watakuwa wanajitafutia un-necessary national political attention ambayo itawapa mwanya maadui wao kisiasa kuwaingia kati kati, kuwagawa na wataishia kufarakana kama enzi za TLP na NCCR na CUF kule visiwani

- Chadema chonde chonde wananchi tunwahitaji sana sasa kuliko wakati wowote uliopita, kumkosesha tembo usingizi huu mwendo wa kutotambuana haujakaa sawa!


William.
 
- Great post bro!, Chadema wamefanya kazi nzuri sana kwenye huu uchaguzi kwa sababu wame-expose weaknesess za uongozi wa CCM kila kona kitu ambacho kitawapa nafasi CCM kujirekebisha au huenda ukawa ndio mwisho wa empire,

- Binafsi siamini kwamba Chadema watasimamia msimamo wa kutomtambua Rais aliyeapishwa tayari, kwa sababu itaishia kuvuruga kazi kubwa na nzuri waliyoifanya tayari, kwa maoni yangu ni kwamba kwa msimamo kama huu watakuwa wanajitafutia un-necessary national political attention ambayo itawapa mwanya maadui wao kisiasa kuwaingia kati kati, kuwagawa na wataishia kufarakana kama enzi za TLP na NCCR na CUF kule visiwani

- Chadema chonde chonde wananchi tunwahitaji sana sasa kuliko wakati wowote uliopita, kumkosesha tembo usingizi huu mwendo wa kutotambuana haujakaa sawa!


William.

Nakubaliana na wewe William.
 
- Great post bro!, Chadema wamefanya kazi nzuri sana kwenye huu uchaguzi kwa sababu wame-expose weaknesess za uongozi wa CCM kila kona kitu ambacho kitawapa nafasi CCM kujirekebisha au huenda ukawa ndio mwisho wa empire,

- Binafsi siamini kwamba Chadema watasimamia msimamo wa kutomtambua Rais aliyeapishwa tayari, kwa sababu itaishia kuvuruga kazi kubwa na nzuri waliyoifanya tayari, kwa maoni yangu ni kwamba kwa msimamo kama huu watakuwa wanajitafutia un-necessary national political attention ambayo itawapa mwanya maadui wao kisiasa kuwaingia kati kati, kuwagawa na wataishia kufarakana kama enzi za TLP na NCCR na CUF kule visiwani

- Chadema chonde chonde wananchi tunwahitaji sana sasa kuliko wakati wowote uliopita, kumkosesha tembo usingizi huu mwendo wa kutotambuana haujakaa sawa!

William.

Kimsingi waliomkataa Jk SIYO Chadema bali ni wananchi walioibiwa kura zao, Chadema wanachofanya ni kuwakilisha tu msimamo wa wapiga kura ambao hawana imani naye hata tume ndiyo maana wananchi wanalinda kura zao wakizunguka ofisi ya kuhesabia kura hata siku mbili bila kulala. .
 
Kama CHADEMA hawamtambui Rais:
1. Watashiriki kupiga kura za kumpitisha/kutompitisha waziri mkuu? Waziri mkuu hupendekezwa na Rais, kushiriki katika kumpigia kura ni kutambua huyo aliyemleta ni Rais halali.

2. Baada ya waziri mkuu kupitishwa, wataweza kumuuliza mwaswali yeye pamoja na mawaziri wengine, ambao wote wameteuliwa na Rais wasiyemtambua?

Ndugu zangu wana JF, tamko hili la CHADEMA ni la kisiasa tu na halitekelezeki. Sababu kubwa ni kwamba wabunge wa CHADEMA hawawezi kugive-up ubunge wao - kwa katiba ya Tanzania kama humtambui Rais huwezi kuwa mbunge.

Wacha uongo weka hapa hicho kifungu cha sheria.
 
Kama CHADEMA hawamtambui Rais:
1. Watashiriki kupiga kura za kumpitisha/kutompitisha waziri mkuu? Waziri mkuu hupendekezwa na Rais, kushiriki katika kumpigia kura ni kutambua huyo aliyemleta ni Rais halali.

2. Baada ya waziri mkuu kupitishwa, wataweza kumuuliza mwaswali yeye pamoja na mawaziri wengine, ambao wote wameteuliwa na Rais wasiyemtambua?

Ndugu zangu wana JF, tamko hili la CHADEMA ni la kisiasa tu na halitekelezeki. Sababu kubwa ni kwamba wabunge wa CHADEMA hawawezi kugive-up ubunge wao - kwa katiba ya Tanzania kama humtambui Rais huwezi kuwa mbunge.

Siyo lazima Chadema watumie mantiki unayotumia wewe kumkubali au kumkataa waziri mkuu. Kitu unachopaswa kufahamu ni kuwa kimsingi waliomkaa JK ni wananchi ambao wameibiwa kura zao. Kura zilizoibiwa siyo za Chadema bali wapiga kura. Ndio walioamua kmpigia kura Slaa. Kwa hivyo Chadema wanawakilisha tu msimamo wa wananchi kutomtambua JK. Halafu unatakiwa kujua kuwa hao wabunge wa Chadema siyo wa Chadema kama unavyofikiria wewe ni wabunge wa wananchi na tumewatuma kazi ya kufanya bungeni. Kwa hiyo siyo suala la kusema Chadema waache ubunge wao. Ni juu ya sisi wananchi kuamua, sisi twananchi utasema hatutambui JK na Chadema wanawakilisha uamuzi wa wananchi. Chadema waendelee kupambana huko bungeni, ndiyo tulivyowatuma wapiga kura. Siyo juu ya Chadema kuacha ubunge ni juu ya wananchi waliowachagua kuamua, wananchi wameamua waendelee bungeni bali rais hatambuliwi.
 
Siyo lazima Chadema watumie mantiki unayotumia wewe kumkubali au kumkataa waziri mkuu. Kitu unachopaswa kufahamu ni kuwa kimsingi waliomkaa JK ni wananchi ambao wameibiwa kura zao. Kura zilizoibiwa siyo za Chadema bali wapiga kura. Ndio walioamua kmpigia kura Slaa. Kwa hivyo Chadema wanawakilisha tu msimamo wa wananchi kutomtambua JK. Halafu unatakiwa kujua kuwa hao wabunge wa Chadema siyo wa Chadema kama unavyofikiria wewe ni wabunge wa wananchi na tumewatuma kazi ya kufanya bungeni. Kwa hiyo siyo suala la kusema Chadema waache ubunge wao. Ni juu ya sisi wananchi kuamua, sisi twananchi utasema hatutambui JK na Chadema wanawakilisha uamuzi wa wananchi. Chadema waendelee kupambana huko bungeni, ndiyo tulivyowatuma wapiga kura. Siyo juu ya Chadema kuacha ubunge ni juu ya wananchi waliowachagua kuamua, wananchi wameamua waendelee bungeni bali rais hatambuliwi.

Asante kwa ufafanuzi wako. Swali langu kuu ni utekelezaji wa kutokumtambua Rais. je, kutokumtambua kwao kutakuwa kwa maneno tu mbele ya waandishi wa habari? kama hivyo ndivyo walivyopanga kufanya basi sawa, lakini hiyo ni siasa tu na haitakuwa na manufaa yoyote kwa mtanzania aliyeambiwa kura yake imeibiwa.
 
Kimsingi waliomkataa Jk SIYO Chadema bali ni wananchi walioibiwa kura zao, Chadema wanachofanya ni kuwakilisha tu msimamo wa wapiga kura ambao hawana imani naye hata tume ndiyo maana wananchi wanalinda kura zao wakizunguka ofisi ya kuhesabia kura hata siku mbili bila kulala. .

- Sawa sawa mkuu, je tunaweza kujadili faida na hasara za kitendo? Ukianza na faida kwanza kwa wananchi halafu kwa wawakilishi wao Chadema?


William.
 
- Sawa sawa mkuu, je tunaweza kujadili faida na hasara za kitendo? Ukianza na faida kwanza kwa wananchi halafu kwa wawakilishi wao Chadema?


William.

Asante sana kiongozi. Maswali yako haya ndio yanapaswa kuwa msingi mkuu wa thread hii.
Again, asante.
 
Asante kwa ufafanuzi wako. Swali langu kuu ni utekelezaji wa kutokumtambua Rais. je, kutokumtambua kwao kutakuwa kwa maneno tu mbele ya waandishi wa habari? kama hivyo ndivyo walivyopanga kufanya basi sawa, lakini hiyo ni siasa tu na haitakuwa na manufaa yoyote kwa mtanzania aliyeambiwa kura yake imeibiwa.

Nataka nikuambie kuwa Chadema hawajaongea na waandishi wa habari bali wananchi. Wananchi ndiyo wanataka Chadema wawawakilishe wananchi kusema wazi mzimamo wa wananchi kukataa kuibiwa kura ili kila mtu ajue uchaguzi wa JK umehusisha wizi wa kura za wananchi. Sisi wananchi ndiyo tumeamua mwizi asemwe hadharani, mbele ya safari sisi wananchi tutaamua tutanye kitu gani zaidi na tutawaamuru Chadema watekeleze pamoja nasi.
 
Wakuu tukate issue hapa mambo ya katiba na ubunge etc ni uongo au siyo? Wacheni danadana hapa? ZeMarcopolo unasemaje kuhusu maneno yako haya: ''kwa katiba ya Tanzania kama humtambui Rais huwezi kuwa mbunge.'' yametoka kwenye katiba au kichwani mwako?
 
- Sawa sawa mkuu, je tunaweza kujadili faida na hasara za kitendo? Ukianza na faida kwanza kwa wananchi halafu kwa wawakilishi wao Chadema?


William.

Hakuna hasara bali faida tu. Kiongozi anawekwa na wananchi, kama amejiweka anaondolewa na wananchi.
 
Wakuu tukate issue hapa mambo ya katiba na ubunge etc ni uongo au siyo? Wacheni danadana hapa? ZeMarcopolo unasemaje kuhusu maneno yako haya: ''kwa katiba ya Tanzania kama humtambui Rais huwezi kuwa mbunge.'' yametoka kwenye katiba au kichwani mwako?

Wacha1 wala usihangaike. Hata kama ingekuwepo, bado katiba haimrihusu mgombea wa urais kuiba kura. Kwa hivyo wapiga kura wanamadaraka zaidi juu ya rais na hiyo katiba, wanaweza kuamua kumwondoa rais na kuibadilisha Katiba
 
Wakuu tukate issue hapa mambo ya katiba na ubunge etc ni uongo au siyo? Wacheni danadana hapa? ZeMarcopolo unasemaje kuhusu maneno yako haya: ''kwa katiba ya Tanzania kama humtambui Rais huwezi kuwa mbunge.'' yametoka kwenye katiba au kichwani mwako?

Strictly speking, rais ni sehemu moja ya bunge kwa mujibu wa katiba. Maana yake bunge halikamiliki bila rais, kwa hiyo ukikubali kuwa mbunge umelitambua bunge, na ukilitambua bunge umemtambua rais ambaye ni sehemu ya bunge.

Haya ndiyo mabadiliko ya katiba yanyotakiwa kufanywa. Huwezi kuwa na mihimili mitatu ya taifa, bunge, mahakama na uongozi, halafu kiongozi wa uongozi (rais) akawa ni sehemu moja nzima ya bunge, I mean rais hata si mbunge, ni sehemu nzima ya bunge ! Where are the checks and balances here ? Wakati kama huu ndio ungekuw mzuri kwa wabunge wa CHADEMA kuonyesha hawana imani na rais, lakini hawawezi, kwa sababu ili kuwa wabunge inawalazimu kumtambua rais.

Kwa hiyo ukienda kwa katiba, kama kweli humtambui rais, huwezi kuwa mbunge.
 
Hakuna hasara bali faida tu. Kiongozi anawekwa na wananchi, kama amejiweka anaondolewa na wananchi.

- Wananchi? Kama ni kweli mkuu wangeshaandamana I mean it works both ways huwezi kuwawakilisha wananchi ambao hawajaandamana kupinga matokeo ya uchaguzi, Unless una evidence ya wananchi kuiomba Chadema on the ishu?

- I mean Rais anawekwa na wananchi kwa mujibu wa katiba, kama katiba imevunjwa si kuna sheria ambayo ingeweza kutumika kuzuia asiapishwe au?

William.
 
Strictly speking, rais ni sehemu moja ya bunge kwa mujibu wa katiba. Maana yake bunge halikamiliki bila rais, kwa hiyo ukikubali kuwa mbunge umelitambua bunge, na ukilitambua bunge umemtambua rais ambaye ni sehemu ya bunge.

Haya ndiyo mabadiliko ya katiba yanyotakiwa kufanywa. Huwezi kuwa na mihimili mitatu ya taifa, bunge, mahakama na uongozi, halafu kiongozi wa uongozi (rais) akawa ni sehemu moja nzima ya bunge, I mean rais hata si mbunge, ni sehemu nzima ya bunge ! Where are the checks and balances here ? Wakati kama huu ndio ungekuw mzuri kwa wabunge wa CHADEMA kuonyesha hawana imani na rais, lakini hawawezi, kwa sababu ili kuwa wabunge inawalazimu kumtambua rais.

Kwa hiyo ukienda kwa katiba, kama kweli humtambui rais, huwezi kuwa mbunge.

Kuna kitu kinasahaulika. Msingi wa madaraka yote ya nchi ni wananchi. Kusema kuwa wabunge wakimkataa rais hawawezi kuwa wabunge ni sawa na kusema kuwa wananchi wakimkataa rais hawezi kuwa wananchi. Mbunge ni mwananchi, usiangalie mbunge kwa kumtofautisha na wananchi, kwa sababu ni mwakilishi wao. Kwa hivyo kama mgombea wa urais amewaibia wapiga kura ambao ni wananchi wanauwezo wa kumkataa. Siyo kinyume chake, ni kuwa wananchi wanaweza kumkataa rais, siyo rais kuwakataa wananchi kwa sababu rais hana madaraka zaidi ya wananchi. Kwa hivyo rais hana madaraka juu ya wabunge kwa kuwa wabunge maana yake ni wananchi.
 
- Wananchi? Kama ni kweli mkuu wangeshaandamana I mean it works both ways huwezi kuwawakilisha wananchi ambao hawajaandamana kupinga matokeo ya uchaguzi, Unless una evidence ya wananchi kuiomba Chadema on the ishu?

- I mean Rais anawekwa na wananchi kwa mujibu wa katiba, kama katiba imevunjwa si kuna sheria ambayo ingeweza kutumika kuzuia asiapishwe au?

William.

Tanzania hamna katiba wala heria, ni show tupu.

Ndiyo maana tunataka mabailiko ya katiba. Huwezi kuwa na true checks and balances kama rais ni sehemu nzima ya bunge, not even mbunge, sehemu nzima ya bunge.
 
- Tanzania kikatiba tunayo mihimili mitatu yaani Bunge, Ikulu, na Mahakama, ninaamini on this one kwamba tatizo hapa sio katiba isipokuwa ni sisi wananchi na hasa wanaopewa nafasi kuongoza hiyo mihimili hasa ya mahakama na Bunge, wamekuwa waoga waoga na wasiojiamini, sasa hili linakuwaje tatizo la katiba?

- I mean ni bunge kwa kutumia katiba ndilo lililowaondoa viongozi waliokuwa wanatuhumiwa na Richmond, na wale viongozi walikuwa ni part ya Ikulu, yaani Executive Branch, lakini baada ya pale tumeona viongozi wa bunge waliosimamia katiba walivyochafuliwa kwamba hawafai na wengine mpaka kutaka kufukuzwa vyama vyao vya siasa, wananchi tumenyamaza kimyaa!

Eti kwenye mihimili mitatu kuna tatizo la katiba?



William.
 
Kuna kitu kinasahaulika. Msingi wa madaraka yote ya nchi ni wananchi. Kusema kuwa wabunge wakimkataa rais hawawezi kuwa wabunge ni sawa na kusema kuwa wananchi wakimkataa rais hawezi kuwa wananchi. Mbunge ni mwananchi, usiangalie mbunge kwa kumtofautisha na wananchi, kwa sababu ni mwakilishi wao. Kwa hivyo kama mgombea wa urais amewaibia wapiga kura ambao ni wananchi wanauwezo wa kumkataa. Siyo kinyume chake, ni kuwa wananchi wanaweza kumkataa rais, siyo rais kuwakataa wananchi kwa sababu rais hana madaraka zaidi ya wananchi. Kwa hivyo rais hana madaraka juu ya wabunge kwa kuwa wabunge maana yake ni wananchi.

Sawa,

Lakini kama alivyokuuliza William hapo juu, wananchi wanafanya nini? Wanaandamana? Na kama hawaandamani CHADEMA watasemje kwamba Kikwete ni mwizi wa kura ambaye wananchi hawamtaki? Tutajuaje kama CHADEMA si walalmishi tu wsiokubali kushindwa?

Natetea mabadiliko ya katiba ili haya mambo yote yawe addressed formally kisheria, sio kwa ulalamishi ambao hauwezi hata kuwa proven.

Tubadilishe katiba, NEC isiwe inachaguliwa na rais, rais asiwe sehemu ya bunge -tayari Waziri Mkuu anaiwakilisha serikali bungeni- then katika situation kama hii wbunge wa CHADEMA na CUF na wangeweza kuendelea kuwa wabunge bila kumtambua rais.

Lakini sasa hivi kukubali ubunge ni kumtambua rais.

Ama sivyo wabunge wajaribu kumpigia rais kura ya no confidence, bunge liwe dissolved na chaguzi zote a ubunge na urais zirudiwe.

Kama wana huo moyo na wanaweza kupata support ya CCM.
 
- Tanzania kikatiba tunayo mihimili mitatu yaani Bunge, Ikulu, na Mahakama, ninaamini on this one kwamba tatizo hapa sio katiba isipokuwa ni sisi wananchi na hasa wanaopewa nafasi kuongoza hiyo mihimili hasa ya mahakama na Bunge, wamekuwa waoga waoga na wasiojiamini, sasa hili linakuwaje tatizo la katiba?

- I mean ni bunge kwa kutumia katiba ndilo lililowaondoa viongozi waliokuwa wanatuhumiwa na Richmond, na wale viongozi walikuwa ni part ya Ikulu, yaani Executive Branch, lakini baada ya pale tumeona viongozi wa bunge waliosimamia katiba walivyochafuliwa kwamba hawafai na wengine mpaka kutaka kufukuzwa vyama vyao vya siasa, wananchi tumenyamaza kimyaa!

Eti kwenye mihimili mitatu kuna tatizo la katiba?



William.

Tatizo la katiba kwa sababu katiba inampa nguvu rais kama mungumtu, rais anateua kuanzia wabunge, majaji mpaka mawaziri.Kwa maana nyingine mihimili mitatu hii inatakiwa kuweka checks and balances, lakini rais ndiye anayeisimamisha, sasa checks and balances zitatoka wapi?

Rais huyo huyo ni sehemu ya bunge.

Rais huyo huyo practically yuko juu ya sheria.

Rais huyo huyo akitaka kumfunga mtu yeyote bila maelezo yoyote kwa kipindi chochote anachotaka kama rais anaweza.

Rai huyo huyo akitaka kuchukua ardhi yoyote ya Jamhuri, na kuitumia kwa sababu zozote anazotaka yeye anaruhusiwa kisheria.

Wewe unaona katiba sawa hii?
 
Back
Top Bottom